Beckham aitaka Man Utd konyesha 'motisha'

Chanzo cha picha, Getty Images
David Beckham amewataka wachezaji wa Manchester United kuthibitisha kuwa wana ari ya kuichezea klabu hiyo yenye matatizo.
Nyota wa zamani wa United, Beckham alikuwa Manchester siku ya Alhamisi kuhudhuria onyesho la kwanza la filamu mpya kuhusu timu iliyoshinda mara tatu mwaka wa 1999.
Beckham alikuwa mchezaji muhimu katika timu ya United ambayo ilishinda Ligi ya Premia, Ligi ya Mabingwa na Kombe la FA chini ya kocha mkuu Alex Ferguson .
Meneja wa United Erik ten Hag anapambana kukwepa kufukuzwa huku timu yake ikilala katika nafasi ya nane kwenye Ligi ya Premia baada ya Jumatatu kupoteza kwa aibu 4-0 dhidi ya Crystal Palace.
Beckham anaamini wachezaji lazima wachukue sehemu yao ya lawama, akisema: "Unatumai kwamba meneja hafai kufanya mengi. "Nadhani hiyo ndiyo maana kamili ya kuwa mchezaji wa Manchester United na kucheza katika michezo hii mikubwa - unapaswa kuwa na motisha."
Msimu mgumu wa Ten Hag wa pili kuinoa unaweza kukombolewa ikiwa United watawashinda wapinzani wao Manchester City kwenye fainali ya Kombe la FA.
Unapokuwa mchezaji wa kulipwa na unafanya kazi unayoipenda na uko kwenye klabu unayoipenda, unapocheza katika mchezo wowote, iwe ni mchezo wa kawaida wa msimu au ikiwa ni fainali ya Kombe la FA dhidi ya wapinzani wako, hiyo inapaswa kuwa motisha tosha," alisema.











