"Kimbunga kutua Ijumaa alfajiri"
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) imetoa taarifa mpya juu ya mwenendo wa kimbunga Kenneth na kusema kuwa kinatarajiwa kutua Ijumaa alfajiri au asubuhi.
Katika Taarifa ya video iliyopakiwa kwenye mtandao wa kijamii wa You Tube, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt Agness Kijazi amesema kufikia sa tisa mchana wa leo kimbunga kitakuwa umbali wa kilomita 177 kutoka pwani ya Mtwara kikiwa na kasi ya kilometa 140 kwa saa.
Kutokana na kasi hiyo kimbunga kinatarajiwa kutua nchini Msumbiji kuanzia Alfajiri ya Ijumaa kikiwa na kasi kilomita 100 kwa saa.
Hata hivyo, kitakapotua kimbunga hicho ni karibu na mpaka wa Tanzania kwa kilomita 230, na athari zake zinatarajiwa kukumba maeneo yaliyo ndani ya kilomita 600.
"Nchini mwetu, maeneo ya mpaka Lindi na Ruvuma yataathirika sana," amesema Kijazi na kuongeza, "wakazi hususani wa Mtwara kwa sasa wanaweza wakaona tu kuna mvua zinanyesha lakini waendelee kuchukua tahadhari. Kadri muda unavyosidi kusonga ndiyo kimbunga kinazidi kukaribia nchi kavu."
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa YouTube ujumbe















