Marekani yatekeleza mashambulizi ya anga kwenye maeneo ya "Walinzi wa Mapinduzi ya Iran" nchini Syria
Marekani imesema kuwa imefanya mashambulizi ya anga kwenye vituo viwili vya Iran vilivyoko kusini mashariki mwa Syria, kufuatia mashambulizi ya hivi majuzi dhidi ya wanajeshi wake nchini Syria na Iran.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin amesema kuwa mashambulizi hayo yalifanywa dhidi ya maeneo "yanayotumiwa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na makundi yenye uhusiano na Iran."
Alisema katika taarifa: "Mashambulio hayo yalifanywa dhidi ya kituo cha mafunzo na jumba la kuhifadhi silaha karibu na miji ya Albukamal na Al Mayadin, mtawalia."
Aliongeza: "Rais hana kipaumbele cha juu zaidi kuliko usalama wa wafanyakazi wa Marekani, na aliamuru kuchukuliwa hatua leo ili kuweka wazi kwamba Marekani itajilinda yenyewe, wafanyakazi wake, na maslahi yake.
Siku ya Jumatano, Marekani ilianzisha "mashambulizi ya kujilinda" kwa kile ilichosema kuwa ghala la silaha linalotumiwa na Walinzi wa Mapinduzi ya Iran na vikosi vyake shirikishi katika eneo la Maysaloun mashariki mwa Syria.