Rayan: Jinsi Morocco ilivyosubiri kwa hofu wakati mtoto alipotumbukia ndani ya shimo

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Firefighters work to rescue five-year-old Rayan, who became trapped in a deep well for days in Morocco's rural northern province of Chefchaouen

Chanzo cha picha, Getty Images

Shuguli ya kumuokoa mtoto mvulana mwenye umri wa miaka mitano Rayan Oram baada ya kutumbukia ndani ya shimo iliwaunganisha Wamorocco kwa siku kadhaa katika matumaini yao na maombi kwamba angepatikana akiwa bado hai.

Baba yake alikuwa akifanyia ukarabati shimo hilo katika mji mdogo wa kaskazini mwa Morocco unaoitwa Tamorot uliozingirwa na milima wakati Rayan alipotumbukia ndani yake Jumanne asubuhi. Kampeni ya mtandao ya #SaveRayan ilisambaa katika nchi nyingi, hata katika mahasimu wa Morocco, Algeria.

BBC haihusiki na dhana za mitandao ya nje yake

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Mtangazaji maarufu wa televisheni ya Morocco Rachid Allali hata alikatiza kipindi chake kwa ushirikiano na Rayan. Maelfu walikusanyika katika eneo la tukio kuwatia moyo waokoaji waliokuwa wakifanya kazi hiyo saa 24 wakitumia taa za mwanga mkubwa nyakati za usiku.

Bystanders watch as Moroccan authorities and firefighters work to rescue five-year-old boy Rayan, who is trapped in a deep well for over two days, near Bab Berred in Morocco's rural northern province of Chefchaouen on February 3, 2022.

Chanzo cha picha, AFP

Operesheni hiyo ilikuwa ngumu kutokana na mchanganyiko wa mwamba, udongo wa mchanga katika eneo hilo, ambavyo vilimaanisha kuwa kuingiliwa kokote kwa shimo hilo kungesababisha kuporomoka kwa udongo.

The site where rescuers worked to reach a five-year-old boy trapped in a well in the northern hill town of Chefchaouen

Chanzo cha picha, Reuters

Wahudumu wa dharura, wakiwemo wazima moto, walisaidia kufukua shimo kubwa pembeni mwa mlima kabla ya kuchimba handaki tofauti la mlalo kuelekea kwenye shimo katika jaribio la kumuokoa Rayan, aliyekuwa amekwama 32 kwenda chini (au futi 104) kupitia shimo hilo ambalo lilikuwa jembamba saa.

Unaweza pia kusoma:

Rescue crews work to reach five-year-old boy Rayan, who became trapped after falling into a well in Morocco

Chanzo cha picha, Getty Images

Miongoni mwa waokoaji, mwanaume mmoja alichaguliwa na kusifiwa kwa namna ya kipekee kwa jina Ba (Uncle) Ali Sahrawi, ambaye alijitolea kutumia ujuzi wake kusaidia kuchimba ili kumuokoa Rayan kwa kutumia shoka, baada ya kubainika kuwa ni hatari sana kutumia machine nzito.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

1px transparent line

Wahudumu wa uokoaji hatimaye walimfikia Rayan siku ya Jumamosi jioni, siku nne baada ya kutumbukia. Ambilansi iliyomchukua kwanza ilipokelewa na kelele za shangwekutoka kwa umati watu kabla ya taarifa ya Mfalme Mohammed VI wa Morocco kuthibitisha kifo chake . Baadaye aliwapigia simu wazazi wa rayan kuwapa rambirambi.

The body of five-year-old Rayan was taken from the scene in Morocco's Chefchaouen province by ambulance

Chanzo cha picha, EPA

Timu ya waokoaji ilishiikana mikono wakati wazazi wa Rayan walipoondoka kwenye eneo la tukio huku mwili wake ukichukuliwa.