Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Watoto wafariki katika msafara wa Wapalestina walioshambuliwa wakitoroka kaskazini mwa Gaza

’Miili kadhaa ikiwemo ya Watoto imetapakaa kwenye sakafu ya lori.Kando dimbwi la damu linatoa taswira ya ukatili uliotokea hapa’

Moja kwa moja

Yusuf Jumah

  1. 'Tunajaribu kutowashambulia raia' - jeshi la Israel

    Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Israel anasema kuna mambo anataka "kufafanua na kusisitiza na kuweka wazi kwa wingi".

    "Raia wa Palestina huko Gaza sio maadui zetu na hatuwalengi hivyo," Conricus anasema.

    "Tunajaribu kufanya jambo sahihi, tunajaribu kuwahamisha raia ili kupunguza hatari kwao."

    Anasema: "Inasikitisha sana na inasikitisha kwamba vyombo vingi vya habari vinazingatia matendo yetu badala ya kuweka jukumu kwenye chombo kinachoongoza ukanda wa Gaza, nacho ni Hamas."

    Anaendelea kusema: "Yote haya ni ya Hamas - tunakabiliana na hali hiyo. Tunajaribu kutowapiga raia au miundombinu yao."

    Kwa mujibu wa mamlaka ya Palestina, karibu watu 2,000 wameuawa katika kampeni ya Israel ya kulipua mabomu katika Ukanda wa Gaza tangu shambulio la Hamas wiki moja iliyopita.

    Jeshi la Israel linaishutumu Hamas kwa kujaribu kuwazuia Wagaza kuhama

    Jeshi la Israeli limetoka tu kufanya mkutano na waandishi wa habari uliorushwa moja kwa moja kwenye X, ambayo zamani ilijulikana kama Twitter.

    Lt Kanali Jonathan Conricus anasema jeshi la Israel "lilitangaza nia yetu mapema...kwa sababu tunataka raia wasiathiriwe na vita".

    "Sio adui zetu, hatujaribu kuua au kujeruhi raia wowote tunaopigana na Hamas," anasema.

    Anasisitiza kuwa haitaki kuumiza raia na iko vitani tu na Hamas.

    Anasema jeshi limeona watu wakisikiliza maonyo yao na kuondoka katika eneo hatari.

    Anasema "inasikitisha na inatia wasiwasi sana" kuona Hamas ikijaribu kuwazuia raia wa Palestina kuhama eneo hilo.

    Hamas inawashikilia mateka zaidi ya 120 - jeshi la Israel

    Jeshi la Ulinzi la Israeli limetoa sasisho juu ya hali ya mateka.

    "Kufikia wakati huu, IDF imethibitisha kuwa zaidi ya raia 120 wanashikiliwa mateka huko Gaza na kundi la kigaidi la Hamas,"ilichapisha kwenye X, ambayo zamani ilijulikana kama Twitter.

    'Tutasambaratisha Hamas' - jeshi la Israel

    Luteni Kanali Conricus anasema wanajeshi wa akiba wa Israel wako kwenye foleni kuzunguka Ukanda wa Gaza wakijiandaa kwa hatua inayofuata ya operesheni.

    "Lengo letu liko wazi kabisa, hatua ya mwisho ya vita hivi ni kwamba tutasambaratisha Hamas na uwezo wake wa kijeshi, na kimsingi kubadilisha hali ili Hamas isipate tena uwezo wa kuleta uharibifu wowote kwa raia au wanajeshi wa Israel."

    Anazungumzia tukio karibu na mpaka wa Lebanon ambalo tuliripoti hapo awali.

    "Wapiganaji wa Hezbollah walirusha kombora la kifaru kuelekea wanajeshi wa Israel, kukawa na vita vya muda mfupi na hatimaye hali ikatulia," anasema."Baadaye Hezbollah ilituma ndege zisizo na rubani nchini Israel na pia kurusha makombora ya kutoka ardhini hadi angani dhidi ya ndege za Israel."

    Anasema majaribio hayo mawili yalizuiwa kwa mafanikio lakini hali kwenye mpaka wa kaskazini "ingali ya wasiwasi".

    Mengi zaidi kuhusu mzozo wa Israel-Gaza

  2. Habari za hivi punde, Miili ya Waisraeli waliotoweka 'ilipatikana kutoka Gaza' - ripoti za vyombo vya habari

    Miili ya baadhi ya Waisraeli walionaswa na Hamas wakati wa shambulizi lake wiki moja iliyopita imepatikana na jeshi la Israel wakati wa shambulio la ardhini huko Gaza siku ya Ijumaa, magazeti ya Israel yanaripoti.

    Haaretz na Kituo cha Yerusalemu wanasema kuwa Jeshi la Ulinzi la Israeli lilipata idadi isiyojulikana ya miili, na kuirudisha katika eneo la Israeli, na kukuta baadhi ya vitu vya watu havipo.

    Vikosi vya askari wa miguu na wenye silaha vilishiriki katika uvamizi huo ambapo seli ya Hamas ambayo ilirusha makombora ya vifaru katika eneo la Israeli "ilitolewa", gazeti la Jerusalem Post linasema.

    "Hali ngumu zaidi ya utekaji nyara ambayo Israeli imewahi kukumbana nayo"

    Takriban mateka 150 waliokamatwa na watu wenye silaha wa Hamas kutoka kusini mwa Israel Jumamosi iliyopita wanaaminika kushikiliwa katika maeneo ya siri ndani ya Gaza.Miongoni mwao ni wanawake, watoto na wazee.

    Hamas ilikuwa imetishia kumuua mateka mmoja kwa kila wakati mashambulizi ya anga ya Israel yakiua raia bila ya onyo.Vyombo vya habari vya Israel vinaripoti kuwa wanajeshi waliokuwa wakivamia Gaza walipata miili na mali za baadhi ya watu waliotoweka.

    Hili linaiacha serikali ya Israel na mtanziko.Je, inajaribu misheni ya uokoaji kwa kutumia silaha, kitu kilichojaa hatari?Au inasubiri kwa muda mrefu zaidi, hadi Hamas itadhoofishwa na mashambulizi ya anga kiasi kwamba inaweza kuwa tayari zaidi kufanya makubaliano?

    Michael Milstein, ambaye alihudumu miaka 20 katika ujasusi wa kijeshi wa Israeli,alimwambia mwandishi wa usalama wa BBC Frank Gardner: "Hii ndiyo hali ngumu zaidi ya utekaji nyara ambayo Israeli imewahi kukumbana nayo katika historia yake".

    Mzozo wa Israel-Gaza:Mengi zaidi

  3. Blinken yupo nchini Saudi Arabia kwa nia ya kuzuia kuenea kwa mzozo wa Israel-Gaza

    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Anthony Blinken amewasili Saudi Arabia.Ni kituo chake cha tano katika ziara ya nchi sita za Kiarabu huku akijaribu kuzuia mzozo kati ya Hamas na Israel kuenea katika eneo hilo.

    Blinken anataka mataifa ya Kiarabu kulaani waziwazi Hamas na pia kuonyesha kujizuia juu ya majibu ya Israel.

    Lakini alipowasili Riyadh, wizara ya mambo ya nje ya Saudia ilitoa ukosoaji wake mkali dhidi ya Israel , ikilaani kile ilichokiita kuwalenga raia wasio na ulinzi.

    Wasaudi walikuwa kwenye mazungumzo ya kurejesha uhusiano na Israeli lakini inaonekana kuwa hatua hiyo imesitishwa sasa.

    Walianza tena uhusiano na Iran mapema mwaka huu, na mwana mfalme wa Saudia alizungumza kwa simu na rais wa Iran wiki hii.

    Blinken atataka kusikia kuhusu hilo kwa sababu anawaomba washirika wake kuionya Tehran dhidi ya kujihusisha na mzozo huo.

    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani pia atazuru Misri, ambayo inashiriki mpaka na Gaza.Hapo atajadili juhudi za kuweka korido kwa ajili ya misaada ya kibinadamu na kuweka maeneo salama kwa raia ndani ya Gaza.

    Mzozo wa Israel-Gaza:Mengi zaidi

  4. Israel yathibitisha uvamizi ndani ya Gaza

    Jeshi la Israel linasema kuwa limeanzisha mashambulizi ndani ya Gaza.Haya ndiyo tunayosikia kuhusu hatua za jeshi hilo:

    • Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) linasema limefanya uvamizi katika eneo la Gaza "kuondoa tishio la seli za magaidi na miundombinu".
    • IDF pia inasema wanajeshi walikusanya ushahidi ambao utasaidia kuwapata mateka.
    • Walichapisha video kwenye X, ambayo zamani ilijulikana kama Twitter,wakisema: "Jeshi la anga la Israel liliendelea kushambulia maeneo ya magaidi wa Hamas na kurusha makombora ya vifaru huko Gaza mara baada ya kutumika kushambulia Israel."
    • Jeshi la wanahewa lilisema IDF ilifanya uvamizi wa ndani katika Ukanda wa Gaza "kukamilisha juhudi za kusafisha eneo la magaidi na silaha" na kujaribu "kutafuta watu waliopotea".

    Siku ya machafuko huko Gaza

    Ni saa kumi na mbili kasorobo saa za Afrika Mashariki na haya ndiyo matukio ya hivi punde:

    • Raia wa Palestina wamekuwa wakikimbia kaskazini mwa Gaza kwa magari, nyuma ya malori na kwa miguu baada ya onyo la Israeli kwamba raia wanapaswa kuhamia kusini mwa Gaza ndani ya saa 24.
    • Takriban watu milioni 1.1 wanaoishi katika maeneo ya kaskazini wametakiwa kuondoka kabla ya mashambulizi ya ardhini yanayotarajiwa kufanywa na wanajeshi wa Israel.
    • Umoja wa Mataifa umelitaja agizo hilo kuwa la kutisha, huku Marekani ikiitaka Israel kuchukua kila tahadhari ili kuepuka kuua raia.
    • Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alisema anafanya kazi na Israel kulinda "maeneo salama" huko Gaza
    • Wapiganaji wa Hamas waliwateka nyara takriban watu 150 na kuwapeleka Gaza wakati wa mashambulizi dhidi ya Israel wiki moja iliyopita na kusababisha vifo vya watu 1,300.
    • Watu 1,900 wameuawa huko Gaza tangu Israel ilipoanzisha mashambulizi ya anga ya kulipiza kisasi, mamlaka zimesema
    • Kizuizi kamili kinatekelezwa huko Gaza, huku mafuta, chakula na maji yakiisha
    • Mwandishi wa habari wa shirika la habari la Reuters, Issam Abdallah, ameuawa alipokuwa akifanya kazi kusini mwa Lebanon

    Mzozo wa Israel-Gaza:Mengi zaidi

  5. Karibu tena

    Hujambo na Karibu tena katika habari zetu zinazoendelea za mgogoro wa Mashariki ya Kati, ambapo maelfu ya Wapalestina wamekuwa wakikimbia makazi yao kaskazini mwa Ukanda wa Gaza kabla ya hatua zaidi za kijeshi za Israel.

    Ni wiki moja sasa tangu wapiganaji wa Hamas wafanye shambulio la kushtukiza nje ya Gaza na kuua zaidi ya raia 1,300 na wanajeshi ndani ya Israel.

    Idadi ya waliofariki katika Gaza, kutokana na mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Israel, imeongezeka hadi 1,900.

    Mimi ni Yusuf Jumah na pamoja na wenzangu tutakuwa tunakuletea habari mpya zaidi kuhusu kile kinachotokea katika eneo hili na athari zake duniani kote.