Tetesi za soka Ulaya Alhamisi tarehe 2.09.2021: Niguez,Haaland, Woodward, Ronaldo, Olmo

Spain striker Dani Olmo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mshambuliaji wa Uhispania Dani Olmo
Iliyochapishwa

Kiungo wa kati wa Uhispania Saul Niguez, 26, anatarajiwa kuvaa jezi namba 17 huko Chelsea baada ya kujiunga kwa mkopo kutoka Atletico Madrid siku ya mwisho ya uhamisho. (Star)

Erling Braut Haaland

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Erling Braut Haaland alijunga na Borussia Dortmund kutoka Red Bull Salzburg Januari 2020

Mshambuliaji wa Borussia Dortmund na Norway Erling Braut Haaland, 21, atakuwa mlengwa mkubwa wa Manchester United msimu ujao licha ya kuwasili kwa mshambuliaji wa Ureno Cristiano Ronaldo mwenye umri wa miaka 36 kutoka Juventus. . (ESPN)

Manchester United executive vice-chairman Ed Woodward

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Ed Woodward amekuwa na jukumu hilo tangu mwaka 2013

Makamu mwenyekiti anayemaliza muda wake wa Manchester United Ed Woodward alikuwa na jukumu muhimu katika kuwezesha kupatikana kwa Ronaldo. (Manchester Evening News)

Spain striker Dani Olmo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mshambuliaji wa Uhispania Dani Olmo

Barcelona itajaribu kumsajili tena kiungo wa kati wa Uhispania Dani Olmo, 23, mnamo mwezi Januari baada ya kushindwa kufanikiwa siku ya mwisho ya uhamisho kwa kitita cha pauni milioni 50 ambayo ilikataliwa na RB Leipzig. (Mail)

Djed Spence

Chanzo cha picha, Rex Features

Maelezo ya picha, Djed Spence

Leicester, Southampton na Nottingham Forest zote zilitoa ofa ya kuchelewa kwa beki wa kulia wa Middlesbrough, Muingereza, 21, Djed Spence. (Northern Echo)

Kocha wa Tottenham, Nuno Espirito Santo alimhakikishia Emerson Royal, mwenye umri wa miaka 22, kwamba atakuwa na jukumu muhimu katika timu hiyo, kabla ya mlinzi wa Brazil kukubali kuondoka Barcelona. (Marca)

Yves Bissouma

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Yves Bissouma

Manchester United, Liverpool na Arsenal ziko tayari kupigania kumsaka kiungo wa kati wa Brighton na Mali, 25, Yves Bissouma mnamo mwezi Januari. (Mirror)

Mlinzi wa Chelsea raia wa Ufaransa Malang Sarr, 22, ameachwa kwenye njia panda baada ya mpango wake wa kuhamia upande wa Bundesliga timu ya Greuther Furth kwa mkopo kushindwa kufanikiwa siku ya mwisho ya uhamisho. (Mail)