Tetesi za Soka Ulaya Alhamisi

Iliyochapishwa

Chelsea inaandaa dau la pauni milioni 38 kumnunua kiungo wa kati wa Sporting Lisbon na Ureno Matheus Nunes, ambaye pia analengwa na Wolves. .(A Bola - in Portuguese)

Arsenal wana uhakika wa kuipiku Manchester United kwenye usajili wa pauni milioni 30 wa kiungo wa kati wa Leicester na Ubelgiji Youri Tielemans, 25. (Sun)

Manchester United wametoa dau la pauni milioni 51 kumnunua mshambuliaji wa Ajax Mbrazil Antony, 22, lakini klabu hiyo ya Uholanzi inashikilia dau la £68m. (Goal)

Nottingham Forest inatumai kukamilisha mikataba ya mlinzi wa kushoto wa Bayern Munich Muingereza Omar Richards, 24, na mlinzi wa kulia wa Liverpool Neco Williams wa Wales, 21, ifikapo wikendi. (Athletic - subscription required)

Southampton pia wanavutiwa na Williams na wanatumai kumpiku Forest kwenye saini ya beki huyo. (Football Insider)

Everton wanajiandaa kumpa winga wa England chini ya umri wa miaka 21 Anthony Gordon, 21, mkataba mpya ili kuzuia nia ya Newcastle. (Times - subscription required)

The Toffees pia hawana nia ya kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Dominic Calvert-Lewin na wanaweza kumpa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 mkataba mpya pia. (Mirror)

Leeds wamewataka Barcelona kutoa ofa ya mwisho kwa Raphinha wiki hii kwani wanataka mustakabali wa mshambuliaji huyo wa Brazili kutatuliwa haraka iwezekanavyo. . (Sport - in Spanish)

Crystal Palace wana matumaini ya kuzishinda Everton na Nottingham Forest katika kumnasa kiungo wa kati wa Wolves Muingereza Morgan Gibbs-White, 22. . (Talksport)

Palace wako kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo wa kati wa Swansea Muingereza Flynn Downes, 23, kwa £8m.  (Mail)

Lakini West Ham pia wanajadili kuhusu mpango wa kumnunua Downes, ambaye alikuwa shabiki wa nyundo wa utotoni. (Sky Sports)

Arsenal wanataka kuuza wachezaji saba - akiwemo winga wa Ivory Coast na aliyesajiliwa kwa rekodi ya klabu Nicolas Pepe, 27, na mlinda mlango wa Ujerumani Bernd Leno - ili kufadhili matumizi ya wachezaji wengine wapya.  (Sun)

Fulham wako kwenye mazungumzo na The Gunners kuhusu kumnunua Leno mwenye umri wa miaka 30.  (West London Sport)

Tottenham wanakaribia kukamilisha usajili wa pauni milioni 15 wa beki wa pembeni wa England chini ya miaka 21 Djed Spence kutoka Middlesbrough. (Telegraph - subscription required)

Club Brugge imekataa ombi kutoka kwa Leeds kwa kiungo wa kati wa Ubelgiji Charles De Ketelaere, 21, ambaye angependelea kuhamia AC Milan. (HLN - in Dutch)

Kiungo wa kati wa Uingereza Jesse Lingard, 29, anatazamiwa kuruka kuelekea Marekani kufanya mazungumzo na timu mbili za Ligi Kuu ya Soka baada ya kuachiliwa na Manchester United mwezi uliopita.  (ESPN)

Wachezaji wa Uingereza watapokea bonasi ya pauni 55,000 kwa kila mchezaji iwapo watashinda Ubingwa wa Ulaya kwa Wanawake.  (Telegraph - subscription required)