Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tetesi za soka Ulaya Jumapili 28.04.2024
Bayern Munich wanapanga uhamisho mwingine wa kumnunua mlinzi wa Manchester City Muingereza Kyle Walker, baada ya kushindwa kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 msimu uliopita wa joto. (Star)
Mmiliki mwenza wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe amekutana na wakala bora Jorge Mendes, ambaye wateja wake ni pamoja na mmoja wa walengwa wa klabu hiyo katika kiungo wa kati wa Benfica na Ureno Joao Neves, 19. (Mirror)
Crystal Palace wako tayari kujiunga na mbio za kumsajili beki wa kati wa Wolfsburg Mfaransa Maxence Lacroix mwenye umri wa miaka 24 msimu huu wa joto. (Telegraph )
Arne Slot atateuliwa kuwa kocha mkuu wa Liverpool badala ya kuwa meneja katika mabadiliko ya muundo wa klabu. (Times)
Matumaini ya West Ham ya kumteua kocha wa zamani wa Wolves Julen Lopetegui kuchukua nafasi ya David Moyes kama meneja msimu huu yanaonekana kukamilika huku AC Milan wakikaribia kuafikiana. (Guardian)
Barcelona wanakaribia kumsajili kiungo wa kati wa Argentina Guido Rodriguez, 30, kutoka klabu nyingine ya La Liga ya Real Betis.(Sport - in Spanish).
Barcelona wanapanga kulinda mustakabali wa mlinzi wa kati Pau Cubarsi mwenye umri wa miaka 17 baada ya kupendekeza mkataba mpya kwa Mhispania huyo ambao unajumuisha kipengele cha kutolewa cha €500m (£423.2m). (AS)
Kiungo wa zamani wa Manchester United na Uhispania Juan Mata, 35, anaamini kuwa klabu yake ya zamani inapaswa kujenga timu yoyote ya baadaye karibu na Bruno Fernandes wa Ureno, 29. (ESPN)
Kipa wa Ujerumani Loris Karius, 30, ataondoka Newcastle United kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu. (Fabrizio Romano)
Juventus wanashughulikia mikataba ya kuongeza kandarasi za mshambuliaji wa Italia Federico Chiesa, 26, na mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 24. (Rudy Galetti).
Juventus wanashughulikia mikataba ya kuongeza kandarasi za mshambuliaji wa Italia Federico Chiesa, 26, na mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 24. (Rudy Galetti).