Aung San Suu Kyi anatunzwa vyema: Jeshi Myanmar
Jeshi la Myanmar limeambia BBC kwamba mamlaka haimtelekezi kiongozi aliyeondolewa madarakani Aung San Suu Kyi.
Kiongozi huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 76- hajaonekana hadharani tangu mapinduzi ya kijeshi ya Februari yaliyomuondoa mamlakani .
Mahojiano ya BBC na msemaji wa jeshi Meja Jenerali Zaw Min Tun yanakuja baada ya kuachiliwa kwa mwanahabari wa Marekani Danny Fenster ambaye alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka 11 gerezani.
Makumi ya wanahabari na maelfu ya watu wamezuiliwa tangu mapinduzi hayo yalipofanyika.
Meja Jenerali Zaw Min Tun amesema Bi. Suu Kyi anatunzwa vizuri kizuizini.
"Namaanisha tulimuacha aishi na watu wake kwenye nyumba ingawa yuko chini ya kizuizi cha nyumbani," alisema. "Tunajaribu tuwezavyo kwa ajili yake, kile anachotaka au chochote anachotaka kula.
Bi Suu Kyi ameshtakiwa kwa kuvunja sheria rasmi ya siri ya enzi ya ukoloni. Pia anakabiliwa na mashtaka ya ufisadi na kumiliki mazungumzo haramu.
Siku ya Jumanne, vyombo vya habari vya serikali viliripoti kwamba alikuwa anakabiliwa na shtaka la ziada: udanganyifu katika uchaguzi, unaohusiana na uchaguzi wa 2020 ambapo chama chake kilishinda kwa kishindo.
Amefikishwa mahakamani lakini hajatoa tamko lolote kando na maonyesho hayo mafupi.
Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuachiliwa kwake.