Mchungaji wa kanisa la Christ Apostolic Bible katika jimbo laOgun lililopo kusini magharibi mwa Nigeria
anaendelea kushikiliwa mahabusu tangu Ijumaa, baada ya kudaiwa kumbaka msichana
wa miaka 16 .
Polisi katika jimbo la
Ogun wanaochunguza tukio hilo wanasema mchungaji huyo alipanga na mke wake
kumbaka msichana huyo ambaye ni mwanakwaya katika kanisa lao.
Lakini Mchungaji Peter Taiwo na mke wake wamekuwa wakikwepa
kueleza ukweli halisi wa kilichotokea.
Mchungaji huyo anasema
yeye na msichana huyo 'wamekuwa katika mapenzi na wote walipendana kimapenzi.'
"Nilimwambia aachane na mpenzi wake wa kiume na aniombe chochote
anachohitaji"
Mchungaji huyo alisema
wakati msichana alipoumia mguu, niliwasaidia wazazi wake kupata usaidizi wa
matibabu yake.
"Kuanzia siku
nilipouangalia mguu wake, msichana alianza kunitumia jumbe za mapenzi na nilikuwa
nazijibu. Bado nina jumbe katika simu yangu ," alisema Mchungaji.
‘’Tuliongea
nikamwambia hakuna kushiriki ngono pamoja lakini tumekuwa tukipendana’’,
alisema Mchungaji na kuongeza kuwa "Wakati ule tulipoanza hatukuwa na mahusiano ya kingono, lakini tulionyeshana mapenzi,"
Pasta Taiwo anasema.
Hatahivyo mchungaji anakiri kuwa waliingia katika
mahusiano ya ngono na msichana na kumfahamisha mke wake, ambaye hakuwa na la
kusema.
Akizungumza na BBC mke wa Mchungaji alisema kuwa hakuwa
anafahamu kuwa mume wake alikuwa anamtumia vibaya msichana.
-
Mchunguaji na mkewe washutumiwa kumbaka msichana wa miaka 16