Virusi vya corona:DRC wataka kujihakikishia usalama wa chanjo

Iliyochapishwa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeahirisha kampeni ya kutoa chanjo ya corona iliyokua ianze leo Jumatatu kwa hofu ya usalama wake.

DRC inaungana na baadhi ya nchi za Ulaya, zilizositisha utoaji wa chanjo hiyo, baada ya baadhi ya watu waliopatiwa kupata athari ya kuganda damu.

Taifa hilo limepokea dozi milioni moja na laki saba ya chanjo hiyo aina ya AstraZeneca na ilikuwa inatarajiwa kuanza zoezi la kuchanja watu leo. DRC inataka kujiridhisha kwanza na usalama wa chanjo hiyo.