Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanahabari mashuhuri Gauri Lankesh auawa India
Iliyochapishwa
Mwanahabari nchini India ambaye pia ni mwanasiasa wa mrengo wa kushoto nchini humo ameuawa kwa kupigwa risasi.
Gauri Lankesh aliyekuwa akihariri gazeti la kila wiki, alikutwa katika bwawa la kuogelea nyumbani kwake mjini Bangalore,huku damu zikiwa zimetapakaa.
Polisi wanasema amepigwa risasi mara mbili kichwani na watu waliovamia nyumbani kwake wakiwa na pikipiki.
Serikali imeyataja mauaji hayo kama kupunguza uhuru wa demokrasia.
Hakuna aliyekamatwa mpaka sasa.