Watu 12 wahukumiwa kwa mashambulio ya mabomu

Shambulio la bomu mjini Mumbai

Chanzo cha picha, PTI

Maelezo ya picha, Shambulio la bomu mjini Mumbai
Iliyochapishwa

Mahakama moja nchini India, imewakuta wanaume kumi na mbili na hatia kwa kuhusika katika mashambulizi ya mabomu kwenye treni mjini Mumbai mwaka 2006.

Mtu mmoja hata hivyo aliondolewa mashtaka hayo na kuachiliwa huru.

Watu waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo

Chanzo cha picha, AP

Maelezo ya picha, Watu waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo

Zaidi ya watu mia moja themanini waliuwawa na mamia ya wengine kujeruhiwa wakati mabomu saba yalipolipuka kwenye treni za abiria.

India iliwashutumu wanamgambo wa Kiislamu, kutoka kundi la la Lashkar-e-taiba, lenye makaazi yake nchini Pakistan, kwa kutekeleza mashambulizi hayo madai ambayo Pakistan iliyakanusha.

Polisi wakichunguza kisa hicho

Chanzo cha picha, AP

Maelezo ya picha, Polisi wakichunguza kisa hicho