Vita vya Ukraine: Urusi yathibitisha kurefusha mkataba wa nafaka
Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imethibitisha kwamba mkataba wa nafaka umeongezwa muda kwa miezi miwili.
Moja kwa moja
Mafanikio ya ulinzi wa anga ya Ukraine ni mshangao usio na furaha kwa Urusi - Uingereza
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Kombora la Kinzahl
Ujasusi wa Uingereza, katika ripoti yake ya kila siku kuhusu
vita vya Urusi- Ukraine, inachambua hali katika anga, na kumalizia kwamba hivi
karibuni imekuwa na faida kidogo kwa jeshi la anga la Urusi, pamoja na. katika
maeneo ya mpaka wa Urusi yenyewe.
Maafisa wa ujasusi wa Uingereza wanasema kwamba mnamo Mei
13, 2023, magari manne ya Kikosi cha Wanaanga wa Urusi (VKS) - helikopta mbili
na ndege mbili – zilishambuliwa katika la Bryansk la Urusi (kumbuka kwamba
vyanzo vya Urusi vilitoa habari inayopingana juu ya hili, na Urusi. Wizara ya
Ulinzi haikuripoti tukio kwa ujumla).
Mnamo Mei 3, Ukraine ilitungua kombora la anga la Kinzhal
lililorushwa na Urusi kwa mara ya
kwanza. Katika siku zilizofuata, Urusi ilikuwa ikijaribu kwa uwazi kupunguza
uwezo wa ulinzi wa anga wa Ukraine ulioongezeka, lakini ilipoteza Kinzhals
chache zaidi
Kuongezeka kwa tishio la anga kwenye mpaka wa Urusi hakuwezi
lakini kuwa na wasiwasi wa kipekee kwa Vikosi vya Anga, kwani maeneo haya
hutumiwa kwa operesheni za kijeshi dhidi ya Ukraine.
Udhaifu unaoonekana wa kinzhal unaonekana kuishangaza Urusi:
Rais Putin amerudia tena kusema kwamba makombora hayo hayawezi kuzuilika.
Watoto wanane kati ya 10 wa Afrika Kusini wanatatizika kusoma wanapofikisha umri wa miaka 10
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Waziri wa elimu wa Afrika Kusini alisema matokeo ya kukatisha tamaa yanatokana na kufungwa kwa shule wakati wa janga la Covid-19.
Watoto
wanane kati ya 10 wa shule nchini Afrika Kusini wanatatizika kusoma kufikia
umri wa miaka kumi, utafiti wa kimataifa umegundua.
Afrika
Kusini iliorodheshwa ya mwisho kati ya nchi 57 zilizofanyiwa tathmini katika Utafiti wa Kimataifa wa Kusoma na
Kuandika, ambao ulijaribu uwezo wa kusoma wa wanafunzi 400,000 duniani kote
mwaka wa 2021.
Kiwango cha
kutojua kusoma na kuandika miongoni mwa watoto wa Afrika Kusini kilipanda
kutoka 78% mwaka 2016 hadi 81%.
Waziri wa
elimu nchini humo alilaumu matokeo hayo kwa kufungwa kwa shule wakati wa janga
la Covid-19.
Akielezea
matokeo hayo kuwa "ya chini na ya kukatisha tamaa", Angie Motshekga
pia alisema mfumo wa elimu nchini unakabiliwa na changamoto kubwa za
kihistoria, ikiwa ni pamoja na umaskini, ukosefu wa usawa na miundombinu duni.
Katika shule
nyingi za msingi "maelekezo ya kusoma mara nyingi huzingatia tu utendaji
wa kuzungumza, huku yakipuuza ufahamu wa kusoma na kuleta maana ya maneno
yaliyoandikwa", aliongeza.
Utafiti
ulionyesha kuwa 81% ya watoto wa Afrika Kusini hawakuweza kusoma kwa ufahamu
katika lugha yoyote kati ya 11 rasmi nchini humo.
Pamoja na
Morocco na Misri, Afrika Kusini ilikuwa mojawapo ya nchi tatu za Afrika ambazo
zilishiriki katika tathmini za kufuatilia mienendo ya kusoma na kuandika na
ufahamu wa kusoma wa watoto wa miaka tisa na 10.
Kulingana na
majaribio yanayofanywa kila baada ya miaka mitano mwishoni mwa mwaka wa shule,
utafiti mpya unaweka nchi katika jedwali la ligi ya kimataifa ya elimu.
Singapore
ilijihakikishia nafasi ya kwanza katika viwango hivyo ikiwa na wastani wa alama
587, huku Afrika Kusini ikishika nafasi ya mwisho kwa pointi 288 - chini ya Misri
iliokuwa na alama 378. Alama hizo zimewekwa dhidi ya wastani wa alama 500 za
kimataifa.
Utafiti pia ulionyesha kuwa kwa ujumla, wasichana
walikuwa mbele ya wavulana katika ufahamu wao wa kusoma katika karibu nchi zote
zilizotathminiwa, hatahivyo pengo la kijinsia limepungua katika duru ya hivi
karibuni ya majaribio.
Mapambano ya Afrika Kusini na mfumo wake wa elimu ni ya
muda mrefu, na ukosefu mkubwa wa usawa kati ya wanafunzi weusi na weupe ni
matokeo ya kutengwa kwa watoto chini ya ubaguzi wa rangi.
Elimu ni moja ya gharama kubwa zaidi za bajeti ya
serikali, ambayo huenda ikakatizwa tamaa na matokeo duni katika masomo kama
haya.
Ukosefu wa nyenzo zinazofaa za kusoma na miundombinu duni
shuleni, kama vile vyoo, kumechangia tatizo hilo.
Mackenzie :Miili 10 zaidi yagundulika kuhusiana na dhehebu tata la msitu wa Shakahola Kenya
Chanzo cha picha, EPA
Miili 10 zaidi imegundulika
katika msitu wa Kenya wa shakahola ambapo waumini wa dhehebu tata walifunga hadi
kufa ili ‘’kumuona Yesu’’ haraka .
Mchungaji wa dhehebu hilo Paul Nthenge Mackenzie anashikiliwa na ngazi za kisheria, kuhusiana na vifo
vya watu katika msitu wa Shakahola.
Zaidi ya miili mia mbili hadi sasa imekwishafukuliwa, huku polisi
wakiendelea kuchunguza vifo vya waumini hao.
Baada ya mapumziko ya siku mbili,
shughuli ya kufukua miili katika msitu huo mkubwa uliopo pwani ya
Kenya imeendelea.
Kulingana na maafisa wa uchunguzi wa maiti, miili ya watoto wawili ni
miongoni mwa ile iliyofufuliwa, na hivyo kupelekea jumla ya miili iliyopatikana
kwa sasa kufikia 211.
Wafuasi watatu wa dhehebu tata pia waliokolewa wakiwa katika mfungo wa hadi
kufa. Walikuwa katika hali mahututi na
kupelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu .
Jumla ya watu 610 wanaoripotiwa
kupotea wanasakwa katika vituo vilivyowekwa kwa ajili ya kutafuta watu wanaodhaniwa
kuwa walipotea baada ya kujiunga na dhehebu tata katika msitu wa Shakahola.
Unaweza pia kusoma:
Paul Makenzie: Mama yangu alikufa, dada yangu sijui kama yupo hai’’
Paul Mackenzie: Ni kipi kinachojulikana kuhusu kiongozi wa dhehebu la kufa njaa nchini Kenya?
Paul Makenzie: '' Alisema yeye na familia yake watakua wa mwisho kuaga Dunia na kwenda mbinguni''
Wanawake 65 watumiwa kondomu zilizotumika katika bahasha
Chanzo cha picha, WIKIPEDIA COMMONS/ANDREW OWENS
Maelezo ya picha, Waathiriwa wanadhaniwa wote walisoma shule moja ya kibinafsi
Polisi wa
Australia wanachunguza kisa kimoja baada ya wanawake wasiopungua 65 kupokea
kondomu zilizotumika kwenye bahasha
Barua hizo,
ambazo pia zilikuwa na jumbe zilizoandikwa kwa mkono, zilitumwa kwa anwani za
kusini-mashariki na mashariki mwa Melbourne.
Polisi
wanaamini kuwa waathiriwa ni sehemu ya shambulio lililolengwa.
Wanawake
wote wanaaminika walisoma shule ya kibinafsi ya wasichana ya Chuo cha Kilbreda
mnamo 1999.
Muathiriwa
wa kwanza alijitokeza mnamo Machi, na hivi karibuni waliripoti matukio kama
hayo , polisi walisema.
Gazeti la
Herald Sun la Melbourne liliripoti kwamba wanawake hao wanashuku kuwa anwani
zao zilipatikana kutoka kwa kitabu cha mwaka cha shule.
Bree Walker
aliliambia jarida hilo kuwa "hakulala" usiku alipopokea barua hiyo,
ambayo ilikuwa na "ujumbe wa picha (ulioandikwa kwa mkono) ". Baadaye
aliwasiliana na marafiki kuona iwapo walikuwa wamepokea bahasha kama hizo.
Polisi wanaamini kuwa wanawake wengi walipokea barua
nyingi, zote zikiwa na kondomu zilizotumika.
Uchunguzi unaendelea na polisi wamemtaka yeyote mwenye
taarifa kujitokeza. Wanatarajiwa kutoa Taarifa zaidi kuhusu kesi hiyo baadaye
Jumatano.
Chuo cha Kilbreda, shule ya wasichana ya Kikatoliki
inayojitegemea, ilianzishwa na Brigidine Sisters mnamo 1904 na ina wanafunzi
wapatao 900 waliosajiliwa.
Mauzo ya Man Utd : Mfanyabishara wa Qatari Sheikh Jassim afanya maboresho ya ofa kununua klabu
Chanzo cha picha, Getty Images
Mfanyabiashara maarufu
wa Qatar Sheikh Jassim bin Hamad Al Thani amefanya maboresho ya ofa yake ili aweze
kuinunua klabu ya soka ya Manchester
United.
Vyanzo vya habari
vimeiambia BBC Sport kwamba dau jipya liliwasilishwa Jumanne asubuhi huku mazungumzo na Raine Group, wanaoshughulikia mauzo yakifanyika.
Mfanyabiashara huyo wa
Qatar ambaye ni mwekezaji katika benki pamoja na Sir Jim Ratcliffe's Ineos Group ndizo pande mbili kuu zinazotazamia kuinunua
klabu hiyo ya Old Trafford.
Makundi hayo yote
mawili yaliwasilisha dau la tatu mwishoni mwa mwezi Aprili.
Inafahamika kuwa dau
jipya ambalo ni kwa ajili ya kuinunua 100%
ya klabu , litalipa deni lote na
kujumuisha pesa nyingine za kando ambazo zitaelekezwa moja kwa moja katika klabu
na shughuli za kijamii za eneo.
Familia ya Glazer ilitangaza
mwezi Novemba kuwa wanaangalia uwezekano wa kuiuzaManchester United huku waki "angalia mikakati
mbadala".
Vita vya Ukraine: Kyiv inasema imeyadungua makombora ya masafa ya hypersonic ya Urusi
Chanzo cha picha, Mitandao ya kijamii
Maelezo ya picha, Video ya vilipuzi imekuwa ikisambazwa kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii
Ukraine imesema kuwa imeyadungua makombora ya masafa ya hypersonic ya Urusi katika "shambulio lenye ukubwa wa kipekee
"yaliyokuwa yamefyatuliwa mjini Kyiv Jumanne.
Kyiv imesema mifumo ya
ulinzi ya Ukraine ilizuia makombora sita
ya masafa aina ya Kinzhal hypersonic,
ambayo Urusi ilidai yanaweza kuhimili mifumo yote iliyopo ya ulinzi wa anga.
Yalikuwa ni miongoni mwa makombora 18 ya aina tofauti yaliyokuwa
yamefyatuliwa mjini Kyiv katika kipindi
kifupi, wamesema maafisa.
Urusi inakanusha kuwa makombora yake ya Kinzhal yalizuiwa na
ilisema moja liliangamiza mfumo wa ulinzi wa anga wa Marekani wa Patriot.
Ukraine ilikanusha kauli hiyo. BBC hatahivyo haijaweza kuthibitisha
madai haya ya nchi mbili kwa vyanzo huru.
Urusi ilianza mashambulio yake ya anga katika wiki za hivi karibuni – kwa kuupiga makombora mji mkuu wa Ukraine mara
nane hadi sasa mwezi huu- kabla ya
shambulio linalotarajiwa la Ukraine.
Jumanne jioni wazairi wa ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu alisema
Moscow haijafyatua makombora mengi ya Kinzhal kama ambayo Kyiv imedai
kuyadungua.
Vita vya Ukraine: Mengi zaidi:
YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
Hujambo na karibu tena kwa matangazo yetu ya mubashara ya leo Jumatano tarehe 17.05.2023