Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Uvamizi wa Ukraine: Urusi yaonya kuwa itashambulia maeneo maalum mjini Kyiv

Wizara ya ulinzi ya Urusi imeonya kwamba inajiandaa kushambulia maeneo maalum katika mji mkuu wa Ukraine.

Moja kwa moja

  1. Baharia wa Ukraine huko Majorca akamatwa kwa kujaribu kuizamisha boti inayomilikiwa na bosi Mrusi kulipiza kisasi

    Mbaharia mmoja wa Ukraine amekiri kujaribu kuizamisha boti inayomilikiwa na mkuu wa kampuni ya silaha ya serikali ya Urusi, kwa lengo la kulipiza kisasi kwa uvamizi wa Ukraine.

    Boti hiyo yenye urefu wa mita 48 sawa na futi 157 inayoitwa Lady Anastasia, inayomilikiwa na mkurugenzi mkuu wa Rosoboronexport Alexander Mikheev, ilikuwa imetia nanga huko Majorca nchini Hispania wakati baharia huyo mtaalamu wa ufundi alipofungua ‘valves’ katika chumba chake cha injini.

    Alikamatwa na maafisa wa ulinzi wa raia siku ya Jumamosi na baadaye kuachiliwa kwa dhamana.

    Alimwambia jaji kwamba hajutii chochote na angeweza kufanya hivyo tena.

    Mtu huyo alisema alijaribu kuizamisha boti hiyo ya Bwana Mikheev baada ya kutazama taarifa za habari kutoka Ukraine kwenye televisheni.

    "Kulikuwa na video ya shambulio la helikopta katika jengo moja mjini Kyiv," alinukuliwa na vyombo vya habari nchini humo.

    "Walikuwa wakishambulia watu wasio na hatia."

    Siku ya Jumamosi, jengo la ghorofa ya juu karibu na uwanja wa ndege wa Zhuliany wa Kyiv lilipigwa na kombora, na kuacha shimo linalofunika angalau ghorofa tano.

    Hakukuwa na maoni ya haraka kutoka kwa Bwana Mikheev au Rosoboronexport, ambayo husafirisha bidhaa za ulinzi za Urusi, ikiwa ni pamoja na mizinga, magari ya kivita, ndege, meli, silaha na risasi.

  2. Jinsi Waukraine wanavyolinda nchi yao

    Vimiminika vinavyoweza kuwaka moto kama vile petroli na vilevi vinamwagwa ndani ya glasi na kuongezwa mafuta ya injini. Mchanganyiko huu unaitwa Molotov cocktail.

    Kipande cha nguo huwekwa ndani yake ili kuning’iniza chupa. Nguo huyeyuka ndani ya kimiminika. Mchanganyiko huu wa Molotov hufanya kazi ya kilipuzi katika kipindi cha dakika moja.

    Ni rahisi kutengenezwa na kutumiwa na wahalifu, waandamanaji, magaidi n ahata jeshi wanapopungukiwa na silaha.

  3. Habari za hivi punde, Wanajeshi wa Urusi washambulia mji wa Kherson , yasema Ukraine

    Maafisa wa Ukraine wanasema kwamba wanajeshi wa Urusi wameanza mashambulizi dhidi ya mji wa Kherson , mji wa kusini uliopo kati ya Mykolaiv na New Kakhovka.

    ‘’Kulingana na walioshuhudia , adui anaingia kutoka uwanja wa ndege kuelekea barabara kuu ya Nikolaev ", iliripoti Ukraine katika mtandao wake wa Telegram .

    Awali , BBC Ukraine iliripoti kwamba milipuko mikubwa ilisikika karibu na uwanja wa ndege wa Kherson.

    Utawala wa kijimbo wa Kherson pia uliandika katika mtandao wake wa facebook kwamba mji huo umezungukwa na wanajeshi wa Urusi lakini haujatekwa.

    Meya wa mji huo alisema kwamba jeshi la Urusi liliweka vizuizi katika barabara kuu ya kuingilia mji huo.

    ‘’Ni vigumu kusema hali itaendelea kuwa mbaya zaidi’’, Meya Igor Kolykhaye aliandika katika mtandao wa facebook , akiongezea, ‘’Kherson ni mji wa Ukraine na utasalia kuwa hivyo’’!

    ‘’Nawaomba musalie watulivu . musiende nje wakati wa kafyu. Musijiingize katika mijadala ya uchokozi na mtu yeyote na musimkasirishe adui’’, alisema Meya huyo.

  4. Msafara wa magari ya kijeshi ya Urusi wenye urefu wa kilomita 64 waelekea mjini Kyiv

    Picha za setlaiti kutoka kwa kampuni ya teknolojia ya Maxar zinasema kwamba ripoti za mapema zinazosema kwamba msafara wa magari ya kijeshi ya Urusi una urefu wa kilomita 27 sio za kweli.

    Ukweli ni kwamba msafara huo wa magari ya kijeshi una urefu wa kilomita 64, kulingana na Maxar.

    Kampuni hiyo iliongezea kwamba , picha mpya ardhini zilikuwa zinaonesha wanajeshi walio ardhini na helikopta za kutekeleza mashambulizi kusini mwa Belarus, ikiwa ni chini ya maili 20 kutoka mpaka wa Ukraine.

  5. Natumai hujambo. Zifuatazo ni habari za moja kwa moja kuhusu matukio tofauti duniani