Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanamgambo 250 wa IS waliondoka Raqqa
Uchunguzi uliofanywa na BBC nchini Syria umebaini kwamba wanamgambo 250 wa IS waliruhusiwa kuondoka katika mji wa Raqqa wakati ulipotekwa na wapiganaji wanaoungwa mkono na vikosi vya Marekani.
Wapiganaji hao walikuwa miongoni mwa watu elfu nne walioondoka katika mji huo, nyingi ya familia zikiwa za wapiganaji wa IS.
Inaaminika kuwa maelfu ya wapiganaji wa IS ambao sio wakaazi wa eneo hilo waliondoka pia.
Mji wa Raqqa ulishikiliwa na wapiganaji wa Iraq wanaoungwa mkono na vikosi vya Marekani mwezi uliopita huku baadhi ya wanamgambo wa IS wakidaiwa bado kuwemo katika mji huo.