Maelezo ya picha, Wapiga kura walipanga foleni tangu mapema asubuhi katika vituo vya kupigia kura kote nchini Kenya
Iliyochapishwa
Ucheleweshaji wa vifaa na changamoto za utambulisho katika baadhi ya maeneo ya kulitia doa nchi siku ya uchaguzi ambao ulikuwa wa amani kwa kiasi kikubwa nchini Kenya.
Shughuli ya kuhesabu kura kwa sasa zinaendelea mara baada ya vituo vya kupiga kura kufungwa huku hesabu ya kura za urais ikipewa kipaumbele.
Kura hii inafuatia kampeni kali iliyotawaliwa na mijadala kuhusu gharama za maisha, ukosefu wa ajira na ufisadi.
Wanaogombea wakuu wa urais ni aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga na Naibu Rais wa sasa William Ruto.
Wakenya pia walikuwa wakichagua bunge jipya na tawala za mitaa.
Tume ya uchaguzi bado haijatangaza jumla ya waliojitokeza kupiga kura, lakini kufikia saa kumi jioni (13:00 GMT) - saa moja kabla ya uchaguzi kufungwa - zaidi ya 56% ya wapiga kura milioni 22 waliojiandikisha walikuwa wamepiga kura zao.
Afisa mkuu wa uchaguzi mjini Nyeri katika eneo la kati nchini Kenya aliwaambia wanahabari kwamba waliojitokeza kupiga kura katika eneo hilo walikuwa wachache ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2017.
Awali Bw Odinga alilakiwa na wafuasi wake alipoenda kupiga kura katika eneo la Kibra - moja ya ngome zake katika mji mkuu, Nairobi.
Hakuzungumza na waandishi wa habari, lakini mkewe, Ida Odinga, alisema "amefurahishwa na uchaguzi".
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Wagombea urais William Ruto (Kushoto) na Raila Odinga (Kulia) wamepiga kura
Bw Ruto alipopiga kura katika mji wa Eldoret uliopo eneo la Bonde la Ufa aliahidi kukubali matokeo ya uchaguzi.
"Nadhani kwa mara ya kwanza katika historia ya demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya, wagombea wote wamejitolea kukubali matokeo ya matokeo," aliambia BBC.
Mzozo kuhusu matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2007 ulisababisha ghasia za wiki kadhaa na kusababisha vifo vya takriban watu 1,200 na kuwalazimu takriban watu 600,000 kuyakimbia makazi yao.
Siku ya Jumanne, kulikuwa na hali ya kufadhaika miongoni mwa wapiga kura asubuhi na mapema katika kituo cha kupigia kura katika shule ya msingi ya eneo la Westlands jijini Nairobi.
Walizuiwa kuingia katika eneo la shule kwa dakika 90.
Chanzo cha picha, BBC/Peter Njoroge
Maelezo ya picha, Watu walikasirishwa na ucheleweshaji wa uchaguzi katika kituo kimoja cha kupigia kura katika mji mkuu, Nairobi
Kilichosababisha kucheleweshwa kwa shughuli hiyo hakikubainishwa lakini baadhi ya watu walianza kupiga mayowe wakisema: "Tunataka kupiga Kura!"
"Nilikuwa hapa mapema sana. Ni hali ya kukatisha tamaa kwamba tulifika hapa mapema na tulilazimika kusubiri kwa muda mrefu," mpiga kura Alex Kipchoge aliambia BBC.
Upigaji kura ulipoanza, hata hivyo, mchakato ulikwenda vizuri.
"Nilifurahi sana. Nimekuwa nikingojea hili kwa muda mrefu na nina furaha kwamba nimepata nafasi ya kupiga kura," mpiga kura wa mara ya kwanza Abigail Awili alisema.
Pia kulikuwa na ucheleweshaji katika eneo la pwani ya Mombasa na baadhi ya maeneo ya kaskazini-mashariki mwa nchi. Na katika sehemu za kaunti ya Kakamega, magharibi, baadhi ya vifaa vya kielektroniki vya kukagua alama za vidole vilishindwa kufanya kazi.
Lakini tume ya uchaguzi ilisema kuwa nchi nzima ni 200 pekee waliovunjika kati ya jumla ya zaidi ya 46,000.
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Wapiga kura walitambuliwa kwa alama za kidole gumba au vidole
Matokeo ya uchaguzi uliopita wa urais mwaka 2017 yalibatilishwa baada ya Mahakama ya Juu kutoa uamuzi kwamba tume ya uchaguzi haikufuata sheria lilipokuja suala la kuwasilisha matokeo kwa mfmo wa kielektroniki kutoka vituo vya kupigia kura.
Majaji waliamua kwamba "uvunjaji wa sheria na ukiukwaji" ulifanyika.
Uchaguzi wa marudio ulishindwa na Bw Kenyatta, lakini ukasusiwa na Bw Odinga - mgombea mkuu wa upinzani wakati huo.
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Wafula Chebukati ambaye pia alikuwa msimamizi wa kura ya 2017 amejaribu mara kwa mara kuwahakikishia Wakenya kwamba timu yake itatekeleza jukumu hilo wakati huu.
Baba v Hustler
Uchaguzi huu unaonekana kama utakuwa na kinyang'anyiro kikali kati ya wagombezi Bw Odinga, 77, na Bw Ruto, 55.
Bw Odinga - kiongozi wa upinzani wa muda mrefu, anayeitwa ''Baba'' na wafuasi wake, anawania urais kwa mara ya tano. Bw Ruto, ambaye amejaribu kusisitiza uhusiano wake na Wakenya wa kawaida kwa kujiita "hustler", anawania kiti cha urais kwa mara ya kwanza.
Wagombea wengine wawili - David Mwaure na George Wajackoya - pia wako kwenye kinyang'anyiro hicho.
Ili kushinda uchaguzi wa urais katika duru ya kwanza, mgombea anahitaji:
zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa kote nchini
angalau 25% ya kura zilizopigwa katika majimbo 24.
Baada ya kuhesabu kura, maafisa watapiga picha ya hesabu ya mwisho na kutuma picha hiyo kwa maeneo bunge na vituo vya kitaifa vya kujumlisha kura.
Ili kuhakikisha uwazi vyombo vya habari, vyama vya siasa na mashirika ya kiraia yamehimizwa kuendesha hesabu zao kwa kutumia matokeo ya mwisho yaliyotangazwa katika vituo zaidi ya 40,000 vya kupigia kura.
Lakini tume ya uchaguzi pekee ndiyo inayoweza kutangaza mshindi wa uchaguzi wa urais baada ya kuthibitisha fomu halisi na za kidijitali zinazotumwa kwa kituo cha kitaifa cha kuhesabia kura.
Ina siku saba kutangaza matokeo.
Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?
Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya
Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake
Raila Amollo Odinga
Muungano wa Azimio la Umoja
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.
William Samoei Ruto
Muungano wa Kenya Kwanza
Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC
George Wajackoyah
Chama cha Roots
Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito
David Mwaure Waihiga
Chama cha Agano
David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
Kupambana na ufisadi uliokithiri.
kuunda nafasi za ajira.
Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.
Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa