'Ninahisi uchungu sana ninapoona wanyama wakubwa hivi wakianguka'
Iliyochapishwa
Vifo vya ndovu katika hifadhi ya kitaifa ya wanyamapori ya Amboseli Kusini mwa Kenya,
Vimeipa wasi wasi watu wa jamii ya Wamaasai ambao wanachukulia vifo hivyo kama tahadhari ya hali mbaya kwa mifugo wao.
Athari za kiangazi ni wazi huku wanyama wakipata tabu kupata lishe- ardhi ni kavu na jua halina huruma katika eneo hili.
Wanahabari wa BBC Ann Ngugi na Judith Wambare walitembelea mbuga hiyo na kupata
mizoga ya wanyamapori waliokufa kwa ajili ya hali ngumu iliyosababishwa na kiangazi hiki.









