Uchaguzi wa Kenya2022:Ratiba na tarehe muhimu kuelekea uchaguzi wa Kenya 2022

TH

Chanzo cha picha, AFP

    • Author, Odhiambo Joseph
    • Nafasi, BBC Africa, Nairobi
  • Iliyochapishwa

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya tayari imetoa ilani ya ya mchakato mzima kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Jumanne tarehe 9 Agosti , 2022.

Katika ilani hiyo kuna baadhi ya tarehe ambazo zinajumuisha viti vyote na kuna nyingine inayohusu viti fulani tu.

Tarehe za jumla

•Jumatano , Februari 9, 2022 - Afisa yeyote wa umma anayetaka kugombea kiti chochote katika uchaguzi huu mkuu atalazimika kujiuzulu ifikapo Jumatano , Februari 9, 2022 ( miezi sita kabla ya uchaguzi)

•Alhamisi , Juni 9, 2022 - Mapingamizi au kesi zinazohusu uteuzi wa wagombea ndani ya vyama ni sharti ziwasilishwe mbele ya tume kabla ya siku ya Alhamisi , Juni 9, 2022.

•Saa za kampeni ni kuanzia saa moja asubuhi hadi kumi na mbili jioni - katika kipindi cha kampeni.

•Jumatatu , Julai 25, 2022- Vyama vya kisiasa pamoja na wagombea watahitajika kuwateuwa na kuwasilisha majina ya mawakala wao kwa tume kabla ya Jumatatu , Julai 25, 2022.

•Jumapili Mei 29, 2022 -Kipindi rasmi cha kampeni za uchaguzi huu mkuu ni kuanzia Jumapili Mei 29, 2022 na kumalizika jumamosi , Agosti 6, 2022, yaani saa 48 kabla ya siku ya kupiga kura.

•Jumanne tarehe 9 Agosti , 2022- Siku ya kupiga kura

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

Masharti na tarehe zinazohusu vyama vya kisiasa

Vyama vyote vya kisiasa vinalazimika kuwasilisha sajili zao za wanachama kwa tume ya uchaguzi ifikapo Jumamosi , Aprili 9, 2022.

•Chama chochote kinacholenga kushiriki katika uchaguzi huu ni sharti kiwasilishe majina ya wale wote wanaonuia kushiriki katika mchakato wa uteuzi wa vyama kwa njia ya mchujo, tarehe ya shughuli yenyewe na mahali penyewe ifikapo Jumamosi , Aprili 9, 2022, ikiwa ni siku 21 kabla ya uchaguzi mkuu.

•Chama kinachopanga kushiriki katika uchaguzi mkuu nisharti washughulike mapingamizi yeyote kwa kutumia mfumo wa ndani wa chama ifikapo Ijumaa Aprili 22, 2022.

•Chama kinachopanga kumteuwa mgombea au wagombea kwa mfumo wa moja kwa moja bila ya mchujo kiwasilishe majina hayo kwa tume ifikapo Alhamisi Aprili 28, 2022.

Masharti na tarehe zinazohusu wagombea huru

•Jumatatu Mei 2, 2022 - Wagombea wanapanga kushiriki katika uchaguzi huu kama wagombea huru ni sharti wasiwe wanachama wa chama chochote cha kisiasa kabla ya Jumatatu Mei 2, 2022, hii ikiwa ni angalau miezi mitatu kabla ya Uchaguzi Mkuu .

•Jumatatu Mei 2, 2022.- Wagombea wanaolenga kushiriki katika uchaguzi huu kama wagombea huru ni sharti wawasilishe majina yao pamoja na nembo zao wanazonuia kutumia katika uchaguzi ifikapo Jumatatu Mei 2, 2022.

•Ijumaa Mei 13, 2022 -Tume ya Uchaguzi itachapisha katika gaezeti rasmi la serikali majina pamoja na nembo ambazo wagombea huru wanapanga kutumia angalau siku 14 kabla ya tarehe rasmi ya uteuzi iliyowekwa na tume, yaani kabla ya Ijumaa Mei 13, 2022

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Masharti na tarehe zinazohusu wagombea urais

Jumatatu Mei 23, 2022 - Wagombea Urais kuwasilisha orodha ya angalau wapiga kura 2000 kutoka zaidi ya nusu ya Kaunti zote 47 kufikia Jumatatu , Mei 23 , 2022

Jumatatu , Julai 25, 202 - Vyama vya kisiasa pamoja na wagombea urais kuteuwa na kuwasilisha majina ya mawakala wake wakuu wa kitaifa na wa maeneo bunge kwa tume ifikapo Jumatatu , Julai 25, 202.

Jumapili , Mei 29 - Zoezi la uteuzi wa Tume kwa wagombea wote wa Urais kupitia vyama vya kisiasa na hata wagombea huru utaanza Jumapili , Mei 29 na kulamilika Jumatatu, Juni 6, 2022

Jumanne Agosti 9 , 2022- siku ya uchaguzi Mkuu wa Kenya