Uchaguzi Kenya 2022: Je wanamuziki wana ushawishi gani katika siasa za Kenya?

Trio
Maelezo ya picha, Mario TJ Kasela akiwa na umri wa miaka 17 ameweza kuimba wimbo 'Sipangwingwi' unaochezwa katika mikutano ya kampeni za uchaguzi nchini Kenya
    • Author, Dinah Gahamanyi
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Iliyochapishwa
  • Muda wa kusoma: Dakika 5

Kinyume na siasa za miaka iliyopita, wanasiasa katika uchaguzi wa mwaka wa 2022, wanaonekana kwenda na wakati, hususan inapokuja katika kuchagua  nyimbo wanazozitumia katika kampeni zao ili kuwavutia wafuasi wao,hasa wale wa umri mdogo .

Kwa mfano Wagombea wakuu wa Urais Raila Odinga na Naibu Rais William Ruto , katika nyakati fofauti wameonekana kutumia wimbo uliovuma al Maarufu ''Sipangwingwi'. 

''Sipagwingwi''ulioimbwa kwa Lugha ya Sheng, na kijana mwenye umri wa miaka 17- Mario TJ Kasela, aliyekuwa shule ya upili, akimshirikisha Exray Taniua, imevuma sana kwenye redio mbali mbali nchini Kenya na sasa hutumiwa kwenye mikutano ya  kambi kuu mbili pinzani za kisiasa katika kampeni za uchaguzi wa  2022.

Wakati wa Kongamano la kitaifa la   Azimio La Umoja katika uwanja wa  Kasarani, mwanamuziki huyu aligonga vichwa vya habari wakati alipoonekana moja kwa moja kwenye Vituo vyote vya Televisheni katika matangazo ya kutoka kwenye kongamano hilo mbele ya umati uliokuwa ukisherehekea kuundwa kwa Muungano wa Azimio la Umoja.

Awali Mwenzake Exray Taniua  pia alionekana akiipiga 'mgoma' hiyo katika Kampeni za Naibu Rais William Ruto mwaka  2021.Mara baada  kukutana,  Naibu Rais aligeuza jina la wimbo, kulingana na ujumbe aliotaka kuufikisha kwa wapinzani wake na kuuita ''Hatupangwingwi'' katika mkutano wake wa kampeni.  Jina jipya la wimbo lililenga kuwaasa wapiga kura kutowaruhusu watu binafsi kuwaamlia kwa niaba yao ni nani atakayekuwa rais ajaye. 

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

 Sauti Sol - 'Tano Tena' wakiwashirikisha Nviiri The Storyteller na Bensoul

Sauti soul

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Sauti Soul

Katika kibao chao hivi karibuni  kabisa  ''Miaka tano tena'' Sauti Soul wakimshirikisha Nviiri The Storyteller na  Bensoul,   kilichopigwa kwa mtindo wa  R &B  ni  ''ngoma'', ambayo pia huenda haitasahaulika  katika uchaguzi wa wa Kenya kutokana na maudhui yaliyomo. ''Miaka tano tena''  ambao tayari umekwishatazamwa na watu zaidi ya laki mbili tangu  kuwekwa kwenye mtandao wa You Tube baada ya video yao kupakuliwa  tarehe 2 Agosti,  una maneno kama ''sikufi miaka tano tena'', na ''sikupi miaka tano tena'' unaonekana kutuma ujumbe unaolenga kuwashauri Wakenya waache kuwapigia kura viongozi walioshindwa kutekeleza ahadi za maendeleo kwa wananchi  au kutowahuduamia wapiga kura baada ya kuwachagua, miaka mitano iliyopita.  Haijulikani iwapo Wakenya watatekeleza maudhui yaliyomo ndani ya wimbo  ''Miaka Tano Tena''

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

 Mbali na kampeni za urais, katika kampeni za wagombea wa viti  vya Ubunge, ugavana, Useneta na madiwani(MCA), wagombea wamekuwa wakitumia tunzi za wasanii wa nyimbo za lugha za jamii zao kunadi sera zao na kuwashawishi wapiga kura kuwapigia kura katika uchaguzi mkuu.

Kubadilika kwa ''ladha'' za muziki kulingana na nyakati

'Ladha' za muziki unaotumika katika siasa za uchaguzi wa Kenya zimekuwa zikibadilika  kulingana na nyakati na mtindo wa muziki uliopo wakati huo na unaopendelewa na jamii hususan vijana.

Katika uchaguzi wa sasa ladha ya ''muziki wa Genge'',inatumiwa zaidi,  uchaguzi Mkuu uliopita kulikuwa na mapambano ya lugha katika matumizi ya nyimbo na kila wimbo uliimbwa kwa manufaa ya  wagombea.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?
Ben githae

Chanzo cha picha, Ben Githae /Facebook

Maelezo ya picha, Katika uchaguzi wa mwaka 2017, wanamuziki Ben Githae (wa kwanza kutoka kushoto akiwa na Rais Kenyatta pamoja na Naibu wake William Ruto) aliimba wimbo kwa ajili ya Muungano wa Jubilee  "Wembe Ni Ule Ule" kuashiria utayari wa Uhuru Kenyatta na Dkt Ruto  wa kuwania mamlaka katika muhula wa pili

Kwa mfano Ben Githae aliimba wimbo kwa ajili ya Muungano wa Jubilee  "Wembe Ni Ule Ule" kuashiria utayari wa Uhuru Kenyatta na Ruto  kuwania uongozi katika muhula wa pili , huku Muungano wa  Nasa ukiwa na wimbo  "Bindu Bichenjanga", ulioimbwa na Amos Barasa ulilenga kuonyesha kwamba mabadiliko  yanakuja katika ardhi ya ahadi , Canaan.

Wimbo mwingine uliovuma katika uchaguzi uliopita ni pamoja na  "Nasa (Tibim)" ulioimbwa na Onyi Jalamo, "Tano Tena" wa Ben Githae, "Jubilee Emet" wa Florence Chepng'etich, na  "Jubilee Tosha" ulioimbwa na Marion Cherotich.

'Ushawishi wa wanamuziki wa Kenya katika siasa sio wa sasa'

Katika kampeni za mwaka  2017, wasanii wawili   waling'aa. Emma Jalamo aliyeimba 'ngoma' iliyovuma NASA  ambapo wimbo wake uliimbwa kwa lugha ya  Luo, wimbo wake ulichezwa katika matukio yote ya kumuunga  mkono Raila na Muungano wake wakati huo -National Super Alliance (NASA). 

 Mwaka  2002, GidiGidi MajiMaji,  wimbo wa bendi yao maarufu ya Hip hop  iliimba kibao kilichoitwa "Unbwogable" kilichovuma na kupendwa wakati Mwai Kibaki wa NARC alipokabiliana na  Uhuru Kenyatta wa KANU katika mbio za kuingia ikulu

 "Hamu ya nchi ya mabadiliko ililetwa kwa njia ya muziki na wasanii .  Wanamuziki wawili, Joseph Ogidi na Jahd Adonija, chini ya jina Gidi Gidi Maji Maji, waliimba  kibao Ting Badi Malo na  I am Unbwogable , kilichokonga mioyo ya wapiga kura'', inasema taarifa ya tathmini ya utafiti uliofanywa na Gordon Omenya na kuchapishwa katika  Tathmini ya gazeti la East African.   

"Unbwogable ukawa wimbo uliotumiwa kuwahamasisha wapiga kura katika kuunga mkono  Muungano wa  -National Rainbow Coalition (NARC). Na tangu wakati huo, wanasiasa wamekuwa mara kwa mara wakiwakodi wasanii kuimba sifa zao na kwenye majukwaa yao ya kisiasa." , anasema Gordon Omenya.

Pia ''Ngoma'' ya DNA na P-Unit  "Una" ilitamba katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2007. 

Je wanamuziki wameweza kuwashawishi Wakenya kupiga kura?

Licha ya umaarufu wa kazi hizi za muziki wa wasanii kwenye majukwa ya wanasiasa wanaowania nyadhifa  mbalimbali za uongozi, kuna dalili ndogo sana za kuonyesha  kwamba wakenya hususan vijana wanashawishika kupiga kura. 

Katika ripoti yake ya ukaguzi ya Juni 2022, Tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) ilionyesha kuwa asilimia ya vijana, wenye umri wa kati ya miaka 18  hadi 34, walijisajili kupiga kura katika uchaguzi wa mwaka  2022  idadi hiyo ikipungua kwa asilimia 5.27 ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2017 - ambao ulibatilishwa na kurudiwa .

Inaaminika kuwa kazi za usanii hatahivyo zilichangia pakubwa katika kampeni za kuelekea uchaguzi , na kuwashawishi vijana kushiriki upigaji kura.

Wajakoya

Chanzo cha picha, Wajakoyah

Maelezo ya picha, Baadhi ya wasanii wameanza kubuni muziki wanavutiwa na kuzungumzia vitu anavyovitetea Bwana George Wajackoyah (Mgombea wa rais), hususan bangi

Mwaka huu kwa upande mwingine Roots Party, chama cha  George Wajackoyah - mmoja wa wagombea wanne wa urais, kimevutia ushawishi na hisia kubwa miongoni mwa vijana  katika uchaguzi wa mwaka huu hususan wale ambao awali hawakujali kuhusu mamsuala ya uchaguzi. Wasanii wameanza kubuni muziki unaozungumzia vitu anavyovitetea Bw. Wajackoyah  katika kampeni zake.

''Baadhi ya vijana wameanza kuimba nyimbo zenye ujumbe wa kuunga mkono -bangi na kutokana na kwamba mtindo  wake wenyewe wa kampeni unaendana na aina ya muziki   maarufu wa vijana, anasema   mkazi wa mtaa wa mabanda wa Kibera.'' Wamaitha Kariuki.,"Ujumbe wake wa  kubuni ajira umechangia pakubwa katika kuikumbusha hadhira kwamba kuna hali  mustakabali mzuri baada ya uchaguzi huu ," aliongeza

.

Unaweza pia kusoma:

,