Nyuma ya pazi ya urembo unaokuwa wa kukuza makalio

- Author, Shona Elliott
- Nafasi, BBC
- Iliyochapishwa
- Muda wa kusoma: Dakika 5
Alice Webb alipokwenda kuongeza makalio ya Ki-Brazil (BBL) bila upasuaji - utaratibu unaohusisha kudungwa sindano ya kujaza jeli kwenye matako - katika kliniki moja mwezi Septemba 2024, alitarajia kumaliza kwa wakati na arudi nyumbani.
Lakini Alice, mwenye umri wa miaka 33, hakurudi nyumbani.
Mama huyo wa watoto watano alifariki chini ya saa 24 baada ya kudungwa sindano, na kuwa mtu wa kwanza nchini Uingereza kujulikana kufariki kufuatia zoezi hilo. Uchunguzi utafanyika katika msimu wa vuli ili kubaini chanzo cha kifo chake.
Hadithi yake imekuwa kitovu cha mjadala unaokua kuhusu tasnia ya urembo inayokua nchini Uingereza, ambapo sindano za urembo sasa zinapatikana kila mahali, kuanzia saluni za urembo, ofisi na vyumba vya hoteli.
Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, nimechunguza tasnia hii, nikifanya uchunguzi wa siri ili kujua kinachoendelea.
Nilikutana na wataalamu ambao walikuwa tayari kuingiza mamia ya mililita za jeli mwilini mwangu kutoka katika vyumba vya matibabu vya muda katika majengo ya ofisi. Nilipewa dawa bila ushauri unaofaa wa daktari na kuuziwa sindano za kupunguza uzito zisizo na lebo kwenye mitandao ya kijamii.
Nimezungumza na wanawake kadhaa ambao wameniambia kuhusu maumivu makali waliyoyapata yaliyosababishwa na sindano za vipodozi ambazo hutangazwa kuwa hazina maumivu na hazina hatari, na maambukizi yaliyotokana na hayo yaliyowapeleka hospitalini.
Huduma ya uidhinishaji wa vipodozi Save Face inasema imeshuhudia visa vingi vya madhara makubwa vinavyohusishwa na matibabu ya urembo - ikiwa ni pamoja na mgonjwa mmoja ambaye aliachwa bila uwezo wa kufunga macho yake baada ya upasuaji wa kope uliokwenda vibaya, na mwingine ambaye aliyetoboka utumbo wakati wa kufyonzwa mafuta.
"Ni jambo la kutisha sana, ni kama aina fulani ya filamu ya kutisha, lakini hizi ni taratibu zinazofanywa katika mitaa yetu," anasema mkurugenzi wa Save Face Ashton Collins.
Uingereza ni mojawapo ya masoko ya sindano za vipodozi yenye udhibiti. Tofauti na nchi nyingi za Ulaya, mtu yeyote anaweza kufunzwa kuingiza jeli kwenye ngozi na kutoa matibabu kwa umma.
Mambo yamebadilika

Chanzo cha picha, PA Media
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Juni 2024 Joanne (ambaye anataka tutumie jina lake la kwanza tu) alikwenda kuchomwa sindano ya kuongeza makalio katika kliniki moja huko Essex kwa sababu aliona ni hatari kwenda Uturuki kwa ajili ya upasuaji - hii ilikuwa kabla ya Alice kufariki.
"Nilitaka tu makalio makubwa," anasema Joanne, mama wa watoto wawili kutoka South Wales. Muda mfupi baada ya matibabu, ambapo alidungwa sindano ya lita 1 (painti 1.8) ya jeli, aliishia hospitalini akiwa na maambukizi kwenye damu. Miaka miwili baadaye, anasema bado ana makovu kwenye mapaja na makalio kutokana na sindano hiyo.
Sindano za vipodozi hapo awali zilihusishwa na watu matajiri, wa umri wa makamo wanaotafuta matibabu ya kupunguza kuzeeka, lakini urembo huo umeenea katika muongo mmoja uliopita.
Matibabu kama vile kujaza jeli katika ngozi, jeli ambayo kwa kawaida hutengenezwa kwa asidi ya hyaluroniki, ambazo hutumika kuongeza ujazo na umbo – sasa zinapatikana kwa urahisi na kutangazwa kama matibabu ya kawaida ya urembo.
Ashton Collins wa Save Face anaamini mitandao ya kijamii na televisheni zimechangia katika kuleta mabadiliko hayo: "Familia ya Kardashian, Love Island na mitandao ya kijamii walifanya iwe mtindo kwa wanawake vijana kuwa na midomo mikubwa, mashavu na nyuso zisizozeeka."
Ndiposa matibabu ya sindano yamezidi kupatikana kwa wingi na mara nyingi hutolewa katika saluni za urembo - jambo ambalo linaweza kuzifanya zionekane kama huduma za kawaida za urembo, kulingana na Collins.
"Watu wanaweza kuwa wanatengeneza kucha au nyusi zao na wanaona matibabu haya kama nyongeza ya hayo," anasema.
Collins anasema, watumiaji mara nyingi huzingatia urahisi, umaarufu na bei badala ya usalama.
"Tunagundua mara kwa mara kwamba watu hawajui kwamba Botox ni dawa inayotolewa kwa agizo la daktari pekee. Hawajui kwamba wanapaswa kupimwa na mtaalamu wa afya," anasema.
Yote haya yamesaidia kuchochea ukuaji wa ajabu katika sekta hii. Lakini Collins anasema pia wameunda watendaji wasio salama kuongezeka.
"Jinsi matibabu haya yanavyowasilishwa kwenye mitandao ya kijamii huondoa mtazamo wa uhatari wake," anasema.
Ukuaji wa kushangaza

Dkt. Alexander Zargaran, daktari bingwa wa upasuaji wa NHS na mtafiti katika Chuo Kikuu cha London, aliamua kupima ukubwa wa soko la dawa ya kuongeza makalio ya Botox.
Uchambuzi wake uligundua kuna karibu wataalamu 20,000 wanaofanya kazi kote Uingereza mwaka 2025, ikilinganishwa na zaidi ya wataalamu 3,500 waliotambuliwa mwaka 2023. "Tunajua kwamba sekta hiyo inakua," Zargaran anasema.
Kulingana na utafiti wake, idadi ya wataalamu wasio wataalamu wa urembo wa tiba iliongezeka maradufu kutoka 12% hadi 24.8% kati ya 2023 na 2025.
Utafiti huo pia uligundua kuwa matibabu ya Botox yanapatikana kwa wingi zaidi katika jamii zenye umaskini mwingi. Watu katika maeneo yenye umaskini mwingi wana ufikiaji mdogo wa wataalamu waliohitimu kimatibabu.
Tatizo ni kubwa

Siku nne baada ya kuchomwa sindano ya BBL katika kliniki ya Essex Oktoba 2023, Louise Moller mwenye umri wa miaka 28 kutoka Bolton alikimbizwa hospitalini akiwa na maambukizi ya damu.
Ili kuzuia kuenea mwilini mwake, madaktari wa upasuaji waliondoa sehemu kubwa za tishu zilizokufa kutoka kwenye tako lake la kushoto.
Janet, mama wa Louise aliripoti tukio hilo na daktari, lakini kwa sababu upasuaji ulifanyika Essex wakati Louise anaishi Greater Manchester, anasema aliambiwa kesi hiyo itahitaji kuchunguzwa.
Mamlaka pia imeonya mara kwa mara kuhusu bidhaa zisizo na leseni na bandia zinazoingia sokoni Uingereza. Polisi huko Ireland Kaskazini walikamata zaidi ya dawa bandia na zisizo na leseni 700,000 mwaka 2023, ikiwa ni pamoja na bidhaa za Botox.
Huko Glasgow, maafisa walipata maelfu ya lita za jeli, sindano na bidhaa za urembo wakati wa uvamizi uliohusishwa na biashara ya urembo.
Zaidi ya muongo mmoja baada ya Keogh Review kuonya kwamba jeli za kujaza ngozi ya matako ni "janga linalosubiri kutokea", wanaharakati wanasema tatizo tayari lipo.















