Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu tisa wauawa katika mlipuko Mogadishu
Iliyochapishwa
Takriban watu tisa wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya bomu lililokuwa limetegwa kwenye gari kulipuka katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
Polisi wanasema gari lililokuwa na bomu hilo lililipuka wakati likielekea katika hoteli ya Posh Treats iliyopo katikati ya mji.
Mmoja wa mashuhuda amesema aliona miili kadhaa ikitapakaa baada ya tukio hilo.
Kundi la wapiganaji wa al-Shabaab limekiri kuhusika na shambulizi hilo.