Mbinu mpya za mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine zina ufanisi gani, na ni kipi kinatarajiwa siku zijazo?

Chanzo cha picha, Getty Images
Siku ya Alhamisi, jeshi la Urusi lilianzisha tena shambulizi kali la roketi dhidi ya Ukraine. Lakini wakati huu shambulizi hilo halikuwa kubwa tu, bali pia kwa viwango tofauti - lilifanywa mara moja na aina tofauti za makombora. Je! ni kwa njia gani mbinu za kuishambuliwa Ukraine na vikosi vya jeshi la Urusi zinaweza kubadilika?
Kati ya aina nane za makombora yaliyokuwa anga ya Ukraine Alhamisi usiku, mfumo wa ulinzi wa anga wa Ukraine sasa hauwezi kuangusha aina tatu. Tunazungumza juu ya Kh-47 "Dagger", Kh-22 na S-300 iliyorekebishwa kwa shambulio la malengo ya ardhini.
Wakati huu, kama wakati wa msimu wa baridi, Warusi walikuwa wakipiga mifumo ya nishati ya Ukraine na kujaribu kuharibu ulinzi wa anga wa Ukraine kwa makombora ya kukwepa rada kama Kh-31P.
Hata hivyo, chanzo cha BBC katika serikali ya Ukraine kilikuwa kimeonya siku chache kabla ya shambulio hilo kwamba madaraja na njia za reli zinaweza kuwa lengo la mashambulizi mapya makubwa.

Chanzo cha picha, CHERINIGOV REGION POLICER
Kwa kuzingatia kwamba haikuwezekana kuiingiza Ukraine katika giza, ambayo jeshi la Kirusi lilikuwa likitegemea, wakati wa msiumu baridi, itakuwa ni mantiki kudhani kwamba wakati huu inaweza kubadili kutoka kwa mifumo ya nishati hadi ile ya usafiri. Inajulikana kuwa jeshi la Urusi limetafuta kwa muda mrefu namna ya kukata njia za usambazaji wa silaha za Magharibi.
Kwa upande mwingine, kujaribu kupata busara katika vitendo vya jeshi la Urusi bado haijawa kazi ya kuridhisha sana.
"Warusi katika vita hivi mara nyingi wanaonyesha kutokuwa na mantiki kwa vitendo," Lakiychuk alisema katika mahojiano na BBC News Ukraine. "Kwa hiyo, haina mantiki kujaribu kutabiri kama adui atabadilika kutoka kuharibu miundombinu ya nishati hadi miundombinu ya usafiri."
"Mashabulizi ya mwaka jana ya majira ya joto-vuli kwenye miundombinu ya usafiri ya Ukraine yalionyesha ufanisi wao wa chini. Hata hivyo, ni lini hii iliwazuia Warusi?" - anaongeza Lakiychuk.
Kuanzia Aprili 2022, jeshi la Urusi lilirusha takriban makombora kumi na mbili kwenye daraja la ghuba karibu na mlango wa Dniester. Mamlaka za eneo hilo zilisema kwamba wakati huo daraja lilikuwa limeharibika vibaya na kwa na drone ya majini.

Chanzo cha picha, TELEGRAM
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Iliwachukua Warusi kushambulia kwa makombora saba kuharibu bwawa la miaka 90 la hifadhi ya Karachunovsky karibu na Krivoy Rog. Pia wanajeshi wa Urusi walijaribu kuharibu daraja karibu na Cherkassy katika msimu wa joto, lakini baadaye barabara na reli kupitia hapo vilirejeshwa.
Kwa upande wake, ilichukua vikosi vya Wanajeshi vya Ukraine wiki nyingi na mashambulizi ya mara kwa mara kwa kutumia mifumo ya Marekani ya HIMARS kufanya daraja la Antonovsky karibu na Kherson lisitumike na vikosi vya Urusi.
“Ni vigumu kugonga madaraja. Makombora hayana usahihi.,” mwangalizi wa kijeshi wa Ukraine Kirill Danilchenko alieleza mwezi Aprili mwaka jana.
Wakati wa a vita vikubwa, Urusi haikuweza kuharibu mawasiliano ya reli nchini Ukraine, ingawa ilijaribu kugonga vituo vidogo vya umeme: Mafundi wa Ukraine hufanya kazi haraka, na ambapo kuna hitaji muhimu, hutumia injini za dizeli.
Lakini, hii haimaanishi kuwa jeshi la Urusi halitafanya mashambulio mapya ya makombora kwenye madaraja na reli, Pavel Lakiychuk anaamini. Hasa ikizingatiwa kwamba wanajaribu kila mara kuboresha mbinu za kusmbulia, kama inavyoonyeshwa Alhamisi usiku.
Mbinu zilizoboreshwa

Chanzo cha picha, OK NORTH
"Kusema kwamba mbinu za makombora makubwa na mashambulio ya anga zimebadilika sana, nadhani, sio sahihi: adui anaendelea kuboresha mbinu za mashambulizi kwa wakati na kulenga pande kadhaa na silaha tofauti," Lakiychuk anabainisha.
Mtaalam huyu anasema kwamba Warusi walikuwa wakijiandaa kwa shambulio hili, kama inavyothibitishwa na mashambulizi ya mara kwa mara ya anga kutokana na "mafunzo" ya ndege za MiG-31K (zinazobeba makombora ya Kinzhal), na shughuli nyingine za anga za Kirusi na za kimkakati, zisizoambatana na kurusha makombora.
Katika muktadha huu, mtu anaweza pia kutaja puto juu ya mikoa tofauti ya Ukraine, madhumuni ambayo yalikuwa kufichua ulinzi wa anga wa Ukraine.
Ushahidi kwamba Urusi inaweza kuwa imeishiwa na akiba ya angalau aina fulani za makombora hutolewa kwa pause ndefu - kutoka kwa wiki mbili au zaidi - kati ya makombora makubwa ya eneo la Ukrain.
Kwa upande mwingine, madai kwamba Warusi wamemaliza usambazaji wao wa makombora ya masafa marefu yamesikika tangu Machi 2022.
"Kwa adui, suala la mipaka ya hifadhi au kiasi cha uzalishaji sio thamani kwake. Ili kutengeneza Kinzhals sita, viwanda vya jeshi la Kirusi vinahitaji miezi 3-6," anasema mchambuzi wa kijeshi wa Defense Express Ivan Kirichevsky.
"Viwanda vya jeshi la Urusi bado vinaweza kudumisha kiwango cha wastani cha uzalishaji wa hadi makombora 40 Kh-101 na hadi makombora 20 ya 3M-14 Caliber kwa mwezi, ingawa sio bila matatizo.
Kwa hivyo vikosi vya jeshi la Urusi vina uwezo wa kuongezea makombora mara baada ya kila mgomo mkubwa, ingawa sio haraka sana.
Mbali na hayo, Yuriy Ignat, msemaji wa amri ya Jeshi la Anga, aliita mabomu ya cruise kwamba jeshi la Urusi lina tishio jipya kwa Ukraine.
"Jeshi la anga la Urusi sasa linarusha mabomu yenye mabawa - mabomu ya angani yaliyokarabatiwa yenye mbawa na yenye uwezo wa kuruka makumi ya kilomita. Hivyo, ndege za Urusi hazihitaji kuingia katika eneo la ulinzi wa anga la Ukraine," Ignat alisema.
"Mabomu haya yanakuwa changamoto mpya kwetu. Tunahitaji kutumia mifumo ya makombora ya masafa marefu ya kuzuia ndege ili kuzuia kuonekana kwa ndege za Urusi karibu na mipaka yetu," jeshi lilionya.
"Mbinu mpya za Warusi zinatatiza kazi ya ulinzi wa anga. Lakini makombora hayo ambayo tunaweza kuyazuai kwa njia tuliyo nayo, kama unavyoona, yanapigwa. Na ufanisi, hata kwa makombora makubwa kama haya, ni ya juu sana. : makombora 34 kati ya 48 yaliangushwa, pamoja na kuongeza manne”, Yuri Ignat aliongeza.















