Maelezo ya picha, Mario TJ Kasela akiwa na umri wa miaka 17 ameweza kuimba wimbo 'Sipangwingwi' unaochezwa katika mikutano ya kampeni za uchaguzi nchini KenyaMaelezo kuhusu taarifa
Author, Dinah Gahamanyi
Nafasi, BBC Swahili
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 5
Kinyume na siasa za miaka iliyopita, wanasiasa katika uchaguzi wa mwaka wa 2022, wanaonekana kwenda na wakati, hususan inapokuja katika kuchagua nyimbo wanazozitumia katika kampeni zao ili kuwavutia wafuasi wao,hasa wale wa umri mdogo .
Kwa mfano Wagombea wakuu wa Urais Raila Odinga na Naibu Rais William Ruto , katika nyakati fofauti wameonekana kutumia wimbo uliovuma al Maarufu ''Sipangwingwi'.
''Sipagwingwi''ulioimbwa kwa Lugha ya Sheng, na kijana mwenye umri wa miaka 17- Mario TJ Kasela, aliyekuwa shule ya upili, akimshirikisha Exray Taniua, imevuma sana kwenye redio mbali mbali nchini Kenya na sasa hutumiwa kwenye mikutano ya kambi kuu mbili pinzani za kisiasa katika kampeni za uchaguzi wa 2022.
Wakati wa Kongamano la kitaifa la Azimio La Umoja katika uwanja wa Kasarani, mwanamuziki huyu aligonga vichwa vya habari wakati alipoonekana moja kwa moja kwenye Vituo vyote vya Televisheni katika matangazo ya kutoka kwenye kongamano hilo mbele ya umati uliokuwa ukisherehekea kuundwa kwa Muungano wa Azimio la Umoja.
Awali Mwenzake Exray Taniua pia alionekana akiipiga 'mgoma' hiyo katika Kampeni za Naibu Rais William Ruto mwaka 2021.Mara baada kukutana, Naibu Rais aligeuza jina la wimbo, kulingana na ujumbe aliotaka kuufikisha kwa wapinzani wake na kuuita ''Hatupangwingwi'' katika mkutano wake wa kampeni. Jina jipya la wimbo lililenga kuwaasa wapiga kura kutowaruhusu watu binafsi kuwaamlia kwa niaba yao ni nani atakayekuwa rais ajaye.
Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?
Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya
Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake
Raila Amollo Odinga
Muungano wa Azimio la Umoja
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.
William Samoei Ruto
Muungano wa Kenya Kwanza
Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC
George Wajackoyah
Chama cha Roots
Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito
David Mwaure Waihiga
Chama cha Agano
David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
Kupambana na ufisadi uliokithiri.
kuunda nafasi za ajira.
Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.
Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa
Sauti Sol - 'Tano Tena' wakiwashirikisha Nviiri The Storyteller na Bensoul
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Sauti Soul
Katika kibao chao hivi karibuni kabisa ''Miaka tano tena'' Sauti Soul wakimshirikisha Nviiri The Storyteller na Bensoul, kilichopigwa kwa mtindo wa R &B ni ''ngoma'', ambayo pia huenda haitasahaulika katika uchaguzi wa wa Kenya kutokana na maudhui yaliyomo. ''Miaka tano tena'' ambao tayari umekwishatazamwa na watu zaidi ya laki mbili tangu kuwekwa kwenye mtandao wa You Tube baada ya video yao kupakuliwa tarehe 2 Agosti, una maneno kama ''sikufi miaka tano tena'', na ''sikupi miaka tano tena'' unaonekana kutuma ujumbe unaolenga kuwashauri Wakenya waache kuwapigia kura viongozi walioshindwa kutekeleza ahadi za maendeleo kwa wananchi au kutowahuduamia wapiga kura baada ya kuwachagua, miaka mitano iliyopita. Haijulikani iwapo Wakenya watatekeleza maudhui yaliyomo ndani ya wimbo ''Miaka Tano Tena''
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo
Mwisho wa X ujumbe
Mbali na kampeni za urais, katika kampeni za wagombea wa viti vya Ubunge, ugavana, Useneta na madiwani(MCA), wagombea wamekuwa wakitumia tunzi za wasanii wa nyimbo za lugha za jamii zao kunadi sera zao na kuwashawishi wapiga kura kuwapigia kura katika uchaguzi mkuu.
Kubadilika kwa ''ladha'' za muziki kulingana na nyakati
'Ladha' za muziki unaotumika katika siasa za uchaguzi wa Kenya zimekuwa zikibadilika kulingana na nyakati na mtindo wa muziki uliopo wakati huo na unaopendelewa na jamii hususan vijana.
Katika uchaguzi wa sasa ladha ya ''muziki wa Genge'',inatumiwa zaidi, uchaguzi Mkuu uliopita kulikuwa na mapambano ya lugha katika matumizi ya nyimbo na kila wimbo uliimbwa kwa manufaa ya wagombea.
Kufikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
Elimu Bure kwa wote.
Huduma ya afya bora kwa wote.
Uchumi
Kukuza sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi na uchumi wa bluu hadi asilimia 30 ya Pato la Taifa.
Kuza bidhaa za "Zilizotengezwa Kenya" kwa kusaidia ukuaji wa biashara ndogo ndogo na za kati.
Mpango wa "Kaunti Moja, Bidhaa Moja" kutegemea utengenezaji kama injini ya uundaji wa utajiri na ajira.
Ufisadi
Kuboresha kwa haraka mamlaka ya kisheria na kiutawala.
Kuongeza kasi ya kurejesha mapato ya rushwa na uwepo wa fedha haramu.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Kupunguza kasi ya ulimbikizaji wa madeni.
Boresha sera za usimamizi wa madeni.
Kuendeleza mazungumzo ya msamaha wa madeni.
Ajira
Kutumia vizuri idadi kubwa ya vijana kwa ustawi
Kuboresha tija katika sekta ya viwanda na kusaidia uzalishaji wa ajira katika sekta hiyo.
Wekeza katika teknolojia zinazoibukia ambazo zitatoa fursa za ajira kwa vijana wa Kenya.
Kawi
Punguza gharama ya umeme.
Tathmini ushuru na kodi za bidhaa za petroli.
Kuongeze utafutaji wa mafuta na gesi kwenye nchi kavu na baharini.
Afya
Huduma ya afya bora kwa wote.
Kukuza uzalishaji wa ndani wa dawa na pembejeo nyingine zinazohusiana na afya.
Kuboresha mazingira ya kazi na malipo ya wataalamu wa afya.
Uhalifu na usalama
Kuhakikisha utekelezaji madhubuti wa mageuzi ya polisi.
Kuwafunza angalau maafisa sita wa polisi katika kila kituo cha polisi kushughulikia uhusiano wa polisi na vijana.
Boresha sheria na sera kuhusu usalama na usalama mtandaoni.
Elimu
Kutoa elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu.
Toa mlo mmoja kwa siku kwa watoto wa chekechea na madarasa ya mwanzo ya shule za msingi
Kukuza uhusiano wa kufanya kazi kati ya taasisi za elimu na utafiti na viwanda.
Usambazaji wa maji
Wekeza na kukuza uvunaji wa maji ya mvua na udhibiti wa mafuriko.
Kupanua miundombinu ya mabwawa na umwagiliaji.
Kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama kwa kila shule na boma
Gharama ya maisha
Tathmini gharama ya mafuta, unga na nishati katika siku 100.
Kuongeza uwezo wa kusambaza umeme na kupunguza upotevu wa gridi kutoka asilimia 23 hadi 10.
Weka mazingira wezeshi ya kupata chakula, mavazi, malazi na mahitaji mengine ya kimsingi kwa bei nafuu.
Roots Party of Kenya
Vipaumbele
Kuendesha serikali yenye faida kupitia kuhalalisha na kudhibiti utumiaji wa bangi kiviwanda
Kuunda majimbo 8 ambayo yatasimamiwa na serikali zao za shirikisho.
Sitisha katiba, ili kuwapa Wakenya fursa ya kuchagua sheria inayowafaa.
Uchumi
Uchumi wa saa 24 wa zamu ya saa nane, siku nne kwa wiki.
Kuongeza bajeti ya serikali kupitia mapato ya fedha za kigeni kutokana na mauzo ya katani ya viwandani.
Pata mapato kupitia ufugaji wa nyoka na kuuza nje nyama ya mbwa.
Ufisadi
Kuanzisha hukumu ya kifo inayotumika kwa watu wanaopatikana na hatia ya rushwa.
Kutovumilia rushwa.
Madeni
Lipa deni la Kenya haraka kwa mapato kutoka kwa kuhalalisha na usafirishaji wa bangi ya viwandani.
Mkopo huo utalipwa kwa awamu 30 kati ya Januari 2021 hadi Julai 2035.
Epuka madeni kwa kutumia mapato yaliyopatikana kutokana na kuhalalisha bangi ili kuongeza mapato ya serikali.
Ajira
Unda fursa za Uwekezaji na ajira kwa kuhalalisha bangi
Kawi
Tumia katani ya Viwanda kuzalisha nishati ya kibayolojia.
Kupunguza gharama ya nishati kwa kupunguza kodi na kushughulikia mzigo wa madeni.
Afya
Huduma za afya na lishe ya bure kwa wazee, walio katika mazingira magumu na wajawazito.
Boresha matibabu na udhibiti wa Alzheimer's, saratani, ugonjwa wa kupooza kwa ubongo na kifafa kwa kutumia moja ya bidhaa za katani za viwandani.
Kutanguliza utafiti na maendeleo katika kampuni za dawa zinazomilikiwa na Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuwalipa polisi vizuri ili kupunguza rushwa.
Elimu
Wape wazazi chaguo la masomo ya nyumbani na kurahisisha mchakato wa usajili.
Boresha mfumo wa elimu wa CBC nchini Kenya.
Usambazaji wa maji
Kuboresha miundombinu ya majisafi na majitaka.
Gharama ya maisha
Tengeneza fursa za ajira na uwekezaji.
Punguza kodi na gharama ya nishati.
Chama cha Agano
Vipaumbele
Unda taasisi zitakazomaliza ubadhirifu wa fedha na kukomesha ufisadi.
Hakikisha kwamba haki za wasio na sauti na waliotengwa zinazingatiwa.
Punguzo la ushuru kwa Wakenya kusaidia kudhibiti gharama ya maisha.
Uchumi
Kupeleka bajeti kwa halmashauri za vijiji badala ya Hazina na Ikulu.
Weka mazingira mazuri kwa sekta binafsi na watu binafsi kuanzisha biashara.
Ufisadi
Fanya ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuwa ushahidi wa msingi wa matumizi mabaya ya ofisi na msingi wa kuwashtaki watumishi wa umma walio wafisadi
Kesi zote za ufisadi zitashughulikiwa ndani ya miezi mitatu.
Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kupewa mamlaka ya kuendesha mashtaka.
Madeni
Majadiliano kwa lengo la kupanga upya ulipaji wa deni na wakopeshaji.
Tumia fedha zilizopatikana kutokana na shughuli za kifisadi kulipa madeni ya nje.
Kurejesha fedha zilizofichwa nje ya nchi ili kusaidia kulipa deni la nje .
Ajira
Tekeleza sheria ya maudhui ya humu nchini kwa kuongeza kiwango cha juu cha kandarasi zinazotolewa kwa makampuni ya kigeni hadi zaidi ya $8.5 milioni (Ksh1 bilioni).
Punguzo la kodi kwa makampuni yanayoajiri wanawake na vijana.
Kuharakisha utekelezaji wa mpango wa Kanda Maalum ya Kiuchumi ili kuhimiza wageni,makampuni ya kuanzisha viwanda vya utengenezaji nchini Kenya.
Kawi
Kusaidia matumizi ya nishati ya jua nje ya gridi ya taifa.
Kufanya nishati kuwa bei nafuu kwa kushughulikia rushwa katika sekta ya nishati.
Afya
Unda tume ya kitaifa ya afya ili kudhibiti kupanda kwa gharama za afya.
Kutoa ruzuku kwa michango ya Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya kwa kila familia Kenya.
Uhalifu na usalama
Kuboresha maisha na mazingira ya kazi ya polisi.
Fanya vikosi vya usalama kuwa vya kisasa ili kuendana na uhalifu wa kisasa.
Punguza msongamano wa magereza na kuboresha hali ya maisha na kazi ya maafisa wa magereza
Elimu
Kuanzisha kipengele cha maadili katika mtaala.
Elimu ya bure katika ngazi zote.
Walimu wawezeshwe kidijitali kufanya kozi za kujiongeza masomo
Usambazaji wa maji
Maeneo kame kupokea maji ya bomba kwa ajili ya umwagiliaji.
Kuondoa tozo dhidi ya vifaa vyote vya kuvuna maji ya mvua.
Kukuza upandaji miti upya.
Gharama ya maisha
Msamaha wa jumla wa 50% kwa PAYE kwa Wakenya wote.
Kenya Kwanza Alliance
Vipaumbele
Tenga $427 milioni (Ksh50 bilioni) kila mwaka ili kutoa mikopo kwa biashara ndogo ndogo na za kadri kwa njia rahisi na inayotegemeka
Kurekebisha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kubadilisha mchango kwa familia/nyumba badala ya watu binafsi.
Mtandao wa bure ndani ya miaka mitano.
Uchumi
Komesha ushuru unaorudiwa
Fanya leseni ya biashara na eneo kuwa haki.
Weka sera thabiti ya ulinzi wa huduma za kifedha ili kuwalinda Wakenya dhidi ya wakopeshaji walaghai.
Ufisadi
Kuzipa uhuru taasisi zinazohusika na vita dhidi ya rushwa.
Taarifa za wafanyabiashara wanaofanya biashara na serikali kuwekwa wazi.
Shirikiana na nchi nyingine kusaidia kurejesha mali zilizoibiwa.
Madeni
Kuimarisha uwezo wa serikali wa kukopesheka kutoka nje na kuongeza upatikanaji wa mikopo nafuu, na kuacha vyanzo vya mikopo vya ndani kwa sekta binafsi.
Ajira
Wekeza kwenye kilimo ili kutengeneza ajira zaidi.
Anzisha Kituo cha Maendeleo ya Biashara cha MSME katika kila kata na bustani ya viwanda.
Kuanzisha kituo cha ukuzi wa biashara katika kila taasisi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.
Kawi
Weka mfumo wa kisheria wa kulinda hazina ya uimarishaji wa mafuta.
Unda vivutio vya kupitishwa kwa mifumo ya usafiri wa umma ya umeme katika miji na miji yote.
Kuharakisha maendeleo ya rasilimali ya kawi ya mvuke
Afya
Huduma ya afya ya msingi inayofadhiliwa kikamilifu.
Kuanzisha mfuko wa kitaifa wa magonjwa sugu.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wa lazima.
Uhalifu na usalama
Imarisha uangalizi wa polisi na kuteua mchunguzi atakayezingatia ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vijana.
Bima ya maisha kwa maafisa wa polisi iwapo watafariki wakiwa kazini.
Mfuko wa hisani wa kuchangia familia za maafisa walioaga dunia na wagonjwa mahututi.
Elimu
Lipia mafunzo ya ualimu kazini.
Tathmini mfumo wa sasa wa maendeleo ya kitaaluma kulingana na mitihani.
Kupunguza pengo la sasa la upungufu wa walimu 116,000 ndani ya miaka miwili ya kifedha.
Usambazaji wa maji
Maji yatapewa kipaumbele kwa ruzuku ya mradi/ufadhili wa masharti nafuu.
Hamisha mwelekeo kutoka kwa mabwawa makubwa hadi kwenye miradi ya maji ya kijamii huku msisitizo ukiwa katika kuvuna na kurejeleza
Gharama ya maisha
Kuongeza tija ya kilimo ili kupunguza gharama ya maisha.
Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.
End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?
Chanzo cha picha, Ben Githae /Facebook
Maelezo ya picha, Katika uchaguzi wa mwaka 2017, wanamuziki Ben Githae (wa kwanza kutoka kushoto akiwa na Rais Kenyatta pamoja na Naibu wake William Ruto) aliimba wimbo kwa ajili ya Muungano wa Jubilee "Wembe Ni Ule Ule" kuashiria utayari wa Uhuru Kenyatta na Dkt Ruto wa kuwania mamlaka katika muhula wa pili
Kwa mfano Ben Githae aliimba wimbo kwa ajili ya Muungano wa Jubilee "Wembe Ni Ule Ule" kuashiria utayari wa Uhuru Kenyatta na Ruto kuwania uongozi katika muhula wa pili , huku Muungano wa Nasa ukiwa na wimbo "Bindu Bichenjanga", ulioimbwa na Amos Barasa ulilenga kuonyesha kwamba mabadiliko yanakuja katika ardhi ya ahadi , Canaan.
Wimbo mwingine uliovuma katika uchaguzi uliopita ni pamoja na "Nasa (Tibim)" ulioimbwa na Onyi Jalamo, "Tano Tena" wa Ben Githae, "Jubilee Emet" wa Florence Chepng'etich, na "Jubilee Tosha" ulioimbwa na Marion Cherotich.
'Ushawishi wa wanamuziki wa Kenya katika siasa sio wa sasa'
Katika kampeni za mwaka 2017, wasanii wawili waling'aa. Emma Jalamo aliyeimba 'ngoma' iliyovuma NASA ambapo wimbo wake uliimbwa kwa lugha ya Luo, wimbo wake ulichezwa katika matukio yote ya kumuunga mkono Raila na Muungano wake wakati huo -National Super Alliance (NASA).
Mwaka 2002, GidiGidi MajiMaji, wimbo wa bendi yao maarufu ya Hip hop iliimba kibao kilichoitwa "Unbwogable" kilichovuma na kupendwa wakati Mwai Kibaki wa NARC alipokabiliana na Uhuru Kenyatta wa KANU katika mbio za kuingia ikulu
"Hamu ya nchi ya mabadiliko ililetwa kwa njia ya muziki na wasanii . Wanamuziki wawili, Joseph Ogidi na Jahd Adonija, chini ya jina Gidi Gidi Maji Maji, waliimba kibao Ting Badi Malo na I am Unbwogable , kilichokonga mioyo ya wapiga kura'', inasema taarifa ya tathmini ya utafiti uliofanywa na Gordon Omenya na kuchapishwa katika Tathmini ya gazeti la East African.
"Unbwogable ukawa wimbo uliotumiwa kuwahamasisha wapiga kura katika kuunga mkono Muungano wa -National Rainbow Coalition (NARC). Na tangu wakati huo, wanasiasa wamekuwa mara kwa mara wakiwakodi wasanii kuimba sifa zao na kwenye majukwaa yao ya kisiasa." , anasema Gordon Omenya.
Pia ''Ngoma'' ya DNA na P-Unit "Una" ilitamba katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2007.
Je wanamuziki wameweza kuwashawishi Wakenya kupiga kura?
Licha ya umaarufu wa kazi hizi za muziki wa wasanii kwenye majukwa ya wanasiasa wanaowania nyadhifa mbalimbali za uongozi, kuna dalili ndogo sana za kuonyesha kwamba wakenya hususan vijana wanashawishika kupiga kura.
Katika ripoti yake ya ukaguzi ya Juni 2022, Tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) ilionyesha kuwa asilimia ya vijana, wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 34, walijisajili kupiga kura katika uchaguzi wa mwaka 2022 idadi hiyo ikipungua kwa asilimia 5.27 ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2017 - ambao ulibatilishwa na kurudiwa .
Inaaminika kuwa kazi za usanii hatahivyo zilichangia pakubwa katika kampeni za kuelekea uchaguzi , na kuwashawishi vijana kushiriki upigaji kura.
Chanzo cha picha, Wajakoyah
Maelezo ya picha, Baadhi ya wasanii wameanza kubuni muziki wanavutiwa na kuzungumzia vitu anavyovitetea Bwana George Wajackoyah (Mgombea wa rais), hususan bangi
Mwaka huu kwa upande mwingine Roots Party, chama cha George Wajackoyah - mmoja wa wagombea wanne wa urais, kimevutia ushawishi na hisia kubwa miongoni mwa vijana katika uchaguzi wa mwaka huu hususan wale ambao awali hawakujali kuhusu mamsuala ya uchaguzi. Wasanii wameanza kubuni muziki unaozungumzia vitu anavyovitetea Bw. Wajackoyah katika kampeni zake.
''Baadhi ya vijana wameanza kuimba nyimbo zenye ujumbe wa kuunga mkono -bangi na kutokana na kwamba mtindo wake wenyewe wa kampeni unaendana na aina ya muziki maarufu wa vijana, anasema mkazi wa mtaa wa mabanda wa Kibera.'' Wamaitha Kariuki.,"Ujumbe wake wa kubuni ajira umechangia pakubwa katika kuikumbusha hadhira kwamba kuna hali mustakabali mzuri baada ya uchaguzi huu ," aliongeza