Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Wanajeshi 25 wauawa katika mlipuko wa bomu Somalia - Jeshi

Chanzo cha kijeshi cha Somalia kimeiambia BBC kwamba wanajeshi 25 wameuawa baada ya mwanamume mmoja kujilipua katika kambi ya Chuo cha Jale Siad

Moja kwa moja

  1. Benjamin Netanyahu hospitalini kabla ya kura kuu ya mageuzi tata ya mahakama Israeli

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amefanyiwa upasuaji wa dharura wa kuweka kifaa cha kudhibiti moyo, baada ya kufikishwa hospitalini Jumamosi usiku.

    Madaktari katika Kituo cha Matibabu cha Sheba walisema matibabu yalifanyika vizuri na hayuko katika hali ya kutishia maisha.

    Kulazwa kwa Bw Netanyahu kunakuja kabla ya kura kuu ya bunge kuhusu marekebisho tata ya mahakama.

    Maandamano ya kupinga mageuzi hayo yameikumba Israel, huku wafanyakazi wengi wakiahidi kugoma iwapo mswada huo utaendelezwa.

    Katika hotuba yake ya video kabla ya upasuaji huo wa usiku kucha, Bw Netanyahu alisema alikuwa anahisi "vizuri" lakini anawasikiliza madaktari wake.

    Kumekuwa na maswali juu ya afya yake baada ya kulazwa hospitalini wiki iliyopita akidaiwa kuwa na upungufu wa maji mwilini.

    Operesheni hiyo ilifanyika vyema "bila matatizo yoyote," Profesa Roy Beinart kutoka Kituo cha Matibabu cha Sheba alisema, akiongeza kuwa Bw Netanyahu "hayuko katika hali ya kutishia maisha".

    Ofisi yake ilisema Bw Netanyahu ataachiliwa Jumatatu, lakini safari zilizopangwa kwenda Cyprus na Uturuki zitapangwa upya.

    Bw Netanyahu alisema anafaa kuwa mzima vya kutosha kuhudhuria bunge baada ya utaratibu huo. Saa 48 zijazo zinatarajiwa kupigiwa kura muhimu kuhusu mipango ya serikali yake kuhusu mabadiliko katika idara ya mahakama.

    Kumekuwa na miezi kadhaa ya maandamano nchini Israel kuhusu mageuzi hayo, ambayo yanalenga kupunguza mamlaka ya Mahakama ya Juu.

    Kura hiyo - inayotarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu - itakuwa sawa na mvutano kati ya muungano wenye msimamo mkali wa kidini-kitaifa na makundi ya jamii ya Israel.

    Bunge lilianza kujadili mswada huo uliokuwa na upinzani mkubwa siku ya Jumapili.

    Siku chache zilizopita zimeshuhudia makumi ya maelfu ya waandamanaji wakiandamana kutoka Tel Aviv hadi Jerusalem kupinga mabadiliko ya mfumo wa haki, huku watu wakijaza barabara kuu.

  2. Vita vya Ukraine: Urusi inaishutumu Ukraine kwa shambulio la ndege zisizo na rubani mjini Moscow

    Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilisema kwamba Ukraine ilijaribu kufanya shambulizi "kwenye vitu kwenye eneo la Moscow" kwa msaada wa magari mawili ya anga ambayo hayakuwa na rubani.

    Meya wa Moscow Sergei Sobyanin alisema katika telegramu yake kwamba siku ya Jumatatu asubuhi mji huo ulishambuliwa na ndege zisizokuwa na rubani.

    "Leo, karibu saa 4 asubuhi, mashambulio ya ndege zisizo na rubani kwenye majengo mawili yasiyo ya makazi yalirekodiwa. Hakuna uharibifu mkubwa au majeruhi," Sobyanin aliandika.

    Vituo vya telegramu pia huchapisha video zinazoonyesha moshi ukipanda kutoka kwa majengo ya juu huko Moscow, pamoja na ndege inayoruka juu ya jiji kwa kelele kubwa.

    Hapo awali, msemaji wa huduma za dharura aliliambia shirika la habari la TASS kwamba moja ya ndege zisizo na rubani ziligonga jengo la kituo cha biashara, na mabaki ya ya pili yalipatikana karibu na jengo la Wizara ya Ulinzi ya Urusi katikati mwa Moscow

    Jeshi la Ukraine halikutoa maoni yoyote kuhusu shambulio hilo la ndege zisizo na rubani.

    Urusi ilidai kuwa ndege hizo zilidunguliwa.

    Shirika la habari la Reuters lilichapisha picha kutoka katikati mwa jiji la Moscow, ambapo ndege mbili zisizo na rubani zilidunguliwa, kulingana na maafisa wa Urusi.

    Vita vya Ukraine: Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  3. Chama cha Kihafidhina nchini Uhispania chakosa ushindi mkubwa

    Kiongozi wa chama cha upinzani cha kihafidhina nchini Uhispania Alberto Núñez Feijóo amedai ushindi katika uchaguzi wa ghafla, lakini bila matokeo aliyohitaji.

    Hata baada ya kuungwa mkono na mrengo wa kulia, chama chake cha Popular Party (PP) kimepungukiwa na wingi wa wabunge bungeni.

    Shangwe katika kambi pinzani ya Usoshalisti zilikuwa kubwa kama vile Waziri Mkuu wa Kisoshalisti Pedro Sánchez alivyotangaza: "Kambi ya upinzani imeshindwa."

    Ingawa wote wanaweza kudai mafanikio, Uhispania imesalia na matokeo ambayo hayajakamilika.

  4. Vita vya Ukraine: Urusi yashambulia Odesa baada ya kujiondoa katika makubaliano ya nafaka

    Maisha mafupi, na dosari zake, lakini nuru pekee ya kidiplomasia iliosalia katika giza la uvamizi wa Urusi.

    Ilikuwa imeruhusu Ukraine kuuza nje nafaka yake kwa ulimwengu kupitia Bahari Nyeusi.

    Ikiwa theluthi moja chini ya usafirishaji wa kawaida, lakini bado tani milioni 33. Hata hivyo, katika miezi ya hivi karibuni, hali ilikuwa imezorota.

    Urusi ilishutumiwa kwa kuzuia kasi ya usafirishaji wa nafaka kupitia vizuizi vya majini na ukaguzi wa muda mrefu, na makubaliano hayo hatimaye yakaathirika.

    Wiki iliyopita Urusi ilijiondoa katika makubaliano hayo. Urusi kisha ilizindua wimbi la makombora kwenye bandari ambayo iliwahi kuahidi kuiwacha

    Mojawapo ya maeneo yalioathirika ilikuwa eneo la nafaka linalomilikiwa na mmoja wa wazalishaji wakubwa wa Ukraine, Kernel. Maafisa wanasema zaidi ya tani 60,000 za nafaka ziliharibiwa katika wiki iliyopita.

    "Tulisimamisha mauzo yetu ya nje kwa miezi miwili hadi mitatu ya kwanza ya vita," anaelezea Yevhen Osypov, Mkurugenzi Mtendaji wa Kernel.

    "Bei za mafuta na nafaka zilipanda kwa 50%, na unaweza kuona hali hiyo hiyo ikitokea tena sasa."

  5. Natumai hujambo