Kurunzi ya Qatar 2022: Yafahamu mataifa matano yanayopigiwa chapuo kutwaa ubingwa

world cup

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa

Hizi ni taarifa kubwa kuhusu kombe la dunia jioni hii

1. Haya ni mataifa 5 yanayopigiwa chapuo Qatar

Brazil haijatwaa kombe la dunia tangu mwaka 2002, lakini mashindano ya mwaka huu ya Qatar 2022, yanaweza kubadili hali hiyo.

Brazil, mshindi mara tano wa kombe la dunia anapewa kipaumbele kwa kupata asilimia 16%, huku ikipewa nafasi kubwa ya kuingia fainali (25%).

Nyuma ya Brazil, ni Argentina yenye Lionel Scaloni (13% ) na ya tatu ni kwa kupewa nafasi ya nne ni Ufaransa (12%), Hisapnia (9%) na England (9%).

2. Mataifa yameanza kuwasili Qatar

world cup

England imewasili Qatar usiku wa Jumanne kuelekea fainali za kombe la dunia zinazoanza Jumapili. Kikosi cha watu 26 cha Gareth Southgate kilipaa kikitokea Birmingham.

Wales, Tunisia, Senegal, Iran, Korea Kusini na Australia ni miongoni mwa mataifa yaliyowasili yakiendelea na maandalizi ya mwisho mwisho kabla ya kuanza kwa fainali hizo.

world cup

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Japan ikiendelea na mazoezi kwenye uwanja wa klabu ya Al Sadd Sports

3. Hiki ndicho kikosi chenye thamani kubwa zaidi

ju

Chanzo cha picha, Getty Images

Kiosi cha England kinaongoza kwa thamni, kikiwa na thamani ya £1.31bn huku kiungo wake Jude Bellingham akiwa ni mchezaji mwenye thamani zaidi, kwa mujibu waCIES Football Observatory.

England imezipiku Brazil (£1.27bn) iliyoshika nafasi ya pili, Ufaransa ya tatu kwa thamani (£1.17bn) na ya tano ni Hispania (£1.05bn).

4. Hatuogopi kusema tutatwaa ubingwa Qatar

Nahodha wa England Harry Kane, ametamba kikosi cha three Lions kitatwaa ubingwa wa kombe la dunia mwaka huu.

Kane anasisititza kwambva ' hatuogopi' kusema. England mara ya mwisho kutwaa kombe la dunia ni mwaka 1966.

harry

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Harry Kane