Vita vya Ukraine: Nini kilichotokea katika mlipuko wa kombora Poland?

Iliyochapishwa

Jeshi la Poland liliwekwa katika hali ya tahadhari siku ya Jumanne jioni baada ya kombora kutua katika eneo lake na kuua watu wawili.

Hatua hiyo ilijiri wakati Urusi iliporusha makumi ya makombora huko Ukraine na vikosi vya Ukraine vilijaribu kuyaangusha kwa makombora yake – ikiwa sehemu ya mfumo wake wa ulinzi wa anga.

Wakati mamlaka ya Poland - pamoja na washirika wa Nato - walipojaribu kubaini ukweli, timu ya uchunguzi ya BBC imekuwa ikichambua ripoti na kusoma picha kwenye mitandao ya kijamii ili kujaribu kufichua maelezo zaidi kuhusu tukio hilo.

Mlipuko huo ulikuwa wapi?

Mlipuko huo uliripotiwa kwa mara ya kwanza kwenye vyombo vya habari vya Poland Jumanne jioni, vikielezea mlipuko karibu na kijiji cha Przewodow, nchini Poland, takriban kilomita 6 kutoka mpaka wa Ukraine.

Ripoti za awali zilisema kuwa kombora hilo lilitua karibu na eneo la shamba ambalo wafanyikazi hupakia na kupima nafaka, na kuharibu jengo la karibu.

Tulikagua picha za satelaiti (ambazo zilionyesha shamba moja pekee katika kijiji) na kuzirejelea kwa njia tofauti na picha zilizopigwa eneo hilo Jumatano asubuhi ili kupata tovuti - ambayo imethibitishwa na mamlaka ya Poland.

Pia tulikagua video ambayo iliwekwa kwenye mitandao ya kijamii jioni ya Jumanne.

Inadai kuonyesha matokeo ya mara moja ya mlipuko kama kombora "lililoanguka kwenye eneo la Poland". Eeneo linalofuka moshi  linaweza kuonekana .

Kuna vidokezo vya kuona kwenye video ambavyo vinafanana na tovuti katika Przewodow.

Mchoro unaoonyesha picha ya skrini ya video na ramani ya eneo karibu na mlipuko

Barabara inayoonekana kwenye video (iliyoangaziwa na sisi kwa rangi nyekundu) ina muundo sawa na ile inayoonekana kwenye picha ya anga ya eneo hilo

Barabara mbele ya jengo la rangi nyepesi (iliyoangaziwa nasi katika machungwa).

Picha zilizopigwa ardhini siku ya Jumatano (zinazoonekana kwenye mchoro wa kwanza) zinaonyesha nyumba ya rangi nyepesi karibu na shamba hilo.

Na mimea na mistari ya miti inaonekana .

Tumejaribu kuwasiliana na mtu aliyechapisha video hii ili kuithibitisha zaidi lakini bado hatujapata jibu.

Picha kutoka kwa tovuti ya mlipuko pia zilianza kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii jioni ya Jumanne, zikionyesha moto na trekta na trela ilioharibika.

Ilikuwa vigumu kupata hizi peke yao kwa sababu ya giza na ukosefu wa dalili pana za kuona.

 

Lakini picha iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii na polisi wa Poland Jumatano asubuhi inaonyesha maafisa wakichunguza eneo la tukio. Trela ​​, nafaka zilizomwagika na uchafuuinaweza kuonekana kwenye picha zote mbili.

Picha nyingine iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii Jumanne usiku - ambayo ilisambazwa sana - inaonyesha kipande cha kombora ambacho kilidaiwa kupatikana katika eneo la tukio

Kulingana na picha hii pekee, BBC hadi sasa imeshindwa kuthibitisha kuwa ilipatikana katika eneo moja kwa sababu ya ukosefu wa vidokezo vya kuona kwenye picha.

Siku ya Jumatano, mwandishi wa BBC aliyeko katika eneo hilo hakuweza kufika karibu na eneo la tukio, ambalo limezuiwa na mamlaka ya Poland.

Tumewaonyesha wataalam wa ulinzi na kuwauliza kama wanaweza kufahamu ni aina gani ya kombora lililoanguka, na ni nani anayeweza kulirusha.

Mark Cancian, kutoka taasisi ya CSIS, anaamini kuwa inaweza kuwa kutoka kwa mfumo wa S-300. Aina hii ya kombora hutumiwa kwa mashambulio ya ardhi hadi angani, na limekuwa likitumiwa na Urusi na Ukraine wakati wote wa vita.

"Ni nani aliyerusha kombora hilo haijulikani," anasema J Andrés Gannon, mtaalam wa usalama katika Baraza la Mahusiano ya Kigeni la Marekani, ambaye anakubali kwamba huenda lilitoka katika  mfumo wa S-300.

"Tunajua Urusi imekuwa ikitumia S-300 kwa mashambulizi ya ardhini, ingawa ni mfumo wa ulinzi wa anga, lakini Ukraine pia inazitumia kwa ulinzi wa anga dhidi ya makombora ya kutoka angani."

Dkt Justin Bronk, mfanyakazi mwandamizi katika tanki ya wasomi ya Rusi, anakubali kwamba inaweza kuwa kutoka kwa mfumo wa S-300, lakini hakuna ushahidi wa kutosha kutambua bado.

Waziri Mkuu wa Poland alisema kuna uwezekano mkubwa kwamba kombora hilo lilirushwa na Ukraine wakati wakijitetea dhidi ya mashambulizi ya Urusi.

Rais wa Marekani Joe Biden amesema "haiwezekani" kwamba kombora hilo lilirushwa kutoka Urusi, huku matokeo ya awali ya maafisa wa Marekani yakionyesha kuwa lilirushwa na walinzi wa anga wa Ukraine.

Sehemu ya karibu zaidi ya Urusi kwenye eneo la mlipuko nchini Poland ni takriban kilomita 580 (maili 360), mbali zaidi ya eneo uliopo mfumo wa S-300 ambao wataalam wanasema ni karibu 90km (maili 56).

Ramani ya eneo la mlipuko

S-300 zinatumikaje?

Urusi na Ukraine zote zinamiliki silaha hizi za S-300 na hulaumiana kwa kusababisha uharibifu katika mashambulizi ya hivi karibuni

Raia wa Ukraine wanazitumia kutungua makombora ya Urusi, na Warusi wamedai kuwa haya yameanguka chini na kusababisha vifo vya raia.

Ni vigumu sana kujua asili ya kombora kutoka kwa uchafu wake, kulingana na wataalam wa silaha.

Kumekuwa na uvumi kwamba Urusi inaweza kuwa inalenga maeneo nchini Ukraine karibu na eneo hili la mpaka wa Poland.

Takriban kilomita 10 (maili 6) kutoka kijijini, kuvuka mpaka na kuingia Ukraine, kuna mtambo wa kuzalisha umeme wa Dobrotvirska.

Laini ya umeme inayotumika inayounganisha Poland na Ukraine pia iko karibu.

Urusi imekuwa ikilenga maeneo ya miundombinu kama haya na vikosi vya Ukraine vimekuwa vikitumia ulinzi wa anga kukabiliana nazo.

Tunaendelea kuchunguza tukio hili na tutasasisha nakala hii tutakapopata maelezo zaidi.