Mkuu wa
Vikosi vya Wanajeshi wa Ukraine alichapisha ripoti ya asubuhi juu ya hali ilivyo
vitani.
Hapa kuna
mambo makuu aliyoangazia:
Katika
ukanda wenye uhasama mashariki na kusini, Warusi wanatumia kikamilifu ndege za
kivita na mizinga katika maeneo mengi - ili kuzuia kusonga mbele kwa askari wa Ukraine.
Mashambulizi
kama hayo yalifanywa na wanajeshi wa Urusi huko Slobozhansky, Kharkov,
Slavyansky, Donetsk, Severodonetsky, Bakhmutsky, Limansky, Avdeevsky,
Kurakhovsky, Novopavlovsky na maeneo ya Zaporozhye, ripoti hiyo inasema.
Katika eneo
la Kharkiv, juhudi kuu za wanajeshi wa Urusi zinalenga kuzuia kusonga mbele kwa
vikosi vya ulinzi kwenye mpaka wa jimbo la Ukraine.
Vikosi vya
Urusi vilifyatua risasi kwa nguvu kutoka maeneo ya makazi ya Kazachya Lopan,
Malye Prohody, Dementievka, Petrovka, Verkhniy Saltov, Rubizhnoye na Kharkov.
Katika eneo
la Donetsk, askari wa Urusi wanaendelea kuzingatia juhudi zao kuu kwenye eneo
la Severodonetsk na Bakhmut, na matumizi makubwa ya anga.
Mapigano
yanaendelea kuchukua eneo la Severodonetsk kuwa chini ya udhibiti.
Katika eneo
la Severodonetsk, askari wa Urusi walifyatua mizinga na makombora katika maeneo
ya makazi ya Lisichansk, Sirotino, Voronovo, Borovskoye, Belaya Gora,
Ustinovka, Mirnaya Dolina, Toshkovka na kuzindua mashambulizi ya anga kutoka
kwa ndege ya Su-25 karibu na Belaya Gora na Mirnaya.
Katika eneo
la Limansky, Avdievsky, Kurakhovsky, Novopavlovsky na Zaporozhye, vikosi vya
Urusi vinajaribu kuzuia kuunganishwa tena kwa wanajeshi wa Ukraine.
Katika eneo
la Liman, wanajeshi wa Urusi walizindua shambulio la anga na ndege mbili za
Su-25 karibu na kijiji cha Prishib na shambulio la kombora karibu na kijiji cha
Mayaki.
Katika eneo
la Yuzhnobuzh, Urusi inaelekeza nguvu zake katika kushikilia maeneo yaliyokaliwa
na kuzuia mashambulizi ya wanajeshi wa Ukraine.
Katika maji ya Bahari Nyeusi na Azov, juhudi kuu
za kikundi cha meli za wanajeshi wa Urusi zinalenga kuzuia shughuli za usafiri
wa raia kaskazini-magharibi mwa Bahari Nyeusi