HRW yaishutumu Mamlaka ya Tigray kwa kuajiri watu kwa nguvu jeshini
Shirika la kutetea hazi za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeri poti kwamba mamlaka za kikanda katika eneo la kaskazini mwa Tigray nchini Ethiopia zimekuwa zikiwateka nyara na kuwaajiri raia kinyume cha sheria, watoto wenye umri wa miaka 15, tangu Aprili 2026.
Harakati ya kuajiri inafuatia miezi kadhaa ya mvutano unaoongezeka kati ya serikali ya shirikisho ya Ethiopia na Tigray People’s Liberation Front (TPLF).
Katika taarifa iliyotolewa 6 Julai 2026, shirika hilo linasema kwamba jamii katika miji na vijiji zinasema vikosi na maafisa wa Tigray wanawakamata wapiganaji wa zamani na wanaume na wavulana kutoka mitaani, ofisini, majumbani wakati wa upekuzi wa usiku, na maeneo ya kuchimba dhahabu.
"Kampeni ya mamlaka ya Tigray ya kuwaajiri wanaume na wavulana kwa nguvu katika vikosi vyao inaunda hali ya hofu katika eneo lote," anasema Laetitia Bader, naibu mkurugenzi wa Afrika wa HRW.
"Mamlaka inapaswa kukomesha kampeni yao mara moja na kuwaruhusu wale walioajiriwa kinyume cha sheria kurudi nyumbani."
HRW imeekodi visa sita vya kulazimishwa kuajiriwa kupitia mahojiano ya mbali na watu 18 mwezi Juni, wakiwemo mashahidi, jamaa za wapiganaji walioandikishwa jeshini, na wale waliotoroka baada ya kutekwa nyara.
Waliohojiwa wamesema kuwa msako mkubwa uliongezeka mwishoni mwa Aprili, huku mamlaka za mitaa zikitumia orodha ya wapiganaji wa zamani na watoa taarifa wa maeneo ili kuwatambua wapiganaji walioandikishwa jeshini.
Inaripotiwa kwamba wapiganaji wapya walishikiliwa katika ofisi za utawala, magereza, au shule kabla ya kuhamishiwa kwenda kwenye kambi za kijeshi kaskazini magharibi na kusini mwa Tigray.
Kundi hilo la haki za binadamu limetoa wito kwa Umoja wa Afrika, pamoja na serikali zilizounga mkono makubaliano ya Pretoria ya 2022, Marekani, na Umoja wa Ulaya, kuishinikiza mamlaka ya Tigrayan kusitisha kulazimishwa kuajiriwa jeshini, kuwaachilia watoto wote na watu walioandikishwa jeshini kinyume cha sheria, na kuondoa tangazo hilo.