Hakuna kizuri au matumaini katika mazungumzo ya amani-Urusi

"Kilicho chanya ni kwamba upande wa Ukraine angalau umeanza kutunga na kuweka kwenye karatasi kile inachopendekeza. Hadi sasa tulikuwa hatujaweza kufikia hilo,"

Moja kwa moja

  1. Habari za hivi punde, Marekani yatoa onyo jipya la usafiri wa Urusi

    Marekani imetoa onyo jipya la usafiri kwa Urusi ambayo inasema mamlaka "inaweza kuwatenga na kuwaweka kizuizini" Wamarekani nchini humo.

    Ikitaja uwezekano wa kuwanyanyasa raia wa Marekani, onyo hilo linarudia wito kwa Wamarekani kutosafiri kwenda Urusi au kuondoka "mara moja".

    Pia ilionya Wamarekani kuhusu "utekelezaji holela wa sheria za mitaa".

    Ushauri huo pia ulisema kulikuwa na ripoti zinazoendelea za raia wa Marekani "kutengwa na kuzuiliwa na jeshi la Urusi" wanapokuwa Ukraine, au wanapohama kwa ardhi kupitia eneo linalokaliwa na Urusi.

    "Ikiwa unataka kuondoka Urusi, unapaswa kufanya mipango peke yako haraka iwezekanavyo,"onyo hilo lilisema.

    Marekani ilisimamisha ubalozi wake na ubalozi mdogo nchini Ukraine siku chache baada ya Rais Putin kutangaza uvamizi wake.

    Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
    • SILAHA:Mzozo wa Ukraine:Makombora ya stinger na silaha nyingine kali zinazotumiwa Ukraine
    • Ahadi ya Urusi kujiondoa ni njama ya upotoshaji - Jeshi Ukraine

      Ukrainian troops east of Kyiv on 28 March

      Chanzo cha picha, Getty Images

      Mkuu wa Jeshi la Ukraine anasema ahadi ya kujiondoa ya vikosi vya Urusi imeundwa kupotosha.

      Katika taarifa ya oparesheni ya kila siku ya iliyotumwa kwenye mtandao wa Facebook, mkuu huyowa majeshi alisema vikosi vya Urusi vinaendelea kuondoka miji ya Kyiv na Chernihiv. Urusi tayari imesema inaelekeza oparesheni yake mashariki mwa eneo la Donbas.

      Jeshi la Ukraine linaamini kuwa uondoaji huo "huenda ni mzunguko wa vitengo vya watu binafsi" unaolenga kupotosha uongozi wa kijeshi wa Ukraine na kuunda "dhana potofu" kuhusu maana ya kutumwa kwao.

      Taarifa hiyo inaangazia kauli zilizotolewa na msemaji wa Pentagon, John Kirby, ambaye alisema tishio dhidi ya Kyiv lilisalia licha ya harakati za wanajeshi wa Urusi mbali na mji huo.

      Mengi zaidi

      • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
      • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
      • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
      • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
      • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
      • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
      • SILAHA:Mzozo wa Ukraine:Makombora ya stinger na silaha nyingine kali zinazotumiwa Ukraine
      • Karibu katika matangazo ya moja kwa moja leo Jumatano 30.03.2022.