Harambee Stars ya kenya yafuzu baada ya miaka 15
Timu ya taifa ya mpira wa miguu nchini Kenya, Harambee Stars ilifuzu kushiriki michuano ya Mataifa Bingwa Barani Afrika (AFCON) mwaka 2019.
Thibitisho kwamba Timu ya Taifa Harambee Stars imefuzu kwa michuano hiyo ya 2019 lilitangazwa baada ya kikao kisicho cha kawaida cha siku nzima cha Kamati Kuu ya Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF) jijini Accra, Ghana.
Kikao hicho kilithibitisha uamuzi wa kuitupa nje timu ya taifa ya Sierra Leone kutoka katika mechi za kufuzu kwa dimba hilo baada ya shirikisho lao kupigwa marufuku na Shirikisho la soka duniani FIFA.
Huku ikiwa imesalia mechi moja ya makundi kukamilika, Shirikisho la CAF liliafikia uamuzi wa kufutilia mbali matokeo yote yaliyohusisha na taifa hilo la Afrika Magharibi na hivyo kuliacha kundi hilo na timu tatu pekee.
Sierra Leone ilikuwa imecheza mechi mbili katika kampeini yao na kwa sababu haikuwa imekamilisha nusu ya mechi zote za kufuzu,
Shirikisho la CAF liliamua kufutilia mbali matokeo yote ya awali yaliyohusisha taifa hilo kulingana na kanuni za kufuzu.

Chanzo cha picha, AFP/GETTY IMAGES

