Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maharamia waiachia huru meli pwani ya Somalia
Iliyochapishwa
Maharamia wa Kisomali wameiachia huru meli ya mafuta waliyokuwa wameikamata kwenye pemba ya Afrika siku ya Jumatatu bila ya kulipwa fedha.
Maafisa nchini Somalia wamesema wafanyakazi saba wa meli hiyo raia wa Sri Lanka waliachiwa pia bila ya kudhuriwa.
Meli hiyo ilikamatwa katika eneo la pwani ya Puntland siku ya Jumatatu, ikiwa ni mara ya kwanza katika eneo hilo katika kipindi cha miaka mitano.
Maharamia hao waliiachia meli hiyo baada ya mazungumzo yao na askari wanamaji wa Puntland.