New Zealand: Spika aongoza mjadala akiwa amempakata mtoto wa mmoja wa wabunge

Spika wa New Zealand Trevor Mallard ambembeleza mtoto wa mmoja wa wabunge wakati wa cradles an MP's baby during a debate

Chanzo cha picha, New Zealand Parliament

Maelezo ya picha, Spika wa bunge la New Zealand Trevor Mallard alisema" Mheshimiwa amejiunga nami" wakati wa mjadala
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 1

Spika wa bunge nchini New Zealand ameonekana akimpakata mtoto wa mmoja wa mmoja wa wabunge akiongoza mjadala katika bunge hilo la wawakilishi.

Trevor Mallard aliweka picha akiwa amempakata mtoto wa kiume wa mbunge Tāmati Coffey katika mtandao wake wa Twitter yake.

Bw. Coffey, ambaye ni mbunge wa Labour wa eneo la Waiariki, alitangaza kuzaliwa kwa mtoto wake, Tūtānekai Smith-Coffey, mwezi Julai.

Siku ya Jumatano Bw. Coffey alihudhuria vikao vya bunge na mwanawe kwa mara ya kwanza baada ya kurejea kazini kutoka likizo ya uzazi.

Wakati wa kikao hicho Spika Mallard alichukua jukumu la kumpakata mtoto pamoja na jukumu la spika.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Presentational white space

Picha hiyo ya Bw. Coffey akiwa amembeba mtoto bungeni iliwekwa na mbunge wa chama cha Green Gareth Hughes kwenye Twitter.

"Inapendeza sana kuwa na mtoto bungeni, hii ni kwa kweli ni nzuri sana @tamaticoffey," Bw. Hughes aliaandika.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Presentational white space

Akizungumza na Newshub, Bw. Coffey alisema "Napata usaidizi kutoka kwa wafanyikazi wenzangu wote Bungeni".

Coffey ni mbunge wa hivi punde kumpeleka mtoto wake bungeni, na kufuata mfano wa wanasiasa wengine duniani.

Lib Dem kiongozi wa Jo Swinson, ambaye alihudhuria vikao vya bunge na mtoto wake mwaka 2018, na Seneta wa Australia Larissa Waters, ambaye alimnyonyesha mwanawe bungeni mwaka 2017, ni miongoni mwa wabunge waliogonga vichwa vya habari kwa kuchukua hatua hiyo.

Mwezi September mwaka jana Waziri mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern aliandikisha historia kwa kuandamana na mtoto wake wakati akitoa hotuba yake ya kwanza katika mkutano wa Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.