Mzozo wa Israeli na Hamas: Picha za hivi punde kutoka Gaza na Israel

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Waziri wa ulinzi wa Israel aagiza "kuzingiwra kamili" kwa Ukanda wa Gaza: "Hakuna umeme, hakuna chakula, hakuna mafuta"
Ambia Hirsi and Yusuf Jumah

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters

Chanzo cha picha, Reuters
Picha za video zinaonyesha jengo likishambuliwa na watu wakikimbia kujificha wakati wa shambulio la kombora la Israeli katika kitongoji cha makazi kaskazini magharibi mwa Gaza.
Mashambulizi ya anga ya Israel yamesababisha vifo vya takriban watu 313 katika Ukanda wa Gaza, na karibu 2,000 kujeruhiwa, maafisa wa Palestina wanasema.
Video imeibuka inayodaiwa kuwaonyesha Wapalestina wakiruka kwenye kifaru cha Israel kilichotekwa na wanamgambo wa Hamas.
Picha hizo, zilizopatikana na shirika la habari la Reuters, pia zinaonyesha wanamgambo wakiingia Gaza kwa kile kinachosemekana kuwa gari la kijeshi la Israel lililotekwa.
Msemaji wa jeshi la Israel alikataa kutoa maoni yake kuhusu Waisraeli kukamatwa na Hamas, kulingana na Reuters. BBC haijathibitisha video hiyo.

Chanzo cha picha, Reuters
Makumi ya mahujaji wa Mauritius wamekwama mjini Bethlehem kufuatia mzozo wa unaoendelea kati ya kundi la wanamgambo wa Palestina Hamas na Israel, wizara ya mambo ya nje ilisema.
Kikundi kinajumuisha washiriki 36, haswa kutoka parokia ya Kikatoliki ya St-Hélène katika jiji la pili kwa ukubwa la Curepipe.
Padre Gérard Mongelard, ambaye anaongozana nao, alisema waumini hao wanaendelea vizuri na kwa sasa wanaishi katika hoteli moja mjini Bethlehem.
Walitakiwa kupanda ndege Jumapili jioni kuelekea Uturuki, ambapo wangerudi nyumbani.
Hata hivyo, mashirika mengi ya ndege yalisitisha safari za ndege kutokana na mashambulizi ya kijeshi ya Hamas dhidi ya Israel.
Unaweza pia kusoma:
Wenye magari walijificha wakati mapigano ya bunduki yakizuka kwenye barabara kuu ya Route 4, kati ya Ashdodi na mpaka wa Gaza.
Mapigano kati ya wanajeshi wa Israel na wanamgambo wa Kipalestina yanaendelea katika ardhi ya Israel karibu na Gaza kufuatia shambulio kubwa la Hamas siku ya Jumamosi.
Picha zinaonyesha matokeo ya mashambulizi ya anga ya Israel huko Gaza, ambapo msikiti uliharibiwa kabisa.
Israel ilianzisha mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya Hamas baada ya kundi hilo la wanamgambo kuanzisha mfululizo wa mashambulizi siku ya Jumamosi, ikiwa ni ongezeko kubwa zaidi katika eneo hilo katika miongo kadhaa.
Kwa mujibu wa maafisa wa Palestina, mashambulizi ya anga ya Israel yameua takriban watu 313 katika Ukanda wa Gaza, na karibu 2,000 kujeruhiwa.
Huko Israel, zaidi ya watu 600 wameuawa, na makumi ya Waisraeli wamechukuliwa mateka.

Chanzo cha picha, Getty Images
Vikosi vya Israel bado vinapambana na wapiganaji wa kundi la Hamas katika maeneo saba hadi nane kusini mwa Israel karibu na Ukanda wa Gaza, Jeshi la Ulinzi la Israel limesema katika kikao fupi leo asubuhi.
Maeneo haya ni pamoja na Be'eri, katika jamii ya wakulima, ambayo yalipenywa na wapiganaji wa Hamas mara moja. Wengi wa wanamgambo hao wameuawa, lakini wengine bado wamejificha katika nyumba za kibbutz, IDF ilisema.
Jeshi la Israel limeongeza kuwa limeshambulia zaidi ya maeneo 1,000 huko Gaza.
"Upeo wa operesheni hii ni kitu tofauti kabisa... Inachukua muda zaidi kuliko tulivyotarajia kurudisha mambo katika hali ya ulinzi na usalama," Luteni Kanali Richard Hecht aliambia mkutano na waandishi wa habari.
Idadi ya waliofariki katika tamasha la muziki la Supernova imeongezeka hadi 260, vyombo vya habari vya Israel viliripoti, vikinukuu shirika la uokoaji la eneo hilo Zaka.
Takriban watu 3,000 waliohudhuria tamasha la usiku kucha walilengwa na Hamas kama sehemu ya shambulio kubwa la kushtukiza dhidi ya Israel.
Tamasha hilo lilifanyika katika jangwa la Negev, karibu na Kibbutz Re'im - sio mbali na Ukanda wa Gaza.

Watu wengi wanahofiwa kupotea katika mji mkuu wa Cameroon Yaoundé, baada ya maporomoko ya ardhi kuharibu nyumba kadhaa katika mtaa unaoitwa Mbankolo.
Hii ni baada ya mvua kubwa kunyesha katika jiji hilo Jumapili jioni.
Bado haijulikani ni watu wangapi wamekufa au hawajulikani waliko hadi sasa, lakini msako unaendelea ili kuwaokoa waathiriwa na kupata wengine ambao hawajulikani walipo.
Mnamo Novemba mwaka jana, maporomoko ya ardhi katika mji mkuu yaliwaua takriban watu 14 waliokuwa wakihudhuria mazishi.
Kwa wiki kadhaa, wapenzi wa muziki waliochangamka walikuwa wakitazamia kwa hamu tamasha la Supernova, lililofanyika jangwani kusini mwa Israeli ili sanjari na sherehe ya Kiyahudi ya Sukkot.
"Wakati umefika ambapo familia nzima inakaribia kukusanyika tena," waandalizi waliandika kwenye mitandao ya kijamii kabla ya kuanza. "Na ni furaha gani itakuwa!"
lakini saa chache baadaye, kurasa zao za mitandao ya kijamii sasa zimefurika watu waliokata tamaa wakijaribu kutafuta wapendwa wao, baada ya wanamgambo wa Kipalestina kuvamia tamasha hilo na kufyatua risasi ikiwa ni sehemu ya shambulio la kushtukiza dhidi ya Israel.
Zaidi ya miili 250 imeripotiwa kupatikana katika eneo la tamasha, kulingana na shirika la uokoaji Zaka.
Mshiriki mmoja wa sherehe, anayeitwa Ortel, alisema ishara ya kwanza kwamba kuna kitu kibaya ni wakati king'ora kilipolia alfajiri, kuonya kuhusu roketi.
Walioshuhudia walisema kuwa roketi hizo zilifuatwa haraka na milio ya risasi.
"Walizima umeme na ghafla wakatoka [wanamgambo] ndani wakiwa na milio ya risasi, wakifyatua risasi kila upande,"aliiambia televisheni ya Israel - Channel 12
Magaidi 50 walifika wakiwa kwenye magari ya mizigo, wakiwa wamevalia sare za kijeshi," alisema.
Unaweza pia kusoma:
Iran "haikuhusika" katika shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa Hamas kusini mwa Israel, ujumbe wake katika Umoja wa Mataifa umesema.
"Tunasimama kwa nguvu katika kuunga mkono Palestina; hata hivyo, hatuhusiki katika shambulio la Palestina, kwani linatekelezwa na Palestina yenyewe," ilisema katika taarifa ya Jumapili, kulingana na Reuters.
Hamas hapo awali ilisema kwamba msaada kutoka kwa Iran uliisaidia kutekeleza shambulio la alfajiri mwishoni mwa juma.
Iran imekuwa ikiunga mkono Hamas kwa miaka mingi na kuwapa wapiganaji wake silaha na mafunzo - na kundi hilo la wanamgambo limesema kuwa msaada uliisaidia kutekeleza mashambulizi yake yaliyoratibiwa.
Lakini Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken aliiambia CNN Jumapili kwamba serikali ya Marekani "bado haijaona ushahidi kwamba Iran ilielekeza au ilikuwa nyuma ya shambulio hili".
Unaweza pia kusoma:

Chanzo cha picha, PA Media
Marekani inasema inahamisha shehena ya ndege, meli na jeti hadi mashariki mwa Mediterania na pia itaipa Israel vifaa na risasi zaidi.
Hii inafuatia shambulio la Hamas kusini mwa Israel, ambalo Rais Biden aliliita "shambulio lisilokuwa na kifani na la kutisha".
Marekani pia ilikuwa ikifanya kazi ya kuthibitisha ripoti kwamba raia wake walikuwa miongoni mwa waliouawa na kuchukuliwa mateka, Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken amesema.
Israel inasema zaidi ya watu 700 wameuawa na 100 kutekwa nyara.
Mjini Gaza, zaidi ya watu 400 wameuawa kufuatia mashambulizi ya anga ya kulipiza kisasi ya Israel, kulingana na maafisa wa Palestina.
Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alisema meli ya kubeba ndege ya USS Gerald R. Ford, meli ya kubebea makombora na zana za kuharibu makombora vimepelekwa katika eneo hilo. Ndege za kivita za Marekani pia zinapelekwa Gaza.
Misaada zaidi ya kijeshi kwa Israel itatumwa katika siku zijazo, Ikulu ya White House ilisema.
Rais wa Iran Ebrahim Raisi ameeleza kuunga mkono shambulio la Hamas akisema Israel inapaswa kuwajibika kwa kuhatarisha eneo hilo.
Mzozo wa Israeli na Hamas: Mengi zaidi:

Chanzo cha picha, EPA
Zaidi ya Wapalestina 123,000 wameyakimbia makazi yao huko Gaza kuanzia saa tatu usiku kwa saa za eneo (18:00 GMT), huku karibu 74,000 wakitafuta hifadhi mashuleni, Umoja wa mataifa unasema katika taarifa yake Jumapili usiku.
Israel imejibu mashambulizi ya kushtukiza ya Hamas kwa mfululizo wa mashambulizi ya anga katika eneo la Gaza.
Ukanda wa Gaza unakaliwa naw atu takriban milioni 2.3 na ni moja ya maeneo yenye msongamano mkubwa zaidi wa watu ulimwenguni.
Maafisa wa afya wa Palestina wanasema kuwa zaidi ya watu 400 wameuawa, huku zaidi ya 2,000 wakijeruhiwa.
Unaweza pia kusoma:
Ikulu ya White House inasema Wamarekani "kadhaa" wameuawa nchini Israel, ingawa hakuna idadi maalum iliyotolewa.
Msemaji wa Baraza la Usalama la Taifa anasema serikali ya Marekani inafuatilia kwa karibu hali hiyo na inaendelea kuwasiliana na mamlaka za mitaa nchini Israel.
Unaweza pia kusoma:

Chanzo cha picha, Getty Images
Asante kwa kujiunga na matangazo yetu ya moja kwa moja
Muda mfupi uliopita, tulipokea uthibitisho kutoka kwa jeshi la Israel kwamba zaidi ya watu 700 huko wameuawa katika mashambulizi baada ya shambulio kubwa lililoratibiwa na wanamgambo wa Hamas lililoanza mapema Jumamosi.
Mzozo wa Israeli na Hamas: Mengi zaidi: