Virusi vya corona: Senegal yakanusha kuagiza dawa ya mitishamba kutoka Madagascar

Rais Andry Rajoelina
Maelezo ya picha, Rais Rajoelina ametaka wanafunzi wapewe kinywaji hicho kwa kiwango kidogo kila baada ya muda kwa siku.
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Senegali imekanusha madai kwamba imeagiza kile ambacho kinasemekana ni dawa ya virusi vya corona ambayo inapigiwa upatu na Rais wa Madagascar Andry Rajoelina, shirika la habari la RFI limeripoti.

Wiki jana, Shirika la Afya Dunia (WHO) lilisema hakuna ushahidi unaoonesha kwamba dawa hiyo ni tiba ya ugonjwa wa Covid-19 baada ya Rais kuizindua rasmi dawa hiyo ya mitishamba inayotengenezwa Madagascar.

Dawa hiyo iliyo kwenye chupa na chai za mitishamba vimekuwa vikinadiwa na rais baada ya kufanyiwa majaribio kwa zaidi ya watu 20 katika kipindi cha wiki tatu, mkuu wa wafanyakazi Lova Hasinirina Ranoromaro aliliambia shirika la BBC.

Ijumaa, Rais Rajoelina aliandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter, kwamba rais wa Senegal Macky Sall, ameagiza dawa hiyo.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Lakini chanzo kilichonukuliwa na RFI kimesema kwamba hakuna oda kama hiyo iliyoagizwa.

Bwana Sall ameandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter kwamba nchi yake inafuatilia utafiti huo kwa karibu.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Rais Rajoelina pia naye ameandika ujumbe kwamba rais wa Guinea-Bissau ametuma ndege tayari kuchukua dawa hiyo ya mitishamba aliyoagiza.

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Coronavirus
  • Coronavirus: Kwa nini ni hatari kugusa uso wako
  • Jinsi ya kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona
  • Majibu ya maswali 10 yanayoulizwa sana kuhusu coronavirus
  • Je unaweza kupata coronavirus mara mbili?
Banner

Kujibu uzinduzi wa dawa hiyo, WHO ilisema kwenye taarifa iliyotumwa kwa BBC, kwamba shirika hilo halipendekezi kujitibu kwa kutumia dawa yoyote... kama njia moja ya kuzuia au tiba ya ugonjwa wa Covid-19.

Shirika hilo lilirejelela matamshi ya Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Adhanom Ghebreyesus kwamba hakuna mkato katika kutafuta tiba ya uhakika ya kupambana na virusi vya corona.

Majaribio katika ngazi ya kimataifa yanaendelea kutafuta tiba stahiki ya kukabiliaba na virusi hivi, WHO iliongeza.