Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Putin: Mzozo wa Israel ni mbaya - lakini Iran haijahusika

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kinachoendelea Israel ni "kibaya", huku akitoa wito kwa pande zote mbili kupunguza mauaji ya raia.

Moja kwa moja

Ambia Hirsi

  1. Zana za kijeshi za Marekani zawasili Israel

    Ndege ya kwanza iliyobeba zana za kijeshi za Marekani imewasili hivi karibuni katika Kambi ya Nevatim kusini mwa Israel, kulingana na mamlaka za eneo hilo.

    "Ushirikiano kati ya wanajeshi wetu ni sehemu muhimu ya kuhakikisha usalama wa kikanda na utulivu wakati wa vita," Jeshi la Ulinzi la Israeli lilisema katika taarifa iliyochapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

    Kundi la washambuliaji la USS Gerald R Ford pia limewasili Mashariki mwa Mediterania.

  2. Tazama: Droni yanasa picha ya kuvutia ya kundi la kondoo wanaovuka barabara kuu ya Marekani

    Picha za angani zinaonyesha kondoo wakitembea kwa mpangilio huku wakiongozwa kwenye barabara kuu na wakulima watatu na mbwa.

    Baada ya kuvuka barabara, wanyama hao wanaendelea kuchungwa shambani.

    Video hii yaa kuvutia lilichukuliwa karibu na jiji la Othello, katika jimbo la Washington, Marekani.

  3. Marekani, Israel na Misri wajadili 'njia salama' kwa watu wa Gaza

    Marekani inazungumza na Israel na Misri kuhusu njia salama kwa raia wa Gaza huku Israel ikiendelea kuishambulia Palestina.

    "Tumezingatia swala hili, kuna mashauriano yanaendelea," mshauri wa usalama wa kitaifa wa Marekani Jake Sullivan aliwaambia waandishi wa habari katika Ikulu ya White House.

    Bw Sullivan hakutoa maelezo zaidi, akisema tu kwamba majadiliano "kati ya mashirika ya uendeshaji" yanaendelea.

    Wizara ya Afya ya Gaza imesema Wapalestina wasiopungua 900 wameuawa na hadi 4,600 wamejeruhiwa tangu Jumamosi.

  4. Mzozo wa Israel na Palestina Israel yajibu mashambulizi ya Syria kwa mizinga: Jeshi

    Jeshi la Israel limesema limejibu kwa mizinga baada ya makombora kurushwa kwenye eneo la Golan Heights, eneo ambalo Israel inakalia kwa mabavu tangu mwaka 1967.

    "Askari wanajibu kwa mizinga na makombora kuelekea eneo lilipotokea shambulio hilo nchini Syria," ilisema taarifa ya jeshi la Israel.

    Jeshi linadai kumekuwa na "idadi ya mashambulizi kutoka Syria ndani ya eneo la Israel".

    Msemaji wa jeshi ameliambia shirika la habari la AFP kuwa inaonekana kuwa ni moto wa chokaa.

    Hii ilikuwa mara ya kwanza kurushiana risasi kati ya Israel na Syria tangu Hamas ilipoanzisha mashambulizi dhidi ya Israel kutoka Ukanda wa Gaza uliozingirwa siku ya Jumamosi.

    Siku ya Jumanne, Israel pia ilirushiana risasi na wanamgambo wa kusini mwa Lebanon.

    naweza pia kusoma:

    • Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
    • Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
    • Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
    • Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
    • Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
  5. Tazama: Mapigano ya makombora na bunduki ndani ya Gaza na Israeli

    Tangu Hamas iliposhambulia Israel siku ya Jumamosi, zaidi ya watu 1,700 wameuawa kwa kupigwa risasi na mashambulizi ya anga.

    Tazama ndani ya Gaza na Israeli wakati wa mapigano.

    naweza pia kusoma:

    • Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
    • Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
    • Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
    • Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
    • Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
  6. 'Hamas ilianzisha vita hivi. Tutaimaliza': Mshauri mkuu wa Israeli

    Mshauri mkuu wa Benjamin Netanyahu ameiambia BBC Newsnight kwamba Israel lazima "ijibu kwa nguvu" Hamas.

    Akizungumza kutoka Jerusalem, Mark Regev, ambaye pia aliwahi kuwa Balozi wa Israel nchini Uingereza, alisema nchi hiyo imeshtuka na wanataka ukweli thabiti zaidi katika eneo hilo.

    “Hamas walianzisha vita hivi. Tutaimaliza na tutaimaliza kwa masharti yetu,” alimwambia Mhariri wa masuala ya Kidiplomasia wa BBC, Mark Urban.

    "Ningeuliza watu wengine, raia wa Uingereza, wa nchi nyingine yoyote, ungefanya nini ikiwa watu wako 1,000 waliuawa kwa siku moja?" alisema.

    "Waziri Mkuu amelinganisha hili na mashambulio ya Septemba 11 nchini Marekani. Lakini ukiangalia ukubwa wa idadi ya Waisraeli na kulinganisha na Wamarekani ... lilikuwa shambulizi baya zaidi kuliko Septemba 11."

    "Ikiwa Israeli haitajibu kwa nguvu, ninahofu kwamba litakuwa funzo katika eneo hili kwamba - unaweza kuipiga Israeli bila kuadhibiwa - hiyo haikubaliki."

    naweza pia kusoma:

    • Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
    • Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
    • Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
    • Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
    • Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
  7. Habari za hivi punde, Mzozo wa Israel na Palestina: Idadi ya Waisraeli waliouawa yafikia 1,200

    Idadi ya vifo nchini Israel imeongezeka hadi 1,200, shirika la utangazaji la umma la Kan limesema. Waathirika walikuwa raia, iliongeza.

    Wakati huo huo Wizara ya Afya ya Palestina imesema watu 770 wameuawa katika Ukanda wa Gaza tangu Israel ilipoanzisha mashambulizi yake ya kulipiza kisasi siku ya Jumamosi.

    Zaidi ya watu 4,100 wamejeruhiwa.

    Unaweza pia kusoma:

    • Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
    • Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
    • Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
    • Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
    • Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas
  8. Hujambo na karibu tena kwa matangazo yetu ya mubashara ya leo, ikiwa ni tarehe 11.10.2023