BBC idhaa ya Kiajemi imepokea video kutoka kwa wakazi wa Isfahan
Idhaa ya Kiajemi ya BBC inaripoti kwamba imetumwa video kadhaa zilizochukuliwa na wakaazi wa mkoa wa Isfahan katikati mwa Iran usiku kucha, ambapo vyombo vya habari vya serikali ya Iran vinaripoti kuwa milipuko imesikika.
Katika video moja iliyowekwa kwenye akaunti ya Instagram ya BBC Persian, sauti za kile kinachoonekana kuwa bunduki za kukinga mashambulizi zinaweza kusikika.