Uchaguzi Kenya 2022: Watawala wa kurithi dhidi ya Watafutaji

Kenyans

Chanzo cha picha, AFP

    • Author, Evelyne Musambi
    • Nafasi, BBC News, Nairobi
  • Iliyochapishwa

Katika hatua inayofanana ya Trump ya kumuunga mkono Clinton katika uchaguzi wa Marekani, Rais wa Kenya anayeondoka  Uhuru Kenyatta anataka kumkabidhi taji la siasa hasimu wake aliyegeuka kuwa rafiki Raila Odinga  - lakini anamshuhudia naibu wake William Ruto akijaribu kunyakua taji hilo katika uchaguzi wa tarehe 9 Agosti. 

Imepelekea kuwepo kwa mchezo wa kuigiza ambapo Bw Ruto anajitaja kama  "hustler" au mtu aliyetafuta, anayepambana  na kile anachokiona kama  jaribio la kuendelezwa kwa ungozi wa mkubwa zaidi wa kuruthi wa-  Familia ya Kenyatta na ya Odinga -ili uendelee kubakia mamlakani.   

Akijaribu kupata huruma kutokakwa Wakenya, Ruto, amekuwa akifanya maombi, kuangua kilio, na kutoa madai makali kwamba Rais Kenyatta anamtisha. 

 "Ili mradi usiue watoto wangu nitakiukabili lakini wacha tuheshimiane," Bw   Ruto alisema, katika moja ya kampeni zake za mwisho huku umati ukimshangilia.

Akipinga madai yake, Bw Kenyatta alisema: "Umenitukana kwa karibu miaka mitatu. Kuna mtu aliyekugusa ?"Malumbano yao yalionyesha  jinsi hasira ilivyotawala kampeni za uchaguzi, huku Bw kenyatta akijitokeza kumuunga mkono Bw  Odinga kama mrithi wake.

"Rais amekwenda kinyume na mwelekeo wa lengo la Ruto, kulumbana naye, na kusahau kuhusu mshindani wake ," mchambuzi wa kisiasa wa Kenya  Profesa Masibo Lumala ameiambia  BBC.

 "Rais ameweza kuonyesha wazi upande wa naibu wake ambao unaonyesha hasira yake, jambo ambalo sio kitu kizuri ," aliongeza.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Naibu Rais William Ruto alikosana na Rais Uhuru Kenyatta wakati wa muhula wa pili. Mchambuzi mwingine Profesa Macharia Munene alisema kuwa malumbano haya makali yalimfanya Odinga'' kuonekana kama mtu mwenye umakini zaidi" wakati wa kampeni, ingawa alipata mapigo kutoka kwa Bw Ruto, akihoji madai yake ya kuwa ''hustler'' akimtaja kuwa "mwanaume wa ardhi nyingi" - akimaanisha utata wa muda mrefu kuhusu jinsi naibu rais alivyokuwa mmiliki mkubwa wa ardhi nchini Kenya. Alikana kunyakua ardhi kinyume cha sheria.

Naibu Rais William Ruto alikosana na Rais Uhuru Kenyatta wakati wa muhula wa pili.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Naibu Rais William Ruto alikosana na Rais Uhuru Kenyatta wakati wa muhula wa pili.

Mchambuzi mwingine Profesa Macharia Munene alisema kuwa malumbano haya makali yalimfanya Odinga'' kuonekana kama mtu mwenye umakini zaidi" wakati wa kampeni, ingawa alipata mapigo kutoka kwa Bw Ruto, akihoji madai yake ya kuwa ''hustler'' akimtaja kuwa "mwanaume wa ardhi nyingi" - akimaanisha utata wa muda mrefu kuhusu jinsi naibu rais alivyokuwa mmiliki mkubwa wa ardhi nchini Kenya. Alikana kunyakua ardhi kinyume cha sheria.

Hatua ya Rais kumuunga mkono Bw Odinga kutaka kukumbukwa kwa kuunganisha familia mbili ambazo ziliungana kupigana na utawala wa mkoloni Muingereza - lakini baadaye zikakosana mwaka 1966, miaka mitatu baada ya uhuru, na kuendelea kupambana hadi kufikia muhula wake wa pili na wa mwisho.

Ilimaanisha kuwa Bw Ruto, ambaye aliunde naye Muungano katika uchaguzi wa mwaka 2013 ukabiliana na mashitaka katika Mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC) juu ya ghasia za mauaji zilizoikumba Kenya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

"Kile kilichokuwa kimewaunganisha kilitoweka ," Profesa Munene alisema, akiongeza kuwa: "Sasa Ruto anataka kuchaguliwa na Uhuru anataka kukumbukwa kwa aliyoyafanya sasa nia maslahi yao yamegongana ."

Bw Kenyatta alifanya mageuzi ya kushirikiana na Bw Odinga baada ya mzozo wa uchaguzi wa mwaka 2017. Akikataa matokeo, Bw Odinga alikuwa ametoa wito wa kusia kampuni kadhaa, ikiwemo ile inayohusiana na familia ya Kenyatta, na kujitangaza kama "rais wa watu" katika mkutano mkubwa katika mji mkuu Nairobi.

"Uhuru alilazimika kumpokea raila Odinga kwasbabu alikuwa na uwezo wa kusababisha matatizo na kuvuruga kazi yake ," Profesa Munene alisema, na kuongeza kuwa Odinga mwenye umri wa miaka 77 mwanasiasa mkongwe alikubali wito wa Bw Kenyatta kwasababu uliongeza uwezekano wa kuwa rais baada ya kushindwa jaribio hilo kwa mara ya nne.

"Bw Odinga anaonekana kuwa anataka sana kuwa rais kwasababu ya umri wake, na hii inaonekana kuwa fursa yake ya mwisho ," anasema profesa Munene.

Raila Odinga amemchagua Waziri wa zamani wa sheria Martha Karua kama mgombea mwenza

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Raila Odinga amemchagua Waziri wa zamani wa sheria Martha Karua kama mgombea mwenza

Familia za Kenyatta na Odinga ni matajiri wa kupindukia. Thamani ya utajiri wao haijulikani wazi, lakini umma ulidokezewa kuhusu utajiri wa familia ya Kenyatta wakati nyaraka za Pandora zilizowahusisha na uwekezaji wa kampuni ya kigeni , ikiwa ni pamoja na hisa na hawala za thamani yad ola milioni 30 (Pauni milioni 22 )

Bw Ruto pia ni tajiri, lakini amekuwa akijionyesha kama mtu ambaye - wakati mmoja aliuza kuku na karanga kando ya barabara - anayefahamu maisha ya taabu wanayopitia masikini, na mtu atayayejali maslahi yao iwapo atachaguliwa.

Raila Odinga amemchagua Waziri wa zamani wa sheria Martha Karua kama mgombea mwenza.

Familia za Kenyatta na Odinga ni matajiri wa kupindukia. Thamani ya utajiri wao haijulikani wazi, lakini umma ulidokezewa kuhusu utajiri wa familia ya Kenyatta wakati nyaraka za Pandora zilizowahusisha na uwekezaji wa kampuni ya kigeni , ikiwa ni pamoja na hisa na hawala za thamani ya dola milioni 30 (Pauni milioni 22 ) .

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Bw Ruto pia ni tajiri, lakini amekuwa akijionyesha kama mtu ambaye - wakati mmoja aliuza kuku na karanga kando ya barabara - anayefahamu maisha ya taabu wanayopitia masikini, na atayajali maslahi yao iwapo atachaguliwa.

Huku wanawake wakiwa ni hadi karibu nusu ya idadi ya wapigakura waliojisajiri, Bw Odinga, tofauti na Ruto, amemchagua mgombea mwenza mwanamke, Waziri wa zamani wa sheria Martha Karua.

Profesa Lumala alimuelezea kama mtu tofauti miongoni mwa kampeni ya inayotawaliwa na wanaume, na anasema aliwapatia Wakenya wakati wao wa "Kamala Harris" katika kampeni.

"Tuliweza kuona umama [ndani yake]. Alitunza heshima yake n ahata wakati wa yalipokuwepo malumbano makali alipima lugha yake ," aliongeza, ingawa yeye pia alimshambulia Ruto katika siku zake za mwisho za kampeni akisema anapaswa "kuacha kuwa Naibu wa Yesu" kwa kulia katika mikutano ya maombi.

th

Pia unawezakusoma:

th