UAE yasitisha utoaji viza kwa Wakenya na mataifa mengine 12 ya Kiislamu

Iliyochapishwa

Kulingana na nyaraka iliotolewa, nchi nyingi zilizoathirika ni za Kiislamu yaani Iran, Syria, Afghanistan na Pakistan.

Chanzo cha ndani kilichozingumza na shirika la habari la Reuters kimesema chanzo cha kusitishwa kwa utoaji visa ni sababu za kiusalama lakini hakuna taarifa zozote za kina zilizotolewa.

Nyaraka hiyo iliotumwa kwa makampuni yanayoendesha shughuli za visa iliyoonesha kwamba inaanza kutekelezwa Novemba 18.

Aidha, nyaraka hiyo pia ilionesha marufuku ya kutolewa kwa visa mpya za ajira pamoja na za raia wa kigeni nje ya UAE, wanaotaka kutembelea nchi hiyo wa nchi 13 pamoja na Somalia, Libya na Yemen hadi siku isiyojulikana.

Serikali ya Kenya bado haijatoa tamko lolote kuhusiana na hatua hiyo sawa na mamlaka husika ya UAE ambayo baada ya kuzungumza na Shirika la Habari la Reuters haikusema lolote.

Hatua hiyo inawadia wiki moja baada ya Ubalozi wa Ufaransa nchini UAE kusihi raia wake kuchukua tahadhari baada ya kutokea kwa shambulizi la bomu dhidi ya wanadiplomasia nchini Saudi Arabia huku wanamgambo wa Islamic State wakadai kuhusika.

Kashfa ya dhahabu Kenya

Mwaka 2019 uhusiano kati ya Kenya na UAE uliathirika kufuatia kashfa iliozunguka biashara ya Dhahabu iliokuwa ikielekea katika taiafa hilo la Kiarabu

Mtawala wa Dubai Sheikh Mohammed Al-Makhtoum, alituma barua ya pingamizi kwa Kenya akitaka kuachiliwa kwa mzigo wa dhahabu uliokuwa ukizuiliwa na idara ya forodha mjini Nairobi.

Kesi hiyo ndio ya hivi karibuni inayowahusisha washirika wa Sheikh al-Makhtoum ambao wamehujumiwa katika biashara ya Dhahabu nchini Kenya na Uganda.

Shiekh Mohammed Al Maktoum: Je mtawala huyu wa Dubai ni mtu wa aina gani?

Sheikh Mohammed pia alihusishwa katika mpango wa babake wa kufidia upungufu wa hifadhi ya mafuta Dubai kupitia kuimarisha uchumi wake na kulifanya eneo hilo kuwa kituo cha biashara pamoja na utalii duniani.

Hii leo zaidi ya asilimia 95 ya mapato ya milki za kiarabu hayatokani na mafuta huku utalii ukichangia asilimia 20.

Idadi ya watu nchini Dubai imeongezeka kutoka 40,000 katika miaka ya sitini hadi milioni 3.3 , ikiwemo watu milioni 3.1 ambao hawatoki katika milki hiyo ya kiarabu, wengi ambao wanaishi katika mamia ya majumba marefu katika mji huo.

Mwaka 1990, Sheikh Rashid alifariki baada ya ugonjwa wa muuda mrefu uliotokana na kiharusi.

Alirithiwa na nduguye mkubwa Mohammed , Maktoum. Miaka mitano baadaye . Sheikh maktoum alitajwa kuwa mwanamfalme wa Dubai. Pia alijipatia kazi ya uendeshaji wa maswala ya kila siku ya Dubai.

Sheikh Mohammed alizaliwa 1949 nyumbani kwao huko katika eneo la Shindagha, karibu na mkondo wa bahari wa Dubai.

Alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto wanne wa Sheikh Rashid Al Maktoum , ambaye aliitawala Dubai kwa miaka 32 tangu 1958.

Baada ya kumaliza shule ya upili 1965, Sheikh Mohammed alihamia Uingereza katika shule ya masomo ya lugha huko Cambridge.

Sheikh huyo aliyekuwa na umri mdogo baadaye alihudhuria mafunzo ya miezi sita katika jeshi la Uingereza kama kadeti mjini Hampshire.

Mwaka 1968, baada ya kurudi Dubai, Shekih Mohammed aliandamana na babake katika mkutano na mtawala wa wakati huo wa Abu Dhabi Sheikh Zayed Al Nahyan, ambapo walikubali kufanya muungano ambao ulipelekea kuundwa kwaMuungano wa milki za kiarbu.

Baada ya UAE kupata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1971, Sheikh Mohammed aliteuliwa kuwa waziri wa ulinzi - wadhfa ambao hadi wa leo anaushikilia.