Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Raia wakimbilia kusini mwa Gaza baada ya onyo la Israel
Mamia ya familia zinasafiri kwenye barabara kuu kutoka kaskazini kuelekea kusini mwa Gaza baada ya Israel kuwataka raia kuondoka kwa usalama wao.
Moja kwa moja
Marekani yatoa tahadhari ya usalama Kenya
Ubalozi wa Marekani, Nairobi nchini Kenya, umetoa tahadhari ya ugaidi, ikionya Wamarekani kupitia tena mipango yao binafsi ya usalama.
Katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wake binafsi Ijumaa, 13 2023 ilisema kuna hatari kubwa ya ugaidi ukilenga maeneo ambayo mara nyingi hutembelewa na raia wa kigeni na watalii katika eneo la Nairobi na kwingineko.
‘’Maeneo ambayo mara kwa mara hutembelewa na Marekani na raia wa kigeni wengine na watalii nchini Kenya, wanaendelea kuwa walengwa wa magaidi wanaopanga kufanya ugaidi,’’ Ubalozi umesema.
Ubalozi pia umetoa namba za mawasiliano ambazo raia wanaweza kupiga wakati wanapohitaji usaidizi wa aina yoyote.
Wapalestina wenye asili ya Kiafrika 'wanalengwa mjini Jerusalem'
Maelezo kuhusu taarifa - Author, Bushra Mohamed
- Nafasi, BBC News
Wapalestina wenye asili ya Kiafrika wanaoishi karibu na Msikiti wa al-Aqsa mjini Jerusalem wameiambia BBC kuwa wananyanyaswa na polisi wa Israel kufuatia shambulio baya la Jumamosi lililofanywa na wapiganaji wa Hamas dhidi ya jamii za Israel karibu na Ukanda wa Gaza.
Mousa Qous, mkuu wa Jumuiya ya Wafrika mjini Jerusalem, alisema anawafahamu Wapalestina wenye asili ya Kiafrika ambao wamepigwa na kudhalilishwa na kijana wa miaka 13 ambaye alikamatwa kwa saa kadhaa.
Bw Qous aliambia BBC wiki hii kwamba watu wachache kutoka kwa jamii yake wanatoka nje huku wakihofia kunyanyaswa na kukamatwa.
"Mpwa wangu alitoka nje leo kununua bidhaa kutoka kwa duka, lakini polisi wa Israeli walimzuia ili kupekua. Walipompekua kwa njia isiyofaa alipokataa, walimpiga," alisema.
"Tunaishi mkabala na lango la Msikiti wa al-Aqsa, polisi wa Israel walituzuia kuingia msikitini kwa ajili ya maombi na tunanyanyaswa na kunyanyaswa." Wapalestina wenye asili ya Afrika wengi wao wanatoka Chad, Nigeria, Senegal na Sudan na wamekuwa wakiishi Jerusalem kwa karne nyingi.
BBC imewasiliana na polisi nchini Israel kwa maoni lakini bado haijapata jibu.
Jaji wa Senegal aamuru Sonko arejeshwe kwenye orodha ya wapiga kura
Baada ya kesi kusikilizwa na mahakama siku ya Alhamisi, jaji aliamuru kiongozi wa upinzani wa Senegal Ousmane Sonko arejeshwe kwenye orodha ya wapiga kura.
Jina la Bw Sonko liliondolewa kwenye orodha ya waliostahili kupiga kura baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela mwezi Agosti.
Alipatikana kuwa alitenda kinyume cha maadili kwa mtu mwenye umri wa chini ya miaka 21, lakini alikanusha madai hayo, akisema kuwa kesi hiyo ilichochewa kisiasa.
Mawakili wa Bw Sonko walisema uamuzi wa jaji huyo Alhamisi ulimfungulia njia ya kuingia kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi wa urais utakaofanyika Februari mwaka ujao. Hata hivyo, hii haijathibitishwa.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyochapishwa Ijumaa, mawakili wa serikali walisema watakata rufaa dhidi ya uamuzi huo.
Kesi hiyo ilisikilizwa katika mahakama ya Ziguinchor, mji wa kusini ambapo Bw Sonko alikuwa kwenye orodha ya wapiga kura, na ambapo yeye ni meya.
Hukumu yake ya "kupotosha vijana" ilizua maandamano ya ghasia katika mojawapo ya mataifa ya Afrika yenye utulivu. Takriban watu 16 walifariki na mamia kujeruhiwa, kulingana na maafisa.
Mwishoni mwa Julai, kiongozi wa upinzani alifungwa kwa mashtaka mapya: kutoa wito wa uasi, njama ya uhalifu kuhusiana na biashara ya kigaidi na kuhatarisha usalama wa serikali.
Aliyekuwa mtumishi wa umma, Bw Sonko alipata umaarufu katika uchaguzi wa urais wa 2019, ambapo aliibuka wa tatu.
Polisi nchini Kenya waombwa kumkamata 'wakili bandia'
Mwanamume aliyeripotiwa kushinda kesi kadhaa nchini Kenya amekuwa akihudumu bila sifa ya uwakili, maafisa wa sheria wamesema.
Mwanamume huyo aliyetambulika kwa jina la Brian Mwenda amejitokeza katika shauri la televisheni kupitia televisheni.
Chama cha Wanasheria nchini Kenya (LSK) kinamshutumu Bw Mwenda kwa kujifanya wakili aliye na jina sawa na hilo, kwa kuchukua wasifu wake kwenye tovuti ya LSK.
Imewataka polisi kumkamata Bw Mwenda, ambaye bado hajazungumzia madai hayo.
China yafurusha 'idadi kubwa' ya waasi wa Korea Kaskazini - Seoul
Korea Kusini inasema China imewarejesha kwa lazima "idadi kubwa" ya waasi wa Korea Kaskazini.
Haya yanafuatia ripoti za hivi punde za mashirika ya kutetea haki za binadamu yanayodai kuwa kiasi ya raia 600 wa Korea Kaskazini wamerudishwa nchini mwao.
Korea Kusini ilisema Ijumaa kwamba ripoti hizo zinaonekana kuwa za kweli, lakini haikuthibitisha idadi kamili ya waliorejeshwa.
Human Rights Watch (HRW) ilisema walioasi, wengi wao wakiwa wanawake, wanaweza kukabiliwa na kifungo, unyanyasaji wa kingono au hata kifo punde tu watakapowasili huko Kaskazini.
Vyanzo vya habari nchini China vimeripoti kuwa mamia waliwekwa kwenye malori na kurejeshwa kutoka katika vituo walivyokuwa wamezuiliwa hadi Korea Kaskazini Jumatatu usiku.
"Msimamo wa serikali ni kwamba kwa hali yoyote hakuna Wakorea Kaskazini wanaoishi nje ya nchi watarudishwa kwa nguvu kinyume na matakwa yao. Kurejeshwa kwa lazima kinyume na matakwa ya mtu ni ukiukaji wa kanuni ya kimataifa ya kutorejeshwa kutoka uhamishoni," alisema Koo Byoung-sam, msemaji wa Korea Kusini, Wizara ya Muungano.
Kutorejeshwa nyumbani kunamaanisha kuwa wakimbizi na wanaotafuta hifadhi wasirudishwe katika nchi ambako wanaweza kukabiliwa na mateso.
Bw Koo alisema Korea Kusini imeandamana hadi China na kusisitiza msimamo wake lakini alikataa kutoa maelezo zaidi.
Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu nchini Korea Kaskazini Elizabeth Salmon anakadiria kuwa takriban raia 2,000 wa Korea Kaskazini wanazuiliwa nchini China kwa kuvuka mpaka bila kibali.
China haiwatambui waasi wa Korea Kaskazini kama wakimbizi. Inadai wao ni "wahamiaji wa kiuchumi" na ina sera ya kuwarudisha, licha ya maombi kutoka kwa serikali za kigeni na mashirika ya haki za binadamu kufikiria upya msimamo wake.
Alipoulizwa kuhusu kurejeshwa kwao, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Wang Wenbin alisema siku ya Alhamisi "hakuna kitu kama kile kinachojulikana kama 'waasi wa Korea Kaskazini' nchini China".
Alisema Beijing inashikilia "mtazamo wa kuwajibika" kwa Wakorea Kaskazini wanaoingia China kinyume cha sheria kwa sababu za kiuchumi, kulingana na Reuters.
Pia unaweza kusoma:
Al-Qaeda yatangaza kifo cha waliyemshika mateka raia wa Mali
Kundi la Al-Qaeda tawi la Afrika Magharibi limetangaza kifo cha waliyemshika mateka raia wa Mali akiwa chini ya ulinzi wake, na kumtaja kwa jina la Idriss Sanogo na kusema alifariki kutokana na ugonjwa ambao haukutajwa.
Kundi la Jamaat Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM) lilituma salamu za rambirambi kwa familia ya mwanamume huyo.
JNIM pia ililaumu serikali ya Mali, ikisema imeshindwa kujadili kuachiliwa kwa Bw. Sanogo.
Kundi hilo lilitangaza habari hiyo katika taarifa fupi siku ya Alhamisi kupitia mitandao ya kijamii.
Ilitoa taarifa kidogo kuhusu Bw Sanogo, mbali na kusema alizaliwa mwaka wa 1952 na alitekwa nyara na wanamgambo wa JNIM katika mji wa Timbuktu nchini Mali miaka mitatu iliyopita.
Mapema Mei 2020, vyombo vichache vya habari viliripoti kutekwa nyara kwa afisa huyo wa serikali - katika eneo la Timbuktu - akimtaja kama "Drissa Sanogo" na "Idrissa Sonogo".
Hadi Alhamisi, JNIM haikuwa imetaja hadharani kuwa inamshikilia Bw Sanogo.
Katika taarifa yake ya hivi punde zaidi, kundi la al-Qaeda lilisema serikali "inawajibika kikamilifu" kwa kifo cha Bw Sanogo, likisema Bamako "alipuuza kesi yake... licha ya kujua hali ya afya yake".
Kundi hilo la wanamgambo lilisema mahitaji yake ni "rahisi" na "yanajulikana kwa wote": "mkomboe ndugu yetu, tunamwachilia ndugu yako" - na kupendekeza kwamba kundi la wanajihadi limetaka kuachiliwa kwa mmoja au wanamgambo wake kadhaa kwa mabadilishano na Bwana Sanogo.
Serikali ya Mali bado haijajibu lolote kutokana na kauli ya JNIM.
Taasisi inayolenga Afrika ya Mafunzo ya Usalama (ISS) ilisema katika ripoti ya hivi majuzi kwamba utekaji nyara wa watu wa ndani nchini Mali na Burkina Faso umeongezeka, na kuishutumu JNIM kwa kuwa mhusika mkuu.
Pia unaweza kusoma:
- Mali: Kipi kifuatacho kwa nchi inayotegemea Wagner kwa usalama wake?
Raia wawili wa Afrika Kusini wauawa katika vita vya Israel na Hamas
Raia wawili wa Afrika Kusini wameuawa katika mzozo unaoendelea kati ya Israel na Hamas.
Idara ya Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini (Dirco) ilitoa habari hiyo Ijumaa, lakini haikufichua ni nani waliofariki.
"Idara ya Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano inaweza kuthibitisha kwamba raia wawili wa Afrika Kusini wamefariki katika mzozo huu unaoendelea kati ya Palestina na Israel," alisema msemaji wa Dirco Clayson Monyela.
"Mchakato wa uthibitishaji kwa sasa unaendelea kwa sababu mmoja wa watu hao ameripotiwa kuwa na nambari ya kitambulisho cha Israeli, kwa hivyo tunahitaji kubaini kama ana uraia pacha."
Akizungumza kwa niaba ya serikali, Bw Monyela alitoa rambirambi kwa jamaa za watu hao.
Alisema: "Shughuli zetu huko Ramallah na Tel Aviv ni kuratibu juhudi na pia kutoa usaidizi wa kibalozi na huduma kwa familia za raia wetu."
Vita hivyo vilianza baada ya wanamgambo wa Hamas kufanya shambulio baya dhidi ya Israel mwishoni mwa juma.
Zaidi ya watu 2,700 nchini Israel na Gaza wameuawa tangu wakati huo.
Katika picha: Wagaza wahama makazi yao
Picha za watu katika Jiji la Gaza wakipakia na kuhama kutoka kwa nyumba zao zinaendelea kuibuka, baada ya Israeli kutaka wahamie kusini.
Miongoni mwa wanaojaribu kutorokea usalama ni watoto. Takriban nusu ya wakazi wa Gaza wako chini ya miaka 18.
Burkina Faso kutia saini mkataba wa nishati ya nyuklia na Urusi
Burkina Faso na Urusi zimeratibiwa kutia saini mkataba wa maelewano (MoU) kwa ajili ya ujenzi wa kinu cha nyuklia katika taifa hilo la Afrika Magharibi, kulingana na shirika la habari la serikali la AIB.
Makubaliano hayo yatakuwa kilele cha mazungumzo ya mtawala wa kijeshi wa Burkina Faso, Kapteni Ibrahim Traoré, na Rais wa Urusi Vladimir Putin mwezi Julai, wakati wa mkutano wa kilele wa Urusi na Afrika mjini Moscow.
"MoU itatiwa saini kati ya Rosatom, wakala wa shirikisho wa nishati ya atomiki ya Urusi, na wizara ya nishati ya Burkina Faso, pembezoni mwa Wiki ya Nishati ya Urusi 2023," AIB ilisema.
Takriban 20% ya wakazi wa Burkina Faso wanapata umeme - ikiwa ni ya viwango vya chini zaidi duniani, kulingana na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA).
Baada ya kutofautiana na washirika wake wa jadi wa Magharibi, ikiwa ni pamoja na Ufaransa, Burkina Faso imegeukia Urusi kwa msaada wa kiuchumi na kijeshi.
Maelezo zaidi:
- Utawala wa Burkina Faso unasema ulizuia jaribio la mapinduzi
- Kwanini Urusi inashangilia mapinduzi ya Burkina Faso
- Ibrahim Traore: Mfahamu kiongozi mpya wa kijeshi Burkina Faso
DR Congo kulegeza vikwazo katika eneo lililokumbwa na migogoro
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo italegeza vikwazo katika maeneo mawili yenye migogoro ambayo yamewekwa chini ya udhibiti wa kijeshi - kimsingi sheria ya kijeshi - imekuwa ikitumika kwa miaka miwili.
Rais Félix Tshisekedi alisema katika hotuba ya televisheni Alhamisi usiku kwamba ameamua "kupunguza polepole na kwa kasi" vikwazo katika majimbo ya mashariki ya Kivu Kaskazini na Ituri.
Hali ya kuzingirwa iliwekwa mnamo 2021 ili kukandamiza machafuko katika eneo hilo. Rais alisema ataondoa amri ya kutotoka nje iliyowekwa, kuruhusu watu na bidhaa kusafiri kwa uhuru na kurejesha haki ya maandamano na mikusanyiko ya amani.
Inakuja miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu, utakaofanyika tarehe 20 Disemba, ambapo Bw Tshisekedi anawania kuchaguliwa tena.
"Hili ni muhimu zaidi kwani wahusika mbalimbali wanaohusika katika mchakato wa uchaguzi wana haki ya kushiriki kikamilifu na bila vikwazo," alisema.
Hatua ya kuzingirwa kwa maeneo hayo imekosolewa na mashirika ya kutetea haki za binadamu ambayo yanasema imesababisha kuzuiliwa kwa watu wengi na vikwazo vya harakati.
Kenya inapanga kutuma ujumbe Haiti kabla ya kupeleka huko vikosi vyake
Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya amesema kuwa nchi hiyo itatuma wajumbe wa tathmini hali nchini Haiti kabla ya kupeleka maafisa wa polisi kushughulikia ghasia za magenge huko.
"Kutakuwa na ziara nyingine za kabla ya kutuma polisi nchini Haiti na wadau mbalimbali kabla ya maafisa wetu kwenda huko," Waziri wa Mambo ya Ndani Kithure Kindiki aliiambia kamati ya bunge siku ya Alhamisi.
Mnamo Agosti, Kenya ilituma ujumbe wake wa kwanza wa kubaini ukweli nchini Haiti.
Bw Kindiki pia alisema kuwa maafisa hao wana vifaa vya kukabiliana na magenge ya Haiti kwani walitumwa ni kufanikiwa katika nchi kadhaa hapo awali, ikiwa ni pamoja na Namibia, Kambodia, iliyokuwa Yugoslavia, Bosnia na Herzegovina, Croatia na Sierra Leone.
Aliongeza kuwa maafisa wa polisi ni sehemu ya vikosi vya usalama vya Kenya vilivyotumwa hivi sasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Somalia na Sudan Kusini.
Hata hivyo, amesema kuwa kupelekwa kwao Haiti kutafanyika baada kukidhivigezo vyote vya sheria, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa na bunge na seneti.
Wiki iliyopita, Umoja wa Mataifa uliidhinisha kupelekwa kwa maafisa wa polisi wa Kenya nchini Haiti lakini mahakama ya Kenya Jumatatu ilisimamisha kwa muda, hatua hiyo, ikisubiri uamuzi kubaini iwapo ni ya kikatiba au la.
Tazama: Picha za ndege zisizo na rubani zinaonyesha athari ya mashambulizi ya anga ya Israel
Picha za ndege zisizo na rubani za BBC zinaonyesha athari za mashambulizi ya anga ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza.
Zaidi ya watu 1,300 wameuawa katika mashambulio hayo kufikia sasa.Idadi ya vifo nchini Israel imefikia 1,300 baada ya mashambulizi ya Jumamosi.
Israel imesema kuwa imeweka zuio kamili - ikiwa ni pamoja na lile la usambazaji wa chakula, mafuta na vitu vingine muhimu - kwa Gaza kwani mashambulizi hayataondolewa hadi mateka waachiliwe.
Unaweza pia kusoma:
- Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
- Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
- Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
- Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
- Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
Orodha Kamili: Droo za hatua ya makundi ya Afcon 2023
Droo ya hatua ya makundi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2023 imefanyikamjini Abidjan, Cote d'Ivoire Alhamisi jioni.
Super Eagles ya Nigeria itachuana na wenyeji Cote d'Ivoire pamoja na Guinea-Bissau na Guinea.
Timu 20 zitashiriki katika shindano lililocheleweshwa ambalo litatozwa Januari 13 na Februari 11, 2024.
Droo ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2023:
Ifuatayo ni droo ya Kombe la Mataifa ya Afrika, iliyofanyika Abidjan, Ivory Coast, Alhamisi
- Kundi A
vory Coast (wenyeji), Nigeria, Equatorial Guinea, Guinea-Bissau
- Kundi B
Misri, Ghana, Cape Verde, Msumbiji
- Kundi C
Senegal (wamiliki), Cameroon, Guinea, Gambia
Kundi D
Algeria, Burkina Faso, Mauritania, Angola
- Kikundi E
Tunisia, Mali, Afrika Kusini, Namibia
- Kundi F
Morocco, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Zambia, Tanzania
Washindi wote wa makundi na washindi wa pili na timu nne zilizo katika nafasi ya juu katika nafasi ya tatu zinafuzu kwa hatua ya muondoano.
Shule tatu za Kiyahudi mjini London zitafungwa kutokana na hofu ya usalama
Shule tatu za Wayahudi kaskazini mwa London zinafungwa leo, baadhi zikitaja maandamano yaliyopangwa kuwaunga mkono Wapalestina.
Wazazi katika shule moja waliambiwa kuwaficha watoto wao ndani kwa sababu ya "hatari ya vurugu mitaani".
Shule ya sekondari ya Menorah, Shule ya Msingi ya Torah Vodaas na Ateres Beis Yaakov, zote za Barnet, zimetuma barua kwa wazazi kutangaza kufungwa.
Jumuiya ya Usalama wa Jamii, shirika linalotoa ushauri wa kiusalama kwa Wayahudi wa Uingereza, lilisema shule zinapaswa kubaki kuendelea na masomo.
Japan yaomba mahakama kufuta kanisa la 'Moonies' kutokana na mauaji ya Shinzo Abe
Serikali ya Japan imeiomba mahakama kuamuru kuvunjwa kwa kanisa ambalo lilichunguzwa baada ya mauaji ya waziri mkuu wa zamani Shinzo Abe, vyombo vya habari vya nchini humo vimeripoti.
Mauaji ya ghafla ya Abe Julai mwaka jana yalipelekea kuchunguzwa kwa Kanisa la Unification , linalojulikana zaidi kama "Moonies".
Mtu aliyemshambulia Bw Shinzo, Tetsuya Yamagami, alisema kanisa lilimfilisi mama yake na alimlaumu Abe kwa kuliendeleza.
Kanisa linasema limetukanwa bila makosa kuhusu mauaji ya Abe.
Uchunguzi huo, ambao uliamriwa na Waziri mkuu wa Fumio Kishida, ulidumu kwa mwaka mmoja.
Yamagami alidai mama yake alilazimishwa kuchangia kanisa, ambapo alikuwa mshiriki kwa miongo mitatu. Madai sawa na hayo yamekuwa mada ya kesi zenye thamani ya mamilioni ya dola.
Chini ya Sheria ya Mashirika ya Kidini ya Japani, dini inaweza kufutwa ikiwa vitendo vyake "vitatambuliwa kwa uwazi kuwa vinadhuru kwa kiasi kikubwa ustawi wa umma".
Umoja wa Mataifa unaomba dola milioni 294 ili kukidhi mahitaji ya dharura ya Wapalestina
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu imetoa ombi la dharura ikizitaka nchi kutoa $294m (£241m) kwa ajili ya ufadhili wa dharura wa mahitaji ya haraka zaidi ya Wapalestina.
Fedha hizo zitatumika kuwasaidia baadhi ya watu milioni 1.2, shirika hilo lilisema.
Zaidi ya watu 84,000 katika mji wa Gaza walikosa makazi siku ya Alhamisi, shirika hilo lilisema, na kuongeza kuwa sasa kuna zaidi ya watu 423,000 wasio na makazi huko.
"Wakazi wengi katika Ukanda wa Gaza hawana tena maji ya kunywa kutoka kwa watoa huduma au maji ya nyumbani kupitia mabomba," shirika hilo lilisema.
Kati ya wanawake wajawazito 50,000 wa mkoa huo, karibu 5,500 wanatakiwa kujifungua ndani ya mwezi ujao. "Wanatatizika kupata huduma muhimu za afya kwani wafanyakazi wa afya, hospitali na kliniki zinashambuliwa."
Umoja wa Mataifa hapo awali ulisema unahitaji dola milioni 502 kufadhili shughuli za misaada ya Wapalestina mwaka 2023 lakini ni chini ya nusu ya lengo malengo hayo yaliyotimizwa.
Unaweza pia kusoma:
- Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
- Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
- Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
- Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
- Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
Tazama: CCTV ikionyesha wakati wanawake wakitoroka shambulio la Kibbutz Israeli
Picha za CCTV zinaonyeshajinsi wanawake wawili walivyoponea shambulio katika kibbutz huko Yachini, Israel siku ya Jumamosi.
Video hiyo inaonekana kuwaonyesha wakiwa wamekwama kwenye mapigano na kisha kukimbila kwa ajili ya usalama wao, baada ya makabiliano ya risasi kati ya wanamgambo wa Hamas na Jeshi la Ulinzi la Israel. Haijabainika ni nini kilimtokea mshambuliaji wa Hamas mwenye silaha.
Idadi ya vifo nchini Israel imefikia 1,300 baada ya mashambulizi ya Jumamosi. Zaidi ya watu 1,300 wameuawa katika mashambulizi ya anga ya Israel huko Gaza.
Unaweza pia kusoma:
- Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
- Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
- Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
- Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
- Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
Mkataba wa Marekani na Iran wa dola $6bn chini ya uangalizi kufuatia shambulio la Hamas dhidi ya Israel
Muandamanaji anayeunga mkono serikali ya Iran mjini Tehran akijumuika na sherehe za shambulio la Hamas dhidi ya Israel
Marekani inasema Iran haijapata pesa zilizokubaliwa katika kubadilishana wafungwa huku Ikulu ya White House ikikabiliwa na ukosoaji kuhusu mpango huo kbaada ya madai kwamba Tehran ilianzisha shambulio la Hamas dhidi ya Israel wikendi iliyopita.
Washington ina "maelewano ya kimya" na mpatanishi kati ya Qatar kutotoa $6bn (£.4.9bn) kutoka kwa mapatano hayo, inaripoti mshirika wa BBC wa Marekani CBS.
Ujumbe wa Iran katika Umoja wa Mataifa ulisema Marekani haiwezi kukataa makubaliano hayo.
Marekani imesema haina ushahidi juu ya uhusiano wa moja kwa moja wa Iran na shambulio la Hamas.
Dola bilioni 6 za ufashili wa mafuta ya Iran zilizokuwa zikishikiliwa nchini Korea Kusini hazikuzuiliwa mwezi Septemba kama sehemu ya makubaliano yaliyopelekea kuachiliwa kwa raia watano wa Marekani na Iran wakiachiliwa baada ya kutekwa nyara.
Mzozo wa Israel na Palestina: Nini kinatokea sasa?
Habari za asubuhi kwa wasomaji wetu. Haya ndio unayofaa kujua
- Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameliambia bunge kuwa "siku ngumu zinakuja" wakati wa kuapishwa kwa baraza lake jipya la mawaziri la vita.
- Umoja wa Mataifa unasema Gaza inakabiliwa na hali "mbaya" kutokana na chakula na maji kuisha haraka na wajawazito 50,000 hawawezi kupata huduma muhimu.
- Wakati huo huo Shirika la Afya Ulimwenguni linasema wafanyakazi 11 wa matibabu wameuawa huko Gaza tangu Jumamosi
- Zaidi ya watu 1,400 wameuawa huko Gaza tangu Israel ilipoanzisha mashambulizi ya anga ya kulipiza kisasi, huku watu 338,000 wakikimbia makazi yao.
- Idadi ya Waisraeli waliouawa na Hamas wakati wa mashambulizi yake mwishoni mwa juma imeongezeka hadi 1,300, huku mateka wasiopungua 150 wakipelekwa Gaza.
- Wakati huo huo, waziri wa habari wa Israel, Galit Distel Atbaryan, amejiuzulu - akisema ufadhili wa idara hiyo utatumika vyema kwingineko.
- Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya Ursula Von Der Leyen atazuru Israel siku ya Ijumaa kuelezea mshikamano wake na wahanga wa mashambulizi ya Hamas.
- Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin pia anasafiri kuelekea Israel siku ya Ijumaa- siku moja baada ya ziara ya waziri wa mambo ya nje Antony Blinken.
- Polisi nchini Ufaransa wamepiga marufuku maandamanoyote ya Wapalestina kwa sababu "yana uwezekano wa kuleta fujo" kwa utulivu wa umma.