Mzozo wa Israel na Hamas: Biden anasema 'hana imani' na idadi ya waliouawa Gaza
Rais wa Marekani Joe Biden alisema "hana imani na idadi ambayo Wapalestina wanaitumia" alipoulizwa kama Israel inafanya vya kutosha "kupunguza majeruhi ya raia" katika mkutano na waandishi wa habari hapo awali.
"Sina dhana kwamba Wapalestina wanasema ukweli kuhusu idadi ya watu waliouawa. Nina hakika watu wasio na hatia wameuawa, na ni garama ya kuanzisha vita," Biden aliwaambia waandishi wa habari Jumatano.
"Waisraeli wanapaswa kuwa waangalifu sana ili kuhakikisha kuwa wanazingatia kuwalenga watu ambao wanaeneza vita hivi. Na ni kinyume na maslahi yao wakati hilo halifanyiki. Lakini sina imani na idadi ambayo Wapalestina wanaitumia,” aliongeza.
Wizara ya afya inayosimamiwa na Hamas mjini Gaza inasema kuwa zaidi ya watu 6,500 sasa wameuawa tangu Oktoba 7, ikiwa ni pamoja na zaidi ya watoto 2,700.
Unaweza pia kusoma:
- Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
- Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
- Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
- Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
- Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas