Kuogelea baharini na nyoka: Mwanamume mmoja nchini Australia alitozwa faini ya zaidi ya dola 2000.
Nchini Australia, mwanamume mmoja ametozwa faini baada ya kumchukua nyoka aliyemhifadhi nyumbani kuogelea baharini.
Igor Fayoza alijulikana sana katika vyombo vya habari vya Australia wakati huo, wakati video zilizochukuliwa akiwa na nyoka wake baharini zilipochapishwa.
Katika picha hizo, inaonekana bwana Fayoza akiwa amembeba kwenye nyoka , ambaye anaogelea baharini.
Shirika la sayansi na mazingira la Australia limesema kuwa kumpeleka nyoka huyo baharini kunaweza kuwa tishio kwa watu wengine na pia kuna uwezekano kuwa nyoka huyo akawadhuru watu
Lakini Higur Feuza, ambaye amempeleka nyoka kwenye maji ya bahari takriban mara kumi, anasema, "Huwa ninampeleka ufukweni, anapenda sana maji. Sikumoja nilienda naye kwenye ubao wa kuogelea ambao ni inafurahisha sana." alitoa."
Bada ya video za Feijoza kuchapishwa kwenye mtandao, mamlaka ya Wakala wa Ulinzi wa Mazingira wa eneo la Queensland nchini Australia walianza kumchunguza na kumtoza faini ya zaidi ya dola 2,300 kwa hatua hii.