Paul Rusesabagina: Mzozo wa kidiplomasia waibuka baina ya Rwanda na Ubelgiji

Ubelgiji na Marekani zimepinga hukumu ya kifungo cha miaka 25 jela iliyotolewa na mahakama ya Rwanda dhidi ya Paul Rusesabagina zikisema "hakupewa haki ya kisheria ", huku Rwanda ikiyataja madai hayo ya Ubelgiji kama "dharau " na kuamua kusitisha mkutano uliotarajiwa kuzikutanisha pande mbili.

Moja kwa moja

Ambia Hirsi

  1. Biden: Ulimwengu unakabiliwa na nyakati zenye maamuzi magumu

    Rais wa Marekani Joe Biden

    Chanzo cha picha, Reuters

    Katika hotuba yake ya kwanza katika kikao cha Umoja wa mataifa rais wa Marekani Joe Biden ametoa wito wa ushirikiano katika kile alichokitaja kuwa nyakati za ‘maamuzi magumu kwa ulimwengu’.

    Hakikisho lake linajiri huku kukiwa na wasiwasi na washirika kuhusu hatua ya taifa hilo kuondoa majeshi yake Afghanistan na mgogoro mkubwa wa kidiplomasia na Ufaransa kuhusu mkataba wa manowari.

    Marekani pia imetangaza kwamba itaongeza maradufu ahadi yake ya ufadhili wa mabadiliko ya tabia nchi kufikia 2024.

    Akithibitisha kuunga mkono demokrasia na diplomasia , Bwana Biden alisema: Tunapaswa kufanya kazi kwa pamoja kama vile ambavyo haijawahi kutokea.

    Kikao hicho cha 76 cha Umoja wa mataifa kinafanyika huku kukiwa na mgogoro wa tabia nchi na mlipuko wa corona , yote yakiwa ni matatizo ambayo yameugawanya ulimwengu.

    Ameahidi kuongeza ufadhili wa mabadiliko ya tabia nchi ili kufikia $11.4bn (£8.3bn) kufikia 2024.

  2. Mahakama: Urusi ilihusika na mauaji ya Alexander Litvinenko

    Alexander Litvinenko

    Chanzo cha picha, Reuters

    Urusi ilihusika na mauaji ya Alexander Litvinenko, Mahakama ya Haki za Binadamu ya Ulaya (ECHR) imebaini.

    Litvinenko, jasusi wa zamani wa Urusi ambaye baadaye akawa raia wa Uingereza, alipewa sumu aina ya polonium-210 jijini London mwaka 2006.

    Uchunguzi uliofanyika miaka 10 baadaye ulihitimisha kuwa mauaji pengine ''yaliidhinishwa'' na rais wa Urusi, Vladimir Putin.

    Urusi mara zote imekuwa ikikanusha madai ya kuhusika na mauaji.

    Uchunguzi wa jopo la Uingereza lilisema kuwa mlinzi wa KGB Andrei Lugovoi na raia mwingine wa Urusi, Dmitry Kovtun kwa makusudi walimpa sumu Bw. Litvinenko, pengine kwa kuweka kitu chenye sumu ya mionzi kwenye chai yake.

    Ilihitimisha kuwa kutokukana kwa Urusi kuhusu madai kwamba ilikuwa imepanga mauaji hayo kulionesha serikali ya nchi hiyo kuwajibika.

    Bw. Lugovoi na Kovtun wamekana kuhusika na tukio hilo.

  3. Wabunge nchini Libya waidhinisha kura ya kutokuwa na imani na serikali

    Bunge la Libya limepitisha kura ya kutokuwa na imani na serikali ya mpito ya nchi hiyo.

    Utawala - unaoongozwa na Waziri Mkuu Abdulhamid Dbeibah - uliwekwa madarakani mapema mwaka huu kama sehemu ya juhudi za kuleta amani zilizosimamiwa na Umoja wa mtaifa

    Serikali hiyo ilitazamiwa kutoa nafasi ya uchaguzi utakaofanyika mwezi Disemba.

    Lakini hali ya taharuki imeibuka baina ya kambi mbili hasimu baada ya spika wa bunge - ambalo makao yake yako mashariki mwa Libya - kuridhia sheria tata ya uchaguzi.

    Wengine waliona hatua hiyo ni ya kumpendelea kamanda wa makao ya mashariki, Jenerali Khalifa Haftar.

  4. Mapinduzi yaliyotibuka Sudan: Serikali yawalaumu wandani wa Bashir

    Kiongozi wa Sudan

    Chanzo cha picha, AFP

    Sudan inasema watu walio na uhusiano na Rais Omar al-Bashir aliyeng'olewa madarakani wamehusika na jaribio la mapinduzi lililotibuka Jumanne.

    Msemaji wa serikali alilaumu "nguvu za giza" akiongeza kuwa wale waliohusika wamekamatwa.

    Bashir, ambaye amekuwa madarakani kwa miongo mitatu aling'olewa uongozini miaka miwili iliyopita.

    Utawala wa sasa- unaojumuisha jeshi, wawakilisha wa kijeshi na makundi ya waandamanaji - ulibuniwa kama sehemu ya makubaliano ya ugawanaji mamlaka.

    Wapangaji wa mapinduzi walijaribu kuchukua jengo la utangazaji la shirika la habari la serikali, Shirika la habari la AFP linaripoti.

    Ripoti za awali kutoka mji mkuu wa Khartoum ana mji ulio karibi wa Omdurman izilielezea shughuli nyingi za kijeshi katika kanda ya mto Nile na daraja kuu la kuvuka mto Nile lilikuwa limefungwa.

    Barabara ya kuelekea Khartoum na bandarini pia imefungwa.

    "Haturudi nyuma... kuna watu wanajaribu kuturudisha nyuma," alisema Waziri wa Habari Hamza Baloul katika taarifa iliyosomwa katika televisheni ya kitaifa TV, ikilaumu "mabaki" ya utawala wa zamani kwa kuhusika na jaribio la mapinduzi ya Jumanne.

  5. Man United kuwauza wachezaji saba Januari 2022

    Lingard

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Manchester United wanajiandaa kuwauza wachezaji wake saba mwezi Januari 2022, ikiwa dirisha la uhamisho wa wachezaji Ulaya likafunguliwa.

    United imekusanya wachezaji wengi sana hivi kwamba inabidi wawachilie wengine, vinginevyo kulipa mishahara kunaweza kuwaingiza katika changamoto ya kiuchumi.

    Kulingana na gazeti The Sun, United litawauza wachezaji Donny van de Beek, Jesse Lingard, Phil Jones, Eric Bailly, Anthony Martial, Diogo Dalot na Alex Telles.

    Klabu hiyo pia itawakopesha wachezaji wa juu kwa vilabu vya juu ili kuboresha ujuzi wao.

    Lakini, United inajitahidi kumshawishi Paul Pogba abaki Old Trafford, huku mkataba wake ukimalizika mwishoni mwa msimu ujao.

    Pogba ananyatiwa na vilabu kadhaa ikiwemo klabu yake ya zamani Juventus, Real Madrid na Paris St Germain, kulingana na ripoti.

    Hata hivyo kujumuishwa kwa jina la Jesse Lingard kwenye orodha ya uhamisho ya United mnamo Januari ni hatua ya kushangaza baada ya Ole Gunnar Solskjaer kudokeza kuwa anataka mchezaji huyo wa kimataifa wa England abaki Old Trafford.

  6. Karibu tani tatu za heroine zakamatwa katika bandari ya Gujarat

    The shipment was seized at Gujarat's Mundra port

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maafisa wa ujasusi wa kupambana na magendo wamekamata karibu tani tatu za heroin - ambayo inasemekana kuwa ya thamani ya karibu dola biioni 2.7 (£ 1.9bn) - katika operesheni kubwa katika bandari ya Gujarat.

    Uchunguzi wa bado unaendelea kubaini thamani ya dawa zilizokamatwa, maafisa wameiambia BBC.

    Watu wawili wamekamatwa na wengine kadhaa wanachunguzwa, taarifa imesema.

    Shehena hiyo imetoka Afghanistan, ambapo iliwasilishwa kama mawe ya thamani ya talc.

    Ilisafirishwa katika bandari ya Mundra katika jimbo la Gujarat kutoka Iran.

    Kurugenzi ya Upelelezi ya Mapato (DRI) ilisema kwamba ilipokea ujasusi kwamba shehena kutoka Bandari ya Bandar Abbas nchini Iran ilishukiwa kuwa na dawa za kulewesha.

    Ilisema ujasusi pia ulibaini kwa shehena hiyo ilikuwa ikiingiizwa nchini na kampuni kutoka mji wa kusini wa Vijaywada.

    "Wakati maafisa wetu walipozuilia shehena hiyo na kuichunguza shehena hiyo, bidavya zilipatikana katika kontena hizo na uwepo wa dawa aina ya heroin ulithibitishwa," taarifa ya DRI ilisema.

    Maafisa walisema upekuzi umefanywa katika miji kadhaa kote India, pamoja na mji mkuu wa kitaifa, Delhi, Ahmedabad na Chennai.

    "Uchunguzi uliofanywa hadi sasa pia umebaini kuhusika kwa raia wa Afghanistan, ambao wanachunguzwa," limesema shirika hilo.

  7. Hali nchini Sudan yadhibitiwa - vyombo vya habari vya serikali

    Baraza la mawaziri nchini Sudan limeripoti kuwa hali "imedhibitiwa" baada ya jaribio la mapinduzi, Shirika la habari la serikali la Suna limeripoti.

    Wale waliohusika na jaribio hilo la mapinduzi wanazuiliwa na uchunguzi dhidi yao unaendelea, iliongeza.

    Majaribio kadhaa ya mapinduzi yamefanyika nchini Sudan tangu Omar al-Bashir alipoondolewa madarakani mwaka 2019 na jeshi kuchukua uongeza.

    Wakosoaji wanadai usalama uliopo sasa katika sehemu za nchi ni jaribio la wanajeshi kuzuia uhamishaji wa uongozi wa Baraza Kuu la Nguvu dhidi ya raia.

    Uhamisho wa madaraka umepangwa Novemba.

    • Urusi ilihusika na mauaji ya Litvinenko - Mahakama ya Ulaya

      Alexander Litvinenko pictured in hospital after being poisoned

      Chanzo cha picha, Getty Images

      Urusi ilihusika na mauaji ya Alexander Litvinenko, Mahakama ya Ulaya ya Haki za Binadamu imebaini.

      Bwana Litvinenko, jasusi wa zamani wa Urusi ambaye alikuwa raia wa Uingereza, aliuawa kwa sumu polonium mwaka 2006 mjini London.

      Uchunguzi wa uma uliofanywa na Uingereza mwaka 2016 alihitimisha kuwa mauaji "labda yameidhinishwa" na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

      Urusi inapinga kuhusika na kifo chake.

      Uchunguzi wa Uingereza ulisema mlinzi wa zamani wa KGB Andrei Lugovoi na Mrusi mwingine , Dmitry Kovtun walimtilia sumu kimaksudi Bwana Litvinenko katika kinywaji chake

      "Mahakama ili baini haswa kwamba kulikuwa na kesi kubwa... katika kutiliwa sumu kwa Bw. Litvinenko, mabwana Lugovoi na Kovtun walihudumu kama maajenti wa taifa la Urusi," mahakama ya Ulaya ilisema.

      Ilihitimisha kuwa kushindwa kwa Urusi kukanusha madai kwamba ilipanga shambulio hilo inaelekeza zaidi kwa jukumu la serikali.

      Bwana Lugovoi na Bw.Kovtun imekanusha kuhusika kivyovyote na mauaji hayo.

      • Zifahamu sumu zinatumiwa na majasusi kuua watu
      • Novichok: Mambo muhimu kuhusu sumu kali ya Urusi iliyotumiwa kumshambulia jasusi
    • Paul Rusesabagina: Mzozo wa kidiplomasia waibuka baina ya Rwanda na Ubelgiji

      Rusesabagina

      Ubelgiji na Marekani zimepinga hukumu ya kifungo cha miaka 25 jela iliyotolewa na mahakama ya Rwanda dhidi ya Paul Rusesabagina zikisema "hakupewa haki ya kisheria ", huku Rwanda ikiyataja madai hayo ya Ubelgiji kama "dharau " na kuamua kusitisha mkutano uliotarajiwa kuzikutanisha pande mbili.

      Bwana Rusesabagina ambaye ni mzaliwa wa Rwanda, mwenye umri wa miaka 67, ana uraia wa Ubelgiji na ana kibali cha nchini Marekani

      Katika tangazo aliolitoa Jumatatu Naibu Waziri Mkuu wa Ubelgiji ambaye pia ni waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Sophie Wilmès amesema kuwa alipata taarifa kuwa hukumu ya Rusesabagina imetolewa mjini Kigali na kuoneza kuwa :"Kuanzia mwanzo wa kesi hii na japokuwa Ubelgiji imekuwa ikiendelea kuomba masuala kadhaa yafanyike, inaonyesha kuwa kesi ya Rusesabagina haikuendeshwa mahakamani kwa njia iliyo ya uwazi na haki kisheria, hususan kuhusu haki yake ya kujitetea".

      Bi Wilmès amesema, serikali ya Rwanda imesema kuwa mkutano wa kando ambao ulitakiwa kuzikutanisha pande mbili wakati wa Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa mjini New York "hautafanyika".

      • Rusesabagina ahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela
      • Utata juu kukamatwa kwa 'shujaa' wa filamu ya mauaji ya Rwanda.
      • Paul Rusesabagina: Rwanda yakiri kuwa 'iliilipa ' ndege iliyomtoa Dubai na kumpeleka Kigali, bila kujua
      • Watoto wa Rusesabagina wadai baba yao anaamriwa cha kuzungumza na kuwa alikataliwa kuwa na wanasheria huru
      • Wanaolimpiki wa Uganda wapandishwa vyeo katika jeshi la polisi

        Gold medallist Chemutai Peruth made police inspector

        Chanzo cha picha, Getty Images

        Maafisa wanne wa polisi walioiwakilisha Uganda katika michezo ya Olimpiki wamepandishwa vyeo na na inspekta jenerali.

        Mshindi wa nishani ya dhahabu Chemutai Peruth amepandishwa cheo kutoka askari wa kawaida hadi inspekta wa polisi.

        Mwanaolimpiki Chelangat Mercyline amepandishwa daraja kutoka cheo cha naimbu inspekata hadi inspekta.

        Chemutai Immaculate amepandishwa cheo kutoko koplo hadi sajenti naye Shida Renny akipandishwa cheo kuwa koplo kutoka askari wa kawaida.

        Cheo cha mshindi wa dhahabu Cheptegei Joshua na mkufunzi wake Njia Benjaminkutoka inspekta hasi naibu mkuu wa polisi kinafuatiliwa.

        Inspecta jenerali amesema wanariadha hao "wanatuzwa kwa mafanikio makubwa na furaha waliyoileta taasisi hiyo na nchi".

        Rais wa Uganda Yoweri Museveni alisema mwezi Augosti kwamba wanariadha walioshinda medali katika michezo ya Olimpiki mjini Tokyo watapewa magari na nyumba.

      • Milipuko ya gurunedi yakumba Bujumbura

        Idadi ya watu wasiojulikana huenda wamejeruhiwa katika shambulio la gurunedi usiku wa Jumatatu katika mji mkuu wa kibiashara wa Bujumbura nchini Burundi.

        Walioshuhudia tukio hilo wanasema milipuko miwili mikubwa ilisikika baada ya gurunedi mbili kulipuka katika kituo cha mabasi kilicho na shughuli nyingi, Damu ilionekana katika eneo la tukio .

        Wanasema maafisa wa polisi walifika haraka katika eneo hilo.

        Milipuko miwili zaidi iliripotiwa , moja katika mtaa maaarufu wa Bwiza ambako guruneti ilirusha katikakati ya wauza samaki.

        Mashuhuda wanasema kuna watu huenda wamefariki na wengine wengi kujeruhiwa. Polisi hawajatioa tamko lolote kuhusiana na mashambulio hayo.

        Hakuna kundi lolote lililojitangaza kuhusika shambulio hili lililotokea siku kadhaa baada ya Rais Evariste Ndayishimiye kusafiri New York ambako anatarajiwa kuhudhuria kikao cha 76 cha mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa.

      • Habari za hivi punde, Jaribio la mapinduzi Sudan latibuka-Mamlaka

        TL

        Chanzo cha picha, AFP

        Serikali ya Sudan inasema kumekuwa na jaribio la mapinduzi lililotibuka katika nchi hiyo na hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo, vyombo vya habari vya serikali vinaripoti.

        "Kumekuwa na jaribio la mapinduzi lililoshindwa, watu wanapaswa kukabiliana nalo, "Shirika la habari la AFP linanukuu ripoti zikisema.

        Kulikuwa na jaribio la kuchukua jengo ambalo lina vyombo vya habari vya serikali, Shirka la habari la AFP linasema likiashiria chanzo cha serikali.

        Msemaji wa serikali amesema shughuli ya kuwahoji wanaoshukiwa kuwa nyuma ya jaribio hilo la mapinduzi itaanza muda mfupi ujao.

        Msemaji huyo aliyenukuliwa na mashirika ya habari ya kimataifa anasema wapangaji wa mapinduzi walijaribu kuchukua udhibiti wa redio ya Serikali huko Omdurman, ng'ambo ya mto Nile kutoka mji mkuu Khartoum.

        Maandamano yalikuwa yamepangwa kufanyika mjini Khartoum leo na wanajeshi walikuwa wametumwa kushika doria mitaani wakati mapinduzi hayo yalipojaribiwa.

        Serikali ya mpito ya Sudan ambayo imekuwepo tangu 2019 imekuwa ikikabiliwa na shinikizo la kuleta mageuzi ya kiuchumi na kisiasa licha ya madai yanayokinzana kutoka kwa maeneo ya kihafidhina na yale huria.

      • Uchaguzi wa Canada: Trudeau asalia madarakani lakini akosa kura ya wengi

        Justin Trudeau

        Chanzo cha picha, Getty Images

        Baada ya wiki tano za kampeni, bunge lililochaguliwa na Wacanada wakati huu linaonekana sawa na lilie walilopigia kura mwaka t2019.

        Justin Trudeau amesalia madarakani lakini anakosa wingi wa wajumbe Chama cha Conservative kimeshinda kura ya wengi lakini kimekosa viti vya kutosha kumuondoa madarakani Trudeau wa chama cha Liberal.

        Ijapokuwa matokeo yataendelea kuwasilishwa katika siku zijazo wakati maafisa wa uchaguzi wanaendelea kujumuisha kura zilizopigwa kwa njia ya posta, hakuna kinachokadiriwa kubadilisha matokeo jumla ya uchaguzi.

        Trudeau aliangazia hatua hiyo kama ushindi katika hotuba kwa wafuasi mapema Jumanne, akiwaambia kuwa "tulichoona usiku wa leo ni mamilioni ya Wakanada [ambao] wamechagua mpango wa maendeleo"

      • Marekani yataka Rais wa Somalia na Waziri Mkuu kutatua tofauti zao

        Rais Mohamed Farmajo na Waziri Mkuu Hussein Roble hawajakubaliana juu ya uteuzi muhimu

        Chanzo cha picha, Reuters

        Maelezo ya picha, Rais Mohamed Farmajo na Waziri Mkuu Hussein Roble hawajakubaliana juu ya uteuzi muhimu

        Marekani imetoa wito kwa Rais wa Somalia na Waziri Mkuu kutatua tofauti zao kwa ajili ya ustawi wa nchi.

        Ilisema ushirikiano wa viongozi wa Somalia, hususan Rais Mohamed Abdullahi Farmajo na Waziri Mkuu Hussein Roble, ni muhimu kwa nchi "kukamilisha haraka mchakato wake unaoendelea wa uchaguzi".

        Mzozo kati ya viongozi hao wawili, uliosababishwa na jinsi serikali ilivyoshughulikia kesi ya jasusi aliyepotea, umezua hofu kwamba mchakato wa uchaguzi wa Somalia unaweza kukumbwa na changamoto nyingi.

        Mzozo uliongezeka wiki iliyopita baada ya rais kusimamisha mamlaka ya Utendaji wa Bw Roble, hatua iliyotajwa na waziri mkuu kuwa "haramu".

        ''Tunatoa wito kwa Rais na Waziri Mkuu waepuke matamko au vitendo vya uchochezi na kusuluhisha kutokubaliana kwao juu ya uteuzi wa wafanyikazi na mamlaka zao kwa amani,” taarifa ya msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Ned Price ilisema.

        Taifa hilo la Pembe la Afrika limepangwa kufanya uchaguzi wa bunge moja kwa moja kati ya 1 Oktoba na 25 Novemba.

        Marekani inasema kuwa kuchelewesha zaidi kwa uchaguzi kunaweza kuongeza "uwezekano wa vurugu na kutoa nafasi kwa al-Shabab na vikundi vingine vyenye msimamo mkali kusambaratisha nchi".

      • Raia wanalengwa katika vita vya Tigray-Tume ya Haki Ethiopia

        th

        Chanzo cha picha, AFP

        Tume ya Haki za Binadamu ya Ethiopia imeibua wasiwasi juu ya raia kuuawa kwa makusudi katika mzozo wa serikali kuu ya Ethiopia na wapiganaji wa jimbo la Tigray.

        Mapigano yameenea katika wiki za hivi karibuni kwa mikoa ya karibu huku wakaazi wakishutumu waasi wa Tigray kuharibi maeneo ya kidini yenye umuhimu mkubwa kwa imani zao, kuua raia, kupora vituo vya afya na shule, na kupeleka mamia ya maelfu ya watu kukimbia kutoka kwa nyumba zao.

        Mzozo huo umekuwa ukiendelea tangu Novemba mwaka jana wakati waziri mkuu Abiy Ahmed alipotangaza vita dhidi ya kundi la TPLF akilishtumu kwa kushambulia kambo ya kijeshi ya serikali kuu .

        Tayari mashirika ya misaada yamesema kuna janga kubwa la baa la njaa na misaada ya kibinadamu inahitajika katika maeneo yote ya nchi hiyo yanayokumbwa na mzozo huo .

      • Dada kutoka Japan wasajiliwa katika kitabu cha Guinnes kama pacha wakongwe zaidi duniani

        ad

        Chanzo cha picha, GUINNESS WORLD RECORDS

        Dada wawili wa Kijapani wamethibitishwa na kitabu cha rekodi za dunia cha Guinness World Record kama mapacha wazee zaidi wanaofanana duniani kwa zaidi ya miaka 107 na siku 300.

        Umeno Sumiyama na Koume Kodama wamevunja rekodi iliyowekwa na dada mapacha wa Japani Kin Narita na Gin Kanie.

        Umeno na Koume, wote waliofafanuliwa kama watu wenye kupenda kutangamana na wengine, walizaliwa mnamo Novemba 5, 1913 kwenye kisiwa cha Shodoshima.

        Tangazo hilo lilitolewa Jumatatu kwendana na ‘Siku ya Wazee’ - likizo ya kitaifa huko Japani.

        Kwasababu ya hali ya sasa na Covid-19, na kama tahadhari, akina dada hao - ambao wanaishi katika sehemu tofauti za Japani - walitumiwa vyeti vyao rasmi kuwasilishwa na wafanyikazi katika nyumba zao tofauti za utunzaji.

        Wamiliki wa rekodi za awali Kin na Gin walikuwa wameshikilia jina la mapacha wazee zaidi duniani wanaofanana katika kipindi cha miaka 107 na siku 175 tangu kifo cha Kin mnamo Januari 2000.

        Gin alifariki dunia mwaka uliofuata, akiwa na miaka 108. Mapacha hao marehemu, ambao majina yao yanamaanisha dhahabu na fedha kwa Kijapani, walikuwa wamezaliwa Agosti mosi, 1892 huko Nagoya, na walikuwa watu mashuhuri kwa vyombo vya habari katika kipindi cha muongo wao wa mwisho.

        Familia ya Umeno na Koume walisema kwamba dada wote wawili walikuwa wamefanya utani juu ya kufikia umri wao.

        Japani, matarajio ya maisha ni ya juu zaidi ulimwenguni, na watu wazee wanapewa heshima kubwa.

        Mtu mzima mkongwe aliyerekodiwa, kulingana na kitabu cha Guinness, ni mwanamke wa Kijapani mwenye umri wa miaka 118 Kane Tanaka.

      • Kesi ya rushwa dhidi ya Jacob Zuma kuendelea leo

        JZ

        Chanzo cha picha, AFP

        Kesi ya rushwa inayomhusisha rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma inapaswa kuanza tena leo.

        Kesi hiyoimecheleweshwa mara kwa mara, hivi karibuni kwa sababu Bwana Zuma alikuwa amelazwa hospitalini kwa hali ya kiafya isiyojulikana.

        Rais huyo wa zamani amekanusha madai hayo, na anasisitiza kuwa maadui zake wa kisiasa wanatumia korti kumlenga. Kukamatwa kwake kulisababisha wiki kadhaa za machafuko nchini humo na kusababisha uporaji wa mali na maafa .

      • Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya moja kwa moja hivi leo Jumanne tarehe 21 Septemba 2021