Marekani yakanusha madai ya Putin kwamba nchi za Magharibi zilipanga maandamano dhidi ya Wayahudi katika uwanja wa ndege
Marekani imepuuzilia mbali madai ya Urusi kuwa "ya kipuuzi" kwamba ghasia dhidi ya Israel katika uwanja wa ndege wa Dagestan siku ya Jumapili ziliandaliwa na Ukraine na nchi za Magharibi.
Katika mkutano wa televisheni siku ya Jumatatu, Rais wa Urusi Vladimir Putin alisema tukio hilo limekuwa sehemu ya jaribio la kueneza "machafuko" nchini Urusi.
Mamia ya watu walivamia uwanja wa ndege wa Makhachkala kabla ya kuwasili kwa ndege kutoka mji mkuu wa Israel Tel Aviv.
Wengi walipeperusha bendera za Palestina na kuimba nyimbo za chuki dhidi ya Wayahudi.
Dagestan, jamhuri ya eneo la Urusi, ina idadi kubwa ya Waislamu, na tukio hilo linakisiwa kuchochewa na hasira juu ya mzozo wa Gaza.
Vikosi vya usalama hatimaye vilidhibiti hali hiyo, na zaidi ya watu 60 wamekamatwa, kulingana na mamlaka za eneo hilo.
"Matukio ya Makhachkala jana usiku yalichochewa kupitia mitandao ya kijamii, haswa kutoka Ukraine, na maajenti wa huduma maalum za Magharibi," Bw Putin aliambia mkutano wa Baraza la Usalama la Urusi.
"Ni nani anayeandaa machafuko mabaya na ni nani anayefaidika nayo leo, kwa maoni yangu, tayari imekuwa dhahiri.
Gavana wa Dagestan, Sergei Melikov, pia alisema ghasia hizo zimechochewa "kutoka eneo la Ukraine na wasaliti" kwa kutumia chaneli ya Telegram iitwayo Morning Dagestan.
Mengi zaidi kuhusu mzozo wa Israel-Gaza
Fuatilia moja kwa moja:Matukio ya hivi punde na kinachoendelea
Mauaji ya Kibbutz:Jinsi Hamas walivyofanya shambulio lisilofikirika
Kiini cha mzozo:Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina