Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 22.03.2024
Manchester United wanamlenga kiungo wa Wolves Joao Gomes, 23, kuwa mbadala wa Mbrazil mwenzake Casemiro, 32. (Mirror).
Arsenal, Liverpool, Manchester City na Manchester United wote wanamtaka mshambuliaji wa Real Madrid, Rodrygo, 23, na miamba hao wa Uhispania wanaweza kushawishiwa kufanya mazungumzo iwapo watapokea ofa ya £85m. (Sport )
Liverpool wanapanga kumruhusu mlinzi wa zamani wa Cameroon Joel Matip, 32, kiungo wa zamani wa Uhispania Thiago Alcantara, 32, na mlinda lango wa Uhispania Adrian, 37, kuondoka msimu huu wa joto. (Football Insider)
Matumaini ya klabu ya Uhispania Getafe ya kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, kwa mkopo tena msimu ujao yanatazamiwa kukatizwa huku Manchester United wakihitaji mkataba wa kudumu iwapo wataamua kumwacha. (Sun)
Barcelona wako tayari kuwapa Everton chaguo la wachezaji wanne, winga wa Uhispania Ansu Fati, 28, mlinzi wa kati wa Ufaransa Clement Lenglet, 23, mlinzi wa kulia wa Marekani Sergino Dest na 20, kiungo wa zamani wa Uhispania Fermin Lopez, katika jitihada za kumpata kiungo wao wa kati wa Senegal aliyekadiriwa kuwa na thamani ya £80m Amadou Onana, 22. (Sport via Teamtalk)
Kiungo wa kati wa Uholanzi Teun Koopmeiners ameiambia klabu yake ya Italia Atalanta kuwa anataka kuondoka msimu huu wa joto, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 akihusishwa kuelekea Liverpool. (Metro)
Kazi ya meneja wa Manchester United Erik ten Hag iko salama kwa msimu uliosalia baada ya kumvutia Sir Jim Ratcliffe katika hatua za awali za wakati wa mmiliki mwenza mpya katika klabu hiyo. (Guardian)
Mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner, 28, tayari anataka kubadilisha mkopo wake kutoka RB Leipzig hadi Tottenham Hotspur kuwa uhamisho wa kudumu ambao unaweza kuigharimu klabu hiyo chini ya pauni milioni 15. (Telegraph)
Mshindi mara saba wa Ligi Kuu ya Manchester United Roy Keane anasema "niliona hilo likifanyika" alipoulizwa kuhusu klabu hiyo kuhusishwa na kocha wa Uingereza Gareth Southgate. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Ufaransa Alexandre Lacazette anavutiwa sana na vilabu vya Saudi Arabia na nahodha huyo wa Lyon mwenye umri wa miaka 32 anaweza kuwa nyota wa hivi punde wa Ulaya mwenye jina kubwa kuhamia huko mwishoni mwa msimu. (L'Equipe)
Newcastle wamekuwa wakimfuatilia mlinzi wa Feyenoord na Uholanzi Quilindschy Hartman, 22, huku wakitafuta kuongeza chaguo la mlinzi wa kushoto. (Football Transfers)
Mlinzi wa Manchester United na Uswidi Victor Lindelof, 29, anasema anaangazia kazi yake ya Red Devils na hana nia ya kuhamia Saudi Pro League. (Fotbollskanalen)