Tutadhibiti Mlango bahari wa Hormuz-Trump
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa Marekani "huenda ikaudhibiti" Mlango wa Bahari wa Hormuz, akidai kwamba Iran "imevunja" makubaliano yaliyokuwa yamefikiwa kati ya nchi hizo mbili.
Akizungumza na kituo cha habari cha Fox News, Trump amesema:
"Tunachukua udhibiti wa mlango huo wa bahari. Hawana chochote. Hawana kitu."
Pia amesema kwamba Marekani ilishambulia Iran kwa nguvu kubwa usiku uliopita, akirejelea mashambulizi kadhaa yaliyofanywa na Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) dhidi ya mali na vifaa vya kijeshi nchini Iran.
Trump ameongeza:
"Tunawadhibiti. Wako katika hali ngumu. Sehemu kubwa ya vifaa vyao vya kijeshi imeharibiwa. Mifumo yao ya ulinzi wa anga imeondolewa."
Mapema Jumatatu, Ubalozi wa Iran nchini Uingereza ulisema kuwa Iran imeanzisha ukanda wa muda wa usalama wa usafiri wa baharini, ambao ni bila vikwazo vya kiufundi na vya kijeshi, katika Mlango wa Bahari wa Hormuz ili kuruhusu meli kupita kwa usalama.
Hata hivyo, ubalozi huo ulisema kuwa hatua za kijeshi za Marekani zimeugeuza Mlango wa Bahari wa Hormuz kuwa eneo lenye hatari kubwa, na hivyo kuongeza wasiwasi kuhusu usalama wa usafiri wa baharini katika eneo hilo.
Unaweza kusoma;