Virusi vya corona: Uganda kumrudisha nyumbani Mtanzania aliyeambukizwa corona

Museveni.

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa

Wizara ya afya nchini Uganda imethibitisha kuwa ipo katika harakati za kumtafuta raia wa Tanzania aliyepatikana na virusi vya corona kwa lengo la kumrudisha nyumbani.

Mtu huyo wa miaka 34, ambaye ni dereva wa lori kutoka Dar es Salaam, Tanzania aliwasili katika kituo cha mpakani cha Mutukula Aprili 16 ,2020.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya mtu huyo hakuonesha dalili zozote za Covid-19.

Hatua ya Uganda kuwarudisha makwao raia wa kigeni waliopatikana na ugonjwa wa corona imezua gumzo kali katika mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi hiyo.

Siku ya Alhamisi waziri wa Afya Ruth Jane Aceng alisema kuwa mataifa wanachama wa Muungano wa Afrika Mashariki yalikubaliana kila raia wa nchi hizo ambaye atakayepatika na virusi vya ugonjwa wa corona atarejeshwa nyumbani kwa matibabu.

Alisema kuwa Uganda kila siku huwapokea hadi madereva 3,000 wa malori kutoka mataifa ya kanda ya Afrika Mashariki na kwamba nchi hiyo haita weza kuwapa huduma za matibabu.

Unachohitajika kufanya ili kuzia mambukizi ya virusi hivi

Ijumaa ya Aprili 17, 2020, Uganda ilithibitisha kuwa na mgonjwa mmoja wa corona baada ya kufanyia uchunguzi sampuli 774 miongoni mwa sampuli kutoka kwa madereza wa maroli katika vituo vya mpakani kabla waingie nchini humo.

Sampuli 376 kati ya sampuli 774 zilizopimwa hazikupatikana kuwa na virusi vya corona.

Kufikia sasa Uganda ina jumla ya wagonjwa 55 wa Covid-19.

Coronavirus
Banner

Hatua zingine zilizochukuliwa Uganda

Mapema wiki hii Rais wa Uganda Yoweri Museveni aliongeza marufuku ya kutotoka nje kwa siku 21 zaida ana kusema kuwa hatua zote zilizotangazwa ilipotangazwa marufuku ya awali zitaendelea kama kawaida.

Hatua hizo ni pamoja na kuzuia kabisa mikusanyiko ya watu. Nyumba za ibada na taasisi zote za elimu zitaendelea kufungwa.

Watu pekee watakaoruhusiwa kutoka na kuendelea na shughuli zao ni wafanyakazi katika sekta muhimu kama afya, ulinzi na usalama, wafanyakazi wa benki na wanahabari.

Wanajeshi

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Amri ya kutokutoka nje nchini Uganda inasimamiwa na vyombo vya ulinzi

Usafiri wa umma na wa ndege za abiria pia umepigwa marufuku.

Magari ya mizigo pamoja na ndege za mizigo zinaruhusiwa kuendelea na shughuli zake. Hata hivyo marubani na wasidizi wao katika ndege za mizigo watawekwa katika maeneo maalumu chini ya uangalizi wa serikali.

Maelezo ya video, Virusi vya Corona: Jinsi marufuku ya misongamano inavyokumbana na vikwazo Afrika