Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Putin anaitayarisha Urusi kwa vita vya muda mrefu - ISW

Katika muhtasari wake wa hivi punde Taasisi ya Marekani ya Utafiti wa Vita (ISW) inachambua hotuba ya hivi punde zaidi ya Rais Vladimir Putin katika mkutano wa Baraza la Haki za Kibinadamu siku ya Jumatano.

Moja kwa moja

  1. Elon Musk ageuza ofisi ya Twitter kuwa 'hoteli' ya kulala kwa wafanyikazi

    BBC imepewa picha za ofisi ya Twitter ambayo imebadilishwa kuwa vyumba vya kulala, ambayo mamlaka ya San Francisco inachunguza kama uwezekano wa ukiukaji wa kanuni za ujenzi.

    Picha moja inaonyesha chumba kilicho na kitanda cha watu wawili, ikiwa ni pamoja na kabati la nguo na sapatu.

    Mfanyikazi wa zamani alisema bosi mpya wa Twitter Elon Musk amekuwa akikaa katika makao makuu tangu aliponunua kampuni hiyo.

    Mwezi uliopita alituma barua pepe kwa wafanyikazi wote wa Twitter akisema "watahitaji kujitahidi sana" ili kufanikiwa.

    Idara ya Ukaguzi wa Majengo ya San Francisco imethibitisha kuwa inachunguza ukiukaji unaowezekana kufuatia malalamiko.

    Katika tweet ambayo sasa imefutwa, Bw Musk alichapisha ujumbe kwamba atafanya kazi na kulala ofisini "hadi shirika litakaporekebishwa".

    BBC pia imepewa picha za kiti aina ya kochi kwenye Twitter zilizotumika kama vitanda.

    Chumba kingine cha mkutano kina saa ya kengele, na picha iliyowekwa juu ya kitanda kilichotengenezwa.

    "Inaonekana kama chumba cha hoteli," mfanyakazi mmoja wa zamani alisema.

    Waliendelea kusema kuwa Bw Musk hulala mara kwa mara katika Makao Makuu ya Twitter huko San Francisco.

    Hata hivyo, Twitter haikujibu mara moja ombi la maoni kutoka kwa BBC.

    Mwezi uliopita Bw Musk - ambaye alikamilisha uchukuaji wake wa kampuni ya Twitter mnamo Oktoba - alituma barua pepe kwa wafanyikazi wote katika kampuni hiyo akisema watahitaji kufanya kazi "saa nyingi kwa juhudi zao zote".

    "Matokeo bora ya kipekee pekee ndio utakaokuwa msingi wa kufaulu," aliandika.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Afghanistan: Muuaji aliuawa hadharani na babake mwathiriwa, Taliban wanasema

    Mwanamume aliyepatikana na hatia ya mauaji alipigwa risasi na babake mwathiriwa wake katika mauaji ya kwanza ya hadhara ya kundi la Taliban tangu kurejea kwao madarakani nchini Afghanistan.

    Msemaji wa Taliban alisema mtu huyo aliuawa katika uwanja wa michezo kusini-magharibi mwa jimbo la Farah.

    Baba wa mwathiriwa alimpiga risasi mtu huyo mara tatu wakati wa kunyongwa, taarifa ya baadaye kutoka kwa msemaji wa Taliban ilisema. makumi ya viongozi wa kundi hilo walihudhuria tukio hilo.

    Inakuja wiki kadhaa baada ya majaji kuagizwa kutekeleza kikamilifu kanuni za Sharia.

    Kiongozi mkuu wa kundi la Taliban Haibatullah Akhundzada alitoa amri hiyo mwezi uliopita, akiwaamuru majaji kutoa adhabu ambazo zinaweza kujumuisha kunyongwa hadharani, kukatwa viungo hadharani na kupigwa mawe.

    Lakini, uhalifu kamili na adhabu zinazolingana hazijafafanuliwa rasmi na Taliban.

    Katika siku za hivi karibuni watu amepigwa viboko hadharani -ikiwa ni pamoja na ile ya watu dazeni kabla ya uwanja wa mpira uliojaa watu katika jimbo la Logar mwezi uliopita - ni mara ya kwanza kwa Taliban kukiri hadharani kutekeleza mauaji.

    Kwa mujibu wa msemaji wao Zabihullah Mujahid, utekelezaji huo ulihudhuriwa na majaji kadhaa wa Mahakama ya Juu, wanajeshi na mawaziri wakuu - wakiwemo wa sheria, mawaziri wa mambo ya nje na wa mambo ya ndani.

    Soma:

  3. Hujambo na karibu.