Massive Attack watoa tamko baada ya Singapore kupiga marufuku onyesho lao kuhusu Palestina
Kundi la Massive Attack limesema lilishangazwa na kukatishwa tamaa na jinsi mamlaka za Singapore zilivyolichukulia baada ya kuonyesha uungaji mkono kwa Palestina wakati wa onyesho katika jiji la taifa hilo.
Kundi hilo liliandika kwenye Instagram siku ya Jumapili kwamba wanachama wake "walizuiliwa na polisi, kutengwa na kuhojiwa kivyao," huku wengine wakikabiliwa na upekuzi wa vyumba vyao vya hoteli na kunyang'anywa pasipoti kwa muda.
Wanachama wawili wa kundi hilo walinyanyua bendera ya Palestina wakati wa onyesho lao la tarehe 29 Julai na kupaza sauti wakisema "Palestina iwe huru" (free Palestine) pamoja na baadhi ya watu waliokuwa wakitazama onyesho hilo.
Singapore, ambayo ina sheria kali kuhusu hotuba za hadhara na mikusanyiko, baadaye ilitangaza kuwa imepiga marufuku kundi la Massive Attack kurejea nchini humo kwa muda usiojulikana.
Msemaji wa polisi aliambia BBC siku ya Ijumaa kuwa wanachama hao wawili wa kundi hilo hawangeruhusiwa kuingia tena Singapore na walipigwa marufuku kufanya maonyesho huko.
Robert Del Naja na Grant Marshall "waliopewa maonyo makali" kuhusiana na madai ya makosa chini ya sheria mbili zinazozuia kuonyeshwa hadharani kwa bendera za kigeni na kudhibiti kauli za kisiasa katika hafla za umma.
Massive Attack ilisema kuwa kabla ya onyesho na tena mwishoni mwake, "sehemu kubwa ya hadhira ilianza kwa hiari yao wenyewe kupaza sauti wakisema 'Palestina iwe huru', wakijua vyema lakini bila kuogopa kwamba kitendo hicho cha hiari kingeweza kukiuka sheria za udhibiti wa maoni za serikali yao".
Kundi hilo halikuzungumzia moja kwa moja marufuku hiyo, lakini lilielezea hali hiyo kama "tukio la ajabu lisilo la kawaida" na kusema kuwa "hawakudhani kwamba kitendo cha kunyanyua bendera ya taifa huru linalotambuliwa na nchi 157 kingeweza kukiuka sheria yoyote".Waliongeza kusema: "Anatoa onyesho linalohitaji nguvu nyingi za kimwili na ustadi wa hali ya juu wa kimichezo. Anafanya maonyesho hayo kwa kiwango cha juu sana, kwa mafanikio na akiwa na afya njema, usiku baada ya usiku."
Onyesho la mwisho la ziara hiyo limepangwa kufanyika tarehe 1 Septemba jijini London.