Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maisha yanaweza kuwepo kwenye sayari inayozunguka nyota 'nyeupe'
Watafiti wanaamini kuwa kunaweza kuwa na sayari ambayo inaweza kudumisha uhai, karibu na jua linalokufa.
Ikiwa itathibitishwa, hii itakuwa mara ya kwanza kwa sayari inayoweza kusaidia maisha kupatikana ikizunguka nyota kama hiyo, inayoitwa "kibete cheupe".
Sayari hiyo iligunduliwa katika "eneo linaloweza kukaa" la nyota hiyo, ambapo hakuna baridi sana wala joto sana ili kuendeleza uhai.
Utafiti huo umechapishwa katika notisi za kila mwezi za Jumuiya ya Kifalme ya Unajimu.
Prof Jay Farihi wa Chuo Kikuu cha London, ambaye aliongoza utafiti huo, alisema uchunguzi huo ni mpya kabisa kwa wanaastronomia.
"Hii ni mara ya kwanza kwa kitu chochote kuonekana katika eneo linaloweza kukaliwa na kibete cheupe. Na kwa hivyo kuna uwezekano wa maisha katika ulimwengu mwingine unaozunguka," aliiambia BBC News.
Ingawa nyota kubwa sana huwa mashimo meusi zinapokufa, ndogo kama vile Jua letu huwa vibete vyeupe - nyota ambazo zimetumia mafuta yao yote ya nyuklia na kupoteza nguvu zao za nje.
Kwa kawaida huwa na ukubwa wa sayari, na hutoa mwanga wa samawati-nyeupe inapoundwa mara ya kwanza.
Sayari inayowezekana, ambayo iko umbali wa miaka 117 kutoka kwa Dunia, inadhaniwa kuwa karibu mara 60 na nyota kuliko sayari yetu ilivyo na Jua.
Timu ya watafiti haina ushahidi wa moja kwa moja wa kuwepo kwa sayari hiyo - lakini mienendo ya miundo 65 yenye ukubwa wa Mwezi inayozunguka eneo linaloweza kukaliwa na kibete cheupe, zinaonyesha kuwa iko hapo.
Umbali wa miundo kuhusiana na kila mmoja haubadilika, ikionyesha kuwa iko chini ya ushawishi wa mvuto wa sayari iliyo karibu.
"Ilikuwa mshtuko kwa timu," Prof Farihi alisema. "Hoja ilikuwa sahihi sana hivi kwamba haungeweza kurekebisha mambo haya."
Eneo linaloweza kukaliwa ni sehemu inayozunguka nyota ambapo maji ya kioevu yanaweza kuwepo kwenye sayari, na hivyo kusaidia maisha. Mara nyingi hujulikana kama "eneo la Goldilocks", kwa sababu ikiwa sayari iko karibu sana na nyota itakuwa joto sana, na ikiwa mbali sana itakuwa baridi sana, ambapo ndani ya sehemu hii hali ni "sawa tu".
Matokeo yanapaswa kuwa kichocheo kwa wanaastronomia kutafuta kwa dhati ushahidi wa moja kwa moja wa sayari zinazozunguka ndege weupe.
"Kawaida katika astronomia, tukipata moja, kwa kawaida inamaanisha kuwa ni ya kawaida," alisema Prof Farihi.