Harakati za Freemason zinazotuhumiwa kusambaza mafundisho ya shetani?

محفل لندن

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa

Mara nyingi kumekuwa na mijadala inayoibuka kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuhusu ushawishi na kilichokuwa nyuma ya pazia ya harakati za Freemason{ Wamasoni} duniani, Majadiliano ambayo hutawaliwa na dhana zaidi.

Hoteli moja ya Wamasoni nchini Uingereza imechapisha tangazo kwenye magazeti kadhaa ikitoa wito wa kukomeshwa kwa vitendo ilivyoviita "kunyanyapaliwa" kwa wanachama wake.

Tangazo hilo lilitanguliwa na taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu kile ilichokieleza kuhusu ushawishi wa Freemasoni kati ya polisi na wabunge wa bunge la Uingereza.

Lakini nini hasa kuhusu harakati za Freemason na nini historia yake?

Freemason na nini

Kwa maelezo yao Freemasoni tafsiri yake yao ni "harakati ya kidugu ya kimataifa ambayo malengo yake ni kusaidiana, urafiki na wema wa watu". Freemasoni imekuwa kitu cha uhasama kwa kanisa, haswa Ukatoliki na watu wanaokuwa na mashaka na hofu na harakati hiyo.

الماسون

Chanzo cha picha, UNITED GRAND LODGE OF ENGLAND

Vyanzo vya harakati hizo za Freemason, kupitia kitabu cha "The Free Masons: The Illustrated Book of an Old Brotherhood" kilichoandikwa na Michael Johnston, kinasema kuna wanachama waandamizi wanaofuatilia asili ya Freemason kabla ya Mafuriko ya Nuhu na hata kabla ya kipindi cha mtume Abraham na mtume Solomon.

Lakini imeenea, kama kwa watafiti wengi, kwamba asili ya Freemasoni inarudi kwenye Zama za Kati, na enzi nzuri za mahitaji ya waashi ya kujenga majumba na makanisa makubwa.

Mwandishi wa Mason "Pat Morgan" anataja katika kitabu chake "Siri za bure za Freemason", na waandishi wengine wawili kuhusu imani hiyo "John Hamill" na "Robert Gilbert" katika kitabu chao cha encyclopedic "The Masonic Movement: A Celebration of Workmanship", na wengine, wanagusia kwamba imani hiyo imetokana na 'Wanajeshi" waliopotea "ambao walijulikana kama" Knights of the Temple "walionekana mwishoni mwa Vita vya Kwanza vya Kidini (1095-1099) kwenye nchi za kiarabu.

Ishara na alama za Freemason

الماسون

Freemason mara zote imekuwa ikihusishwa na alama na ishara ambazo nyingi zinawawakilisha. Kwa mfano kwenye kona ya majengo yao kuna alama kama mwezi au nyota, zinazowakilisha ukweli na uelewa, alama ya jicho na herufi ya kilatin ya G. Kwa mujibu wao herufi G inawakilisha neno 'God' kwa maana ya Mungu. Freemason wanawajibika kuamini kwamba yupo kiumbe mkuu ambaye wanamwita "mbuni mkubwa wa ulimwengu," hata kama hawamwiti Mungu.

Na kuhusu alama ya jicho inayoonekana kwenye majengo yao, inaamaanisha jicho linaloona kila kitu. Wenyewe wanasema jicho hilo linamaanisha kwamba "Mungu anaweza kuchunguza kwa kutumia macho yake kina cha mioyo na roho za watu. " Kwamba anaweza kujua kilichoko myoyoni na kwenye roho za watu.

Jicho linaloona kila kitu

الماسون

Kw upande mwingine , wasiounga mkono freemason wanasema jicho linalosema sio jicho la "Mungu" , wanachokiamini ni kwamba jicho hilo ni "jicho la shetani," ambalo kupitia shughuli zao, wanatafuta kutawala dunia, na kufanya "kila kitu kiwe chini ya utawala wao."

Kwa mujibu wa kitabu cha "Explanation of Masonic Symbols" kinachoangalia alama za freemason kilichoandikwa na "Dr. Cathy Burns," , anasema, "herufi G inawakilisha Venus, moja ya sayari ulimwenguni. Na Venus huwakilisha kiungo cha kiume kwa wanaume, na pia ni moja ya majina ya shetani.

Wanaopinga Freemason wanaongeza kwa kusema mwandishi "Michael Benson" anasema kupitia kitabu chake cha "Inside Secret Societies" kwamba "alama ya jicho inayoonekana kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye pesa ya dola moja, inaonyesha ni namna freemason wanavyotawala Marekani na dhamira yao ya kutawala dunia, ikiwa tu yoyote anayetengeneza alama hiyo na kuchora michoro yao, anakuwa na asili ya Freemason.

Hata hivyo Freemason wenyewe wanapingana na dhana hiyo kuhusu utawala wao Marekani na kwenye pesa pamoja na dhamira inayosema kutawala dunia.

Marufuku siasa na dini

Kitu kinachofanya watu wengi kujiuliza kuhusu harakati za freemason ni kwamba freemason wanakatazwa kuzungumzia kuhusu siasa na dini. Kuna wanasiasa wengi na viongozi wakubwa wa dini katika historia ya Uingereza, ambao walikuwa sehemu ya Freemason, mmoja anayefahamika zaidi ni waziri mkuu wa zamani wa Uingereza "Winston Churchill", na kiongozi wa zamani wa kanisa la Anglikana, "Jeffrey Fisher".

Mambo ya kuyajua kuhusu Freemason ni kwamba Freemason hukutana katika hekalu, ambalo wanaita "Jukwaa", na ni mahali ambapo - kama inavyoaminika - wajenzi wa zamani walikuwa wakikutana walipokuwa wakifanya kazi kanisani au kanisa kuu.

Kila mwanachama wa Freemason anavaa 'apron', ambaye asili yake inarudi kwenye nadharia kwamba Freemason ilibadilika kutoka kwa Masons wa zamani, ambao walivaa aproni kuwalinda kutoka kwa viboko .

Freemason maarufu ni pamoja na Winston Churchill, Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, na Sir Arthur Conan Doyle, mwandishi wa Sherlock Holmes, Rudyard Kipling, Robert Burns, Oscar Wilde na Peter Sellers.